KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Wednesday, July 30, 2014

WAISLAMU WATAKIWA KUWA NA UMOJA UTENGANO UNA LETA MADHARA IKWA PAMOJA NA VITA


Waislamu Mkoani Ruvuma wametakiwa kuwa na umoja na kufuata Mambo mazuri ambayo hayawezi kuiweka Nchi Mahali pabaya, Umoja Mshikamano na kuaminiana ndiyo silaha ya kuweza kuendeleza Amani.

Mataifa ya Waarabu yameingia katika Vita na kukosa Amani kutokana na Unafiki na kuyajali Mataifa makubwa. Hayo yamesemwa katika kusherehekea Sikukuu ya Iddi Fitri Mjini Songea.

Sheikh Shaban Chitete wa Masijidi Huda amesema endapo Waislamu watakuwa wanafiki basi huo ndio utakuwa mwanya wa watu wabaya kupata nafasi ya kuwagombanisha, amesema katika kuitafuta Katiba Mpya Wabunge tuliowachagua wamejigawa na kujiita Ukawa hiyo ni kutaka kufuja Fedha za Wananchi .

Waumini wa Dini ya kiislam Katika Misikiti mbalimbali ya Manispaa ya Songea wamemuomba Mungu aendekeze Amani na Utulivu tulionao na kuwaombea wale wenye nia ya kutaka Taifa la Tanzania liwe na Mfarakano washindwe. Alahamdulilahi Labiramina,

Katibu wa BAKWATA Mkoa wa Ruvuma Mauridi Hassan Said ameiomba Serikali kuangalia upya kuhusu Ujenzi wa Mabucha ya Nguruwe, kuweka Mabucha ya Nguruwe hadharani kama ilivyo katika Soko la Mazao SODECO ni kuwadhalilisha Waislam. Waislamu wanashindwa kununua bidhaa katika Soko la SODECO kutokana na Mabucha ya Nguruwe kuwa wazi wazi.
Sheikh Shabani Chitete akiwa katika membali ya Masijid Huda Mabatini akitoa Hotuba ya Sikukuu ya Iddi Fitiri
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu amewataka Waislamu kuwaimarisha watoto katika kujiendeleza kielimu

Katibu wa BAKWATA amesema katika kuendeleza Elimu kila Msikiti utakuwa na Shamba la zao la chakula, pia kila Msikiti utakuwa na Orodha ya Waislam na orodha zao kila msikiti uhakikishe una ekari mbili za miti ili kulinda mazingira.
Wanafunzi wa Shule ya wasichana Songea wakiwa nje ya Msikiti wa Masijidi Huda wakifurahia Iddi Fitiri
Mzee na Familia yake wakitoka kuswali katika msikiti wa Huda Mabatini Manspaa ya Songea
                                                                swala ya iddi firiri
Iddi Mbara kwa waislamu, wahimizwa kuwa na upendo wenyewe kwa wenyewe
waumini wa msikiti wa mjini kati wakiwa katika dua la kupombea amani Serekari ya Tanzania

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu ameyasema hayo katika Baraza la Iddi lililofanyika katika ukumbi wa Songea girls. Amesema Waislamu ili kuyafikia Maendeleo ya kweli ni lazima wajidhatiti katika Elimu hasa kwa kuwaendeleza watoto wao.

Masijidi Huda katika Manisipaa ya Songea waumini wakiwa ndani ya Msikiti
Hivyo hivyo wanaume walio kosa nafasi ndani ya Msikiti wakiwa wana swali nje ya Msikiti wa Mjini kati Songea
Akina mama katika Msikiti wa Mjini Kati katika Manispaa ya Songea wakiwa wametandika Mikeka Nje baada ya kukosa nafasi ndani ya Msikiti
                               wanawake wakiwa msikiti wa mjini kati songea
Akina mama walio miminika katika Msikiti wa Masijidi Huda wakiwa Tayari kwa Swala ya Iddi

Aidha Katibu wa BAKWATA Maurid Hassan Said amesema Waislamu walio wengi ni wakulima, mwaka huu kumekuwa na Mahindi mengi. Mwaka jana Serikali ilinunua Tani 53,000 tu za mahindi. Mwaka huu Inatarajia kununua Tani 48,000  Nipungufu kuliko mwaka jana katika ununuzi. Wameiomba Serikali kuongeza ununuzi ili kuwaokoa Wananchi katika kukabiliana na Umaskini.
Waisilamu Katika Manspaa ya Songea Wakiombea Amani wakati wa Swala ya Iddi
Waisilamu wakiwa katika swala ya iddi katika msikiti wa Huda Mabatini mjini Songea

Friday, July 25, 2014

WAVUVI WA MWAMBAO WA ZIWA NYASA WAMEIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA VIFAA VYA UWOKOZI NA VIKINGA MAJI ILI KUKABILIANA NA MAJANGA YA KUZAMA ZIWANI DHORUBA INAPO TOKEA

Hiyo ni hali halisi kwa Wakazi wa Mwambao wa Ziwa Nyasa wanavyokabiliana na hali ya Majanga yanayotokea Ziwani, hakuna Uokozi wa uhakika bali kutumia zana za Asili katika kuwaokoa watu wanaopatwa na majanga katika Ziwa Nyasa.
Vijana wa uokoaji katika Mwambao wa Ziwa Nyasa wakitoka kuwaokoa Vijana wawili waliozama kwenye Maji, Yohana Behewa na john Behewa waliozama Kilindini kilometa 20 kutoka nchi kavu katika maeneo ya Kijiji cha Chiulu Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma .
Vijana wa Uokozi wakivuta Mtumbwi uliowaokoa vijana waliokuwa wamezama kutokana na kupigwa na Wimbi wakati wa Dhoruba kali wakati wakiwa Ziwani.
Hapo ni vijana waliookolewa wakiwa wamefikishwa Nchi kavu ambako walipatiwa msaada baada ya kuokolewa na vijana wenzao huku wakiwa wamechoka kutokana na kunywa  maji.
Kikosi cha ukoaji Kilichopo Kijiji cha Chiulu wakivuta mtumbwi uliobeba watu waliowakoa kutoka Ziwani baada ya kupigwa na dhoruba na kuzama majini hali iliyotokana na matumizi ya Zana hafifu ambazo hazikidhi kwa kushindana na Mawimbi makali yanayo tokana baada ya  Dhoruba kali  inapotokea katika Mwambao wa Ziwa Nyasa. Wananchi wa Mwambao wa Ziwa Nyasa wamesema hali hiyo imekuwa ikitokea mara kwa mara na hakuna njia nyingine inayotumika kuokoa wahanga wanaopatwa na kadhia hiyo zaidi ya kutumia vifaa duni walivyonavyo.
Mwambao wa Ziwa Nyasa hauna Kikosi cha Polisi cha Wanamaji wa kuweza kusaidia uokozi wa majanga yanayotokea Ziwani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msekhela amesema juhudi za makusudi zinafanywa ili kupata kikosi cha waokoaji wa Maji kwa upande wa Polisi  juhudi zinafanywa ili kupata  kikosi chja wana maji wa Jeshi la Police ,Pamoja na hilo Jeshi la Police litatoa Mafunzo kwa Vijana wanao ishi kandokando mwa Mwambao wa Ziwa Nyasa .

Wednesday, July 23, 2014

SEREKARI IMEJISAHAU VIPI HADI KULETA HOFU KWA BINADAMU WASIO NA KOSA ?



Viungo mbali mbali vya binadamu vimekutwa katika eneo la kutupa taka la Bunju mjini Dar es Salaam katika mazingira ambayo haijafahamika mara moja kuwa viungo hivyo vimetoka wapi.
Kwa mjibu wa Afisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema viungo hivyo vya binadamu vilivyokutwa ni miguu,vidole ambavyo vilikutwa vikiwa vimefungwa ndani ya mifuko.
Hata pamoja na viungo hivyo pia vifaa vya upasuaji vimekutwa zikiwemo glovuzi.
Mtu mmoja anashikiliwa kuhusishwa na tukio hilo ambaye ni dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo lililobeba viungo hivyo vya binadamu.
Haijafahamika mara moja miili hiyo ya binadamu imetolewa wapi na ilipelekwa eneo hilo kwa lengo gani.
Katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikikabiliwa na tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino ambapo viungo vyao huchukuliwa,japo kuwa viungo hivi vilivyokutwa kwa sasa bado havihusishwi moja kwa moja na matukio ya mashambulizi na mauaji ya walemavu hao

IMG-20140721-WA0008


WA MAMA WA KIPARE WATOA MSAADA KATIKA HOSPITARI YA MKOA RUVUMA

Kutoa ni moyo na si utajiri ambko kunaambatana na moyo wa huruma kwa wenye mahitaji, pichani ni Bi Swaumu akiwa katika hospitali ya Mkoa kutoa zawadi kwa wazazi waliojifungua katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma iliyopo Manispaa ya Songea zawadi ambayo japo ni kidogo imekuwa ni faraja kubwa kwa wazazi waliolazwa hospitalini hapo.
Ndugu msomaji unafahamu faida za uzazi na matatizo yanayotokana na Uzazi hasa ikiwa ukuzingatia maagizo ya wataalamu wa Afya. Huyo unayemuona ni  Muuguzi Mkuu wa Wodi ya Wazazi katika hospitali ya Mkoa akitoa Elimu ya Malezi ya watoto na kuelimisha dalili za hatari kwa watoto wachanga na wazazi waliotoka kujifungua ambazo zinapojitokeza Mzazi anapaswa awahi katika Kituo cha Afya kilicho karibu naye. Elimu hiyo alikuwa akiitoa kwa Wazazi 30 waliojifungua siku hiyo.
Wazazi pamoja na kubeba jukumu la kutakiwa kuongeza familia tunatakiwa kutambua athari za uzazi usio wa Mpango wataalamu siku zote wanashauri kuzaa kwa mpango idadi ambayo utaweza kumudu kuihudumia mahitaji ya msingi. Mama unayemuona hapo amejifungua watoto mapacha katika Hospitali ya Mkoa wa ruvuma na huo ni uzazi wake wa tano. Jee ingekuwa wewe huyo ni mkeo ungetoa ujshauri gani ili kumsaidia kiafya na Malzi bora ya Familia?
 Kikundi cha Akina Mama wa Kipare na walioolewa na wapare waishio Manikspaa ya Songea baada ya kuguswa na uchungu wa Uzazi na kwa kutambua adha wanazozipata akina mama katika uzazi waliamua kuchangishana pesa toka mifukoni na Kununu zawadi ya sabuni zenye thamani ya sh. laki mbili na kutembelea wazazi waliojifungua na wanaotarajia kujifungua na kuwafariji kwa kuwapa zawadi ya Sabuni ili iwasaidie kidogo kwa kufanyia usafi maana Mzazi anapokuwa katika hali ya kulea au kutarajia kuanza ulezi anahitaji usafi wa hali ya juu kwa usalama wa afya yhake na ya mtoto. Hapo akina mama wakiwa getini wakimsubiri muuguzi awaongoze kuelekea wodini kutimiza lengo lao.
 Siku hizi kuna watu wengi ambao wana uwezo na hujitolea sana katika starehe mfano katika Harusi, Send Of, Kitchen part na hata Majamanda sehemu ambazo watu hutoa kwa kushindana lakini wanasahau kama kuna watu wenye mahitaji ambao hawana uwezo na wanahitaji faraja. Hebu tuige mfano wa akina mama hao ambao hawana shughuli lakini wamejikuta wakiwa na huruma na kutembelea makundi maalumu kama Kituo cha watoto Yatima, na Hospitali kuwafariji wazazi wenzao na Mungu atawabariki. Jee wewe unayekesha baa na kutumia pesa nyingi au unatoa katika mambo mengine ya anasa kwa nini usitumie kiasi kingine kutoa kwa watu wasio na uwezo kama walikvyofanya wamama wa kipare waishio Songea?
 Aina Mama wakipare wakiwa na Muuguzi wa Wodi za Uzazi katika Hospitali ya Mkoa akiwaongoza kwenda kutoa kidogo walichokusudia kukitoa kwa wazazi wenzao. Jee ndugu msomaji jiulize Mungu amekupa Kipato Kiasi gani na umetumia katika kusaidia Watu gani. Na kwanini alikupa wewe na akawanyima wengine?
 Akina mama wa kipare na walioolewa na Wapare wanaoishi Manikspaa ya Songea wakiongozwa na Mama wa Nikdhamu wakifurahia kwenda kuwafariji wazazik wenzao kwa Sabunik ikiwa ni sehemu ya kuwafariji na kuwapongeza kwa kukubali kutimiza Jukumu walilojaliwa na Mwenyezi Mungu la kuongeza familia na kulea.
 Bi Fatujma Swai mmoja wa wanakikundi cha Akina mama wa kipare ambacho huwezeshana katika majanga na kufariji makundi mbalimbali yanayohitaji faraja. Hapo ni Wodi ya Wazazi wanaosubiri kujifungua wakiwapa zawadi ya sabuni ikwasaidie kidogo kwa kufulia nguo zao.
 Mzazi aliyejifungua akipokea sabuni na kushukuru kwa faraja toka kwa akina mama hao wa Kikundi cha kuwezeshana cha wapare na walioolewa na wapare waikshio Manikspaa ya Songea. Mama huyo amesema ameshukuru sana kwa moyo huo ameomba na wengine wenye nafasi waige mfano huo wa kuwakumbuka wagonjwa. Amesema kwa upande wake yeye ni mwenyeji wa Mbinga lakini toka alipofika Hospitalini hapo na kulazwa ana zaikdi ya wiki moja lakini hajawahi kutembelewa na ndugu yeyote wala rafiki yeyote aliyethubutu kumletea choichote hivyo amefarijika sana leo kupata sabunik ya kuweza kumsaidia kufanyia usafi atapumzika kuomba kwa wenzake amb ao walikuwa wakimsaidia siku zote.
 Mama wa Kipare akifurahi na Mtoto aliyezaliwa siku baada ya kutoa zawadi ya sabuni amesema amejisikia faraja kutembelea siku hiyo katika wodi ya wazazi kwani na yeye siku hiyo ndiyo aliyozaliwa na kuingia duniani hivyo ametoa zawadi hizo huku naye akifurahia kuzaliwa kwake pamoja na watoto wote waliozaliwa tarehe ambayo naye alizaliwa.
 Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ambayo inakabiliwa na Msongamano wa Wazazi katika wodi za Uzazi na hata wazazi wengine kulazimika kulala kitanda kimoja wazazi wawili, wamepata bahati ya kutembelewa na Akina Mama wenye moyo wa Huruma na na wenzao. Pichani ni Mwenyekiti wa Kikundi cha LUKUNDONYIKANAVA CHEE kikundi cha akina Mama wa Kipare Mama Mbaruku akitoa maelekezo kwa wanakikundi kuhusu wodi watakazozitembelea kutoa zawadi.
 Kikundi cha akina Mama wa Kipare wakiwa Nje ya wodi za Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma muda mfupi baada ya kutoa zawadi katika wodi za wazazi wanaosubiri kujifungua, wodi ya wazazi waliojifungua kawaida na wa oparesheni na wodi ya wazazi waliojifungua watoto wa maangalizi maalum (Njiti) ambako walikfanikisha kutoa sabuni kwa kila mzazi mwenye mtotot mmoja nche mmoja na walio na mapacha miche miwili 2
 Akina mama wa Kikpare hapo wakitoka wodini kutoa zawadi za Sabuni kwa wazazi wenzao.
 Ndugu msomaji nadhani unafuatilia vyombo vya habari na taarifa mbalimbali juu ya vitendo vya unyanyasaji wa akina Mama na Watoto ama ukatili wa kijinsia vitgendo ambavyo vinapingwa na kupigiwa kelele siku zote. Vitendo hivi pia vimeikumba na jamii ya Mkoa wa Ruvuma kumekuwa na matukio mbalimbali ya kutupa vichanga na ukatili wa aina nyingine kama wazazi kunyonga watoto wao, kupiga kupita kiasik n.k. kutokana na ugumu wa maisha, na unafahamu ugumu wa malezi ya familia inapotokea mzazik mwenza anakutelekeza, kwa nini usione fahari kusaidia japo kikdogo ulichonacho kwa kundi hili la wazazi ili kuwapa moyo na faraja ya kuwafanya wasiwe na mawazo ya kutupa au kuuwa viumbe visikvyo na hatia? Sikuzote tukumbuke ukitoa na Mungu atakubariki zaikdi.
 Mzazi aliyejifungu Muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Mkoa akifurahia zawadi na huduma nzuri ya wauguzi wa Hospitali ya Mkoa hasa kwa kuwapa elimu ya Malezik na jinsik ya kutambua dalili hatarishi za mtoto na mzazi anaporudi nyumbani ambazo atatakiwa awahi kukimbia hospitali kupata matibabu.
 Wanakikundi cha LUKUNDONYIKA NAVACHEE Bi Fatuma Swai na B i Swaumu wakiwa na furaha kubwa baada ya kutimiza dhamira yao ya kuwafariji wazazi waliojifungua walioko katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.
 Jamii inatakiwa itambue kuwa kila jambo lina heri kwa Mwenyezi Mungu hasa unapotoa kwa moyo kidogo ulichonacho lazima na Mungu atakupa ili uweze kusaidia waliokosa kukipata. Jambo walilolifanya Akina Mama hao ni la thawabu kubwa hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
 Nani Kama Mama? Kwa kweli Mama anahitaji faraja na kupongezwa kwa kazi ngumu aliyopewa na Mwenyezi Mungu tgangu uzazi hadi malezi. Ndugu Msomaji jiulize Mungu amekupa uwezo kiasi gani na nanik aliyekufanya uzaliwe, ukue na kufikia umri wa kujitambua, Jee unadhani ni halali kumdharau Mama tafadhali tuige mfano wa kikundi hiki cha akina Mama ambao sik shirika wala Serikali lakini wameweza kutembelea Watoto Yatima wa Kituo cha Yatima Chipole na baadaye kutembelea Wodi ya Wazazik wa Hospitali ya Mkoa kutoa faraja kwa wenzao Kikundi amb acho hakina Mrfadi wowote. Jee wewe na Mimi tunasubiri nini na tumejaliwa kiasi Gani. kama si wewe muelimishe mwenye nafasi atoe kwa wasiojiweza.

 Hapo akina Mama wakiwa katika Geti la Kuingia Wodini katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wakisubikri kuingia katika Wodi ya Wazazi kwenda kutoa Sabuni kwa Wazazi wenzao.
 Akina Mama wakiwa wamebeba Sabuni wakisubiri kuongozwa Wodi ya Wazazi kutoa zawadi kwa akina Mama waliolazwa Matenity.
 Kulia ni Mc wa kikundi cha Akina Mama wa kipare na walioolewa na Wapare akiongoza Msafara wa Wanakikundi kuelekea Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Mkoa HOMSO

 Mwenyekitik wa Kikundi Mama Mbaruku akitoa Maelezo kwa Wauguzi wa Wodik ya Wazazi katika hospitgali ya mkoa kuhusu sababu ya kutembelea wodi ya Wazazi.
 Akina Mama wa Kipare wakionyesha Moyo wao wa huruma ambao Mwenyezi Mungu amemjalia Mwanamke kuwa nik Mtu wa Huruma kwa kutoa Msaada kwa wagonjwa. Hnapo nik baada ya kutoka Wodi za Wazazi ambko walikuwa wakitoa zawadi ya Sabuni kwa wazazi wenzao.
Mama huyo unayemuona ni miongoni mwa wana kikundi cha akina Mama wa Kipare na Walioolewa na Wapare waishio Songea Akiwa katika Wodi ya Wazazi Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ambako wamekuja kutoa sabuni kwa wazazi hapo amepakata mtoto akiwa na Furaha kuzaliwa kwa kuwa siku hiyo ndiyo siku ambayo naye alizaliwa