KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Monday, July 27, 2015


Waumini wa Kiislamu na Madhehebu mengine wametakiwa kuwa na huruma kwa kusaidia watu wenye shida wakiwemo maskini, wafungwa na wagonjwa waliolazwa Hospitalini.


Katibu wa Msiki wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Mohamed Mfyule ameyasema hayo wakati akigawa chakula kwa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wapatao 1000. 


Katibu wa Msiki wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Mohamed Mfyule
amesema wakati wa Siku ya sikukuu mbambali  ni wajibu wa Waumini  wa Dini mbalimbali kufanya Hija katika Hospitali kwa kuwaona  Wagonjwa waliolazwa na kuweza  kuwafariji hiyo nayo ni ibada

Wagonjwa akila chakula baada ya waislamu kuwa gawia katika kusherekea sikukuu ya idi
Akina mama waja wazito wakijipatia chakula katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma
P0amoja na sherehe ya sikukuu ya iddi waisilamu walijitolea kushinda hospitali
Wagonjwa wapatao 1000 mwakijipatia chakula na kuwaombea waisilamu waendelee na moyo huo huo
Ukiwa siyo mzazi huwezi kujua uchungu wa mimba pamoja na waislamu kujitolea kupeleka chakula lakini akina mama hawa wana sema chakula hakinogi wanaomba waislamu wawaqombee ili wajifungue kwa haraka
Waislamu wakiendelea kutoa chakula huku wakiwafariji waja wazito
muguzi mama mbawala akiwa wodini ,hapo ana washukuru waislamu kwa kutoa chakula na kuwaomba madhehebu mengine waige mfano huo
kweli moyo wawaumini upo kwenye matatizo ndivyo inavyo dhirisha katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma
Unapo sherekea sikukuu ni lazima ujue niviumbe vingapi vina kutegea hapo paka akiwa ameshiba baada ya kupewa chakula
                   Katibu wa Msikiti wa Hospitali akisimamia kwa makini mtu asikose chakula
                  Mambo hayo hapo ni kula tu waislamu wana fanya kazi
Waumini mbalimbali waliokuja kuwaona wagonjwa wao  nao wameshukuru moyo ulio onyeshwa na Waislamu kwa  kujitolea kutoa chakula kwa wagonjwa 1000 


Wagonjwa mbalimbali waliolazwa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wamewaomba wa watu mbalimbali kuja kutoa misaada kwa wagonjwa kwani wako wagonjwa wengine ambao hawana ndugu.  Nao wauguzi wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma  wamewashukuru  waislamu kwa kuweza kutoa  msaada wa  chakula  kwani chakula ni dawa  ikiongozana na ufariji wao wagonjwa .

Saturday, July 25, 2015

CCM NA WAGOMBEA MKOANI RUVUMA FOMU YA KUGOMBEA MILIONI TATU NA LAKI MOJA 3,1OO,000/=

Viongozi ambao wamejitokeza kuchukua Fomu katika jimbo la Songea Mjini wamefikia nane na waliorejesha fomu hizo ni wagombea sita.

Viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi wamejitokeza kurudisha fomu wakiwemo Mbunge wa zamani wa Jimbo la Songea Mjini Dr. Emmanuel john Nchimbi.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Mjini amewataja wagombea waliochukua fomu kuwa ni Sebastian Waryuba, Tereza Uviza, Azizi Mohamedi Fakili, Musa Laurence Gama,  Leonidas Twitbet Gama, Raymond Muhenga, Erick Mapunda na Dr. Emmanuel John Nchimbi.  
                                                          Sebastian Waryuba,

Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini Juma Mpeli amesema mwamko wa wagombea umekuwa mkubwa ingawa wagombea wote wameonyesha imani ya kuwa wagombea,
Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Vijijini Rajabu Uhonde amesema wagombea Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi Songea Vijijini waliojitokeza  kuchukua fomu katika

Majimbo mawili ya Uchaguzi ni 13, Madaba wagombea 10 na Jimbo la Peramiho watatu
Amewataja wanaosndania katika Jimbo la Peramiho ni pamoja na Jenista Johakim Mhagama, Lazaro Venas Pius Mgaya na Glorias B. Luoga, kwa Jimbo jipya la Madaba wagombea ni pamoja na Joseph Kizito Mhagama.

WAGONJWA 1000 WAPEWA CHAKULA NA WAISLAMU SONGEA


Waumini wa Kiislamu na Madhehebu mengine wametakiwa kuwa na huruma kwa kusaidia watu wenye shida wakiwemo maskini, wafungwa na wagonjwa waliolazwa Hospitalini.


Katibu wa Msiki wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Mohamed Mfyule ameyasema hayo wakati akigawa chakula kwa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wapatao 1000. 


Katibu wa Msiki wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Mohamed Mfyule
amesema wakati wa Siku ya sikukuu mbambali  ni wajibu wa Waumini  wa Dini mbalimbali kufanya Hija katika Hospitali kwa kuwaona  Wagonjwa waliolazwa na kuweza  kuwafariji hiyo nayo ni ibada

Wagonjwa akila chakula baada ya waislamu kuwa gawia katika kusherekea sikukuu ya idi
Akina mama waja wazito wakijipatia chakula katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma
P0amoja na sherehe ya sikukuu ya iddi waisilamu walijitolea kushinda hospitali
Wagonjwa wapatao 1000 mwakijipatia chakula na kuwaombea waisilamu waendelee na moyo huo huo
Ukiwa siyo mzazi huwezi kujua uchungu wa mimba pamoja na waislamu kujitolea kupeleka chakula lakini akina mama hawa wana sema chakula hakinogi wanaomba waislamu wawaqombee ili wajifungue kwa haraka
Waislamu wakiendelea kutoa chakula huku wakiwafariji waja wazito
muguzi mama mbawala akiwa wodini ,hapo ana washukuru waislamu kwa kutoa chakula na kuwaomba madhehebu mengine waige mfano huo
kweli moyo wawaumini upo kwenye matatizo ndivyo inavyo dhirisha katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma
Unapo sherekea sikukuu ni lazima ujue niviumbe vingapi vina kutegea hapo paka akiwa ameshiba baada ya kupewa chakula
                   Katibu wa Msikiti wa Hospitali akisimamia kwa makini mtu asikose chakula
                  Mambo hayo hapo ni kula tu waislamu wana fanya kazi
Waumini mbalimbali waliokuja kuwaona wagonjwa wao  nao wameshukuru moyo ulio onyeshwa na Waislamu kwa  kujitolea kutoa chakula kwa wagonjwa 1000 


Wagonjwa mbalimbali waliolazwa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wamewaomba wa watu mbalimbali kuja kutoa misaada kwa wagonjwa kwani wako wagonjwa wengine ambao hawana ndugu.  Nao wauguzi wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma  wamewashukuru  waislamu kwa kuweza kutoa  msaada wa  chakula  kwani chakula ni dawa  ikiongozana na ufariji wao wagonjwa .

Friday, July 17, 2015

RAYMOND MBUNGU APOTEA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA WILAYANI MBINGA

Raymond Mbungu (17) Mkazi wa Mbinga Mjini Mtaa wa Uzunguni ametoweka katika mazingira ya kutatanisha toka siku ya jumatatu ya tarehe 13/07/ 2015 mpaka sasa haijulikani mahali alipo.

Raymond Mbungu ni Mwanafunzi katika Sekondari ya Ruhuwiko Jeshini . Kwa yeyote atakayemuona au kufahamu mahali alipo atoe taarifa kwenye kituo chochote cha Polisi kilicho karibu naye, au awasiliane na wazazi wake kwa namba zifuatazo:  0756 047754 / 0768 220065 / 0764 199264.

Au unaweza kuwasiliana na kituo cha Redio Free Afrika Songea kwa Namba zifuatazo; 0755 731234 / 0755 061588

Tuesday, July 7, 2015

MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID THABIT MWAMBUNGU KUSHIRIKI FUTURU NA VIONGOZI WA DINI IKULU NDOGO SONGEA



Serikali Mkoani Ruvuma imetoa tahadhari kwa wale wote waliojiandaa  kufanya vurugu wakati tukielekea katika uchaguzi  kuvuruga Amani tuliyonayo, Serikali itachukua hatua kali za kisheria   za kupambana na watu hao
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu ameyasema hayo katika futuru ya Mwezi wa Ramadhani iliyoandaliwa Ikulu ndogo ya Songea na kujumuisha Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wakristu wakiwemo  ma Askofu na Masheikh

Wanawake wakiwa katika futuru iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga wamewaomba wanawake wenzao kusimamia maadili ya vijana na watoto wao majumbani wanaokengeuka kwa kutamani kuchochea vurugu na kupoteza amani iliyopo. Wamesema wamama kama walezi wa familia wana wajibu wa kuelimisha watoto wao na kuzuia kujiunga na masuala yanayoashiria uvunjifu wa amani.

Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria Futuru ya Mwezi wa Ramadhani iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu ni Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga, Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Bakari Nalicho, Viongozi wa kisiasa na viongozi wa dini ya kikristo ngazi ya mapadre na Maaskofu
Waumini waliohudhuria katika Futari ya mwezi wa Ramadhani 2015 Ikulu ndogo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wameomba Viongozi wa Dini kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha Amani ya Tanzania inaendelea kudumishwa kwa kuhubiri amani upendo na Mshikamano katika Misikiti na Makanisa na hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Oktoba 2015.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu amesema dalili ya mvua ni Mawingu lakini Serikali imejidhatiti kukabiliana na Vurugu zozote zitakazojitokeza , Serikali  haitamvumilia Kiongozi yoyote wa dini au wa Kisiasa   kufanya uchochezi kwa waumini wake ili kuhatarisha amani serekari ita kuwa macho muda wote.



Sheikh wa Mkoa wa madhehebu la  Suni Shaban Chitete aliweza kuiombea Nchi ya Tanzania ili iendelee kuwa na Amani pamoja na kuwalinda viongozi waliopo .