KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, March 14, 2015

MTOTO WA KIKE AOMBA MSAADA WA KUENDELEZWA ENYI WASAMALIA WENYE MOYO WA MUNGU AKIWEMO MAMA SALIMA KIKWETE.MKAPA FOUNDATION NA WATANZANIA WOTE


MAOMBI YA MSAADA WA KUSOMESHWA (KUENDELEZWA KIELIM

Ndugu GABRIELA  NGONYANI anaomba msaada wa kusomeshwa Elimu ya Sekondari Form Five na Six.

Mtajwa mwenye jina la hapo juu, ni mwanafunzi aliyehitimu Kidato cha Nne  katika Shule ya Sekondari ya St Agness Chipole Songea Vijijini na kupata Ufaulu wa Daraja la Pili (Division Two)

Gabriela Ngonyani ni Mtoto Yatima hana Baba wala Mama hata ndugu wa karibu wa kuweza kumsaidia hayupo, Kwani hata kufikia Elimu ya Kidato cha Nne alipata Ufadhili wa wasamalia wema na sasa anachoomba ni kuendelezwa Kidato cha Tano na cha Sita.

Maendeleo yake kitaaluma toka awali ni Mazuri na ana Ufaulu nzuri wa Masomo ya Sayansi.


MATOKEO NI KAMA IFUATAVYO. CIV-C, HIST-B, GEO-B, ENGL-B, NUTRITION-B, KISWAHL-B, CHEMIST-C, BIOS-C, MATH-E,



 Kwa yeyote atakayeguswa na Taarifa hii anaombwa Msaada wa Hali na Mali ili Kumuwezesha Binti huyu kutimiza Ndoto zake na Mungu atakubariki.

Kwa Mawasiliano piga Simu No: 0755 731234 / 0672 527377 /0755 061588

Saturday, March 7, 2015

UHARIBUFU WA MAZINGIRA UNATOKANA NA WATU WENYE VYEO KUFUMBIWA MACHO MKOANI RUVUMA BILA KUCHUKULIWA SHERIA ZA KINIDHAMU


Moja ya mambo ambayo huleta madhala katika jamii ni pamoja na kukunja sheri pale wakubwa wanapo kosea, Kwa mfano Idara ya Mistu kazi yake ni kulinda Mistu lakini wanapo bahatika kumkamata mhalifu hasa kizitokumchukulia sheria ina kuwa ngumu hebu angalia miti hii iliyo katwa kabla ya kukomaa ambayo ingeweza kutoa mbao mzuri hapo baadaye, aliye kamatwa anawaka kamambogo jee hii ni halali. Nenda pale misitu wlaya utikuta hiyo miti uliza kwa nini ipo hapo jibu utakalo pata ni kuwa katisha taami waaa wafanyakazi wa sekita ya Mistu
 Huu ni mmoja ya mikaa iliyo shikwa na wafanyakazi wa Maliasili ikiwa Wilayani Songea na wenyewe wakiwa wame kimbia

Wafanyakazi wa Mistu mkoa wa Ruvuma wanajitahidi kufanya doria la mara kwa mara lakini uhalibifu unao tokana na Moto ni Mkubwa sana, Hebu angalia Uchomaji wa Mkaa unavyo asili Misitu. Mkaa huo wote unao onekana umekamatwa na wachomaji mkaa wote wamekimbia jee kwa hali hii mistu ita pona
Uchomaji huu wa Mkaa hau fuati Taratibu hata miti midogo huchomwa moto ukienda Porini hivi sasa hata Mwembe wana choma Mkaa ,kwa hali hii wewe na mimi tuna saidia vipi

Baadhi ya wanchi walio kuja kuangalia miti inayo katwa ovyo na mkaa unao chomwa bila kufuata sheria.watu hao walio shuhudia uhalibifu huo wamesema imefika wakati sasa kwa wananchi kutoa tarifa kwa wale wote wanao choma mistu na kusababisha hasara kwa wananchi

HIRIZI PEKEE YA KUDUMISHA AMANI NI KUWA JALI MAYATIMA,MASIKINI,MAFUKARA, NA KUTOA ELIMU KWA NYANDA ZOTE


Amani ina tokana na nini Amani inatokana na vitendo vya viongozi ,kujali Mayatima pale wanapo sherekea siku zao za kuzaliwa aqu sherehe za Crismasi ,Iddi Fitiri na sherehe zingine za kitaifa ni lazima uone jirani yako yuko masikini fukara au yatima kama anavyo onyesha Msitaiki Meya Chares Mhagama kwa kula chakula na Mayatima.

 Watot hawa wanasema wange omba sikukuu ya Mwaka mpya iwe kila siku ili wale wanye kama wanavyo onekana lakini kuwa fanya hivyo kuna tokana na wazazi kila mzazi akijua kuna yatima na kutenga bajeti yake ataweza kufanikiwa kwa kulisha mayatima na masikini
 Watoto wa Manspaa yaSongea wakisherekea sikuuu ya Mwaka Mpya kwa kula Chakula na Meya wa Manispa Chares Mhagama
 Chares Mhagama Meya wa Manspaa ya Songea amesema kila wakati katika kicha chake anawaza ingewezekana watoto wanao ishi katika mazingira magumu tunge weza kugawana watu wote ili kupunguza aza inayo wakabili watoto hao

Mababu zamani ili kuweka maadili mazuri kwa vijana wao walikuwa na kitu kinacho itwa jando, jando ni moja ya kumweka kijana maisha ya ndoa ili aingiapo katika ndoa ajue jinsi ya kutunza familia yake kilicho sisitizwa ni nyumba kuto kuwa na njaa, kuwaq shujaa wakati janga likitokea ,kuzima moto,kupambana na wanyama, pia kuwa mlinzi wa jamimi. Jambo hilo hivi sasa lina fanywa kwa kupeleka vijana kaiti kambi za JKT  kama wavyo onekana hapa yote ni kuwa fundisha kulinda inchi yao na kuleta amani


Viongozi wa kitaifa na wa mikoa mara zote wanatakiwa kuwa na ubunifu kutafuta njia za kuweza kuwafanya wananchi wawe na imani nao kwa kuweza kutafuta njia za kuwa toa katika umasikini, Viongozi wakiwa jirani na wananchi kama wanavyo onekana hapo ita saidia kujua matatizo ya wananchi hapo meya  Chares Mhagamaana mbungeDr Emanuel John Nchimbi wana badilishana mawazo kuhusu maendeleo ya jimbo la songea

 Nikawaida kwa Viongozi wenye Msimamamo kuongea na Waandishi wa Habari katika kujua Maendeleo yaliyo fanyika Hapo kiongozi Shupavu aqmbaye Mungu amempenda zaidi na kuweza kuchukuliwa na Mungu Cap John Komba akiongea na waandishi wa Habari kutoka kushoto Nathani Mtega na anaye fruata Juma Nyumayo wa Mwisho kulia ni Adamu Nindi, Jee Viongozi wote wana fanya hivyo,Viongozi igeni igeni mfano wake Cap John Komba ili kuendeleza amani
 Uhuru wawatoto ni kwenda kila wapendapo na kuhakikisha ulinzi wao upo na amani ina patikana kama unavyo ona katika picha hii
 Watoto hupenda sana michezo kama alivyo samaki anavyo penda maji ,wazazi waacheni watoto wenu kushiriki michezo mbalimbali.Lakini amani hii ina tokana na viongozi wazuri tuwe macho hapo Octoba Mwaka huu kuchagua viongozi Bora ili amani idumu

Tunapo sema Amani ni pamoja na kuona watoto wanawake wana kuwa na sehemu za kiupata burudani na kuweza kusitarehe na watoto wao ,Ndugu8 zangu kama unavyo ona watoto wakicheza kwa furaha hiyo ina tokana na serekari kujali zaidi kudumisha amani, sasa tuna enda kwenye uchaguzi tufanyeje ili amani hii iendelee ? jibu ni kuchagua viongozi bora na siyo bora viongozi.

 Angalia Furaha ya Watoto wanapo kuwa na Amani ndugu zangu Mke ukiwa naye huwezi kuona Uzuri wake ndivyo ilivyo amani ikitoka tuta juta na sisitiza tuchague viongozi wazuri
Mtoto kutembea bila hofu ni furaha kwa wazazi hebu ona kuku kila wakati haamini kama mtoto wake yuko salama kazi kubwa ni kuogopa Mwewe,Paka,Nyoka, Lakini watoto wa kitanzania wao wako huru,

Friday, March 6, 2015

MWANDISHI WA HABARI FATUMA GAFUSSI AFARIKI DUNIA AKIWA MKOANI DODOMA

 Nimeweka picha mbili za kutoka makitaba ya Songea Habari Blog ili uweze kuona Marehemu Fatuma Gafusi aliye katikati ambaye afariki akiwa Dodoma, Fatuma Gafusi alikuwa Mwandishi wa Habari wa Star Tv na Radio Free afirika amefariki kwa ugonjwa wa  Moyo au Shindikizo la damu 5/3/2015 Mwenyezi Mungu aiweke Roho yake Mahali Pema Peponi Amina
Fatuma Gafusi  aliye katikati alikuwa mtetezi wa haki za Mama na Mtoto pia alijiunga na TGNP Katika kutetea haki za Wanawake Fatuma Gafusi kabla ya Kufari aliweza kujiunga na GEMSA Mtandao wa waandishi wa Habari wa afirika Mashariki na ya kati,Bwana alitoa na Bwana ametwaa

Thursday, March 5, 2015

TANZANIA INA INGIA KWENYE UCHAGUZI MKUU MWAKA HUU JEE WATANZANIA WAPO KATIKA MAOMBI YA KUTAKA KUPATA RAIS MWENYE KUFUATA MAADILI YA UONGOZI ?


Ndugu mtanzania ni wakati mgumu wa kuweza kutoa maamuzi ya kisiasa kuhusu hatima ya nchi ya Tanzania
Niwakati mgumu kutokana na viongozi wengi wanao taka madaraka wengine nia yao ni kuongoza watanzania katika matumaini na kuwapeleka katika utulivu na amani.wengine wanagombea ili kutunisha mifuko yao,


Katibu wa chama cha mapinduzi Taifa Abrahamani Kinana amekuwa msitari wa mbele kuhakikisha wana CCM hawaingii katika tama ya uongozi jee watanzania tufanyeje ili lile linalo zungumuzwa na viongozi tuna lifuata.


Hapa Sipika wa Bunge Mh, Anna Makinda  akisalimiana na wana CCM Jee hali kama hiyo haipendezi kwa watanzania tufanye juhudi kulinda matunda haya
Mfanya bishara Mashuhuri akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama Abrahamani Kinana katika uwanja wa Ndege Luwiko Songea,
Nimoja ya Mioyo Mizuri ya kulinda demokorasia kuwa jali watu wa chini ndiyo fundisho analo toa Katibu Mkuu wa CCM Abrahamani Kinana


Hebu tuone hawa  hapa ni viongozi ambao waliacha shuguli zao na kukimbia kuja kumuzika mwenzao Cap John Damiani Komba, jee kuna uwezekano wakuendelea katika iti kadi hiyo ?

Afisa Biashara Manspaa ya Songea Mohamed Challe akipeana Mkono wa Heri na Waziri Msitahafu Edward Luwasa katika uwanja wa Ndege Songea
Nikazi ngumu kwa viongozi wanapo fika kusalimiana na kila aliye mbele yake lakini hiyo inatokana na jinsi unavyo jituma kwa watu ndivyo ilivyo kwa Waziri Mstahafu Edward Luwasa
Vijana wa Chipukizi hawa kuwa mbali na kiongozi wao Waziri Mkuu Mstahafu Edward Luwasa kila mmoja alitaka kuushika mkono wake


Waziri mkuu mstahafu Edward Luwasa amekuwa akionyesha mfano wa upendo kwa watanzani hii ni mara ya pili kuja kushiriki shuguli za kijamii tarehe mosi mwezi wapili alikuja kushuhudia miaka 38 ya CCM sherehehe zilizo fanyika mkoani Ruvuma pia katika mazishi ya Cap John Komba amekuja kwa ndege ya kukodi, uzalendo huo tunauonaje ?

Nema kwa wanachi wa Mkoa wa Ruvuma kusalimiana na kiongozi wanaye mpenda mwenye kujali watu enzi zake, shukurani za wana ruvuma ni kupeana naye mkono
Kijana Machachali wa CCM akiwa na Furaha kuona lengo lake la kuonana na waziri Mstahafu Edward Luwasa lime timia, alisikika akisema nilazima niende uwanja wa Luhuwiko ili ni mlaki  Edward Luwasa
Katibu wa CCM Abrahamani Kinana akisalimiana na Vijana wa Chipukizi na kuwa sisitiza kukilinda chama na kuwa mstari wa mbele kutekeleza ilani za Chama


Kila mmoja ana jua kuwa hakimu au jaji anapo hukumu kesi wasikilizaji wana kuwa Mahakimu namba moja,Hata mpira wa miguu unapo chezwa mashabiki ndio wanao kuwa waamuzi, Mwamuzi akienda kinyume basi ujue mashabiki wata mzomea, kwa maana hiyo naomba kila mtanzania awe mwamuzi wa uchaguzi unao kuja ili tuweze kuchagua viongozi wazuri.



Viongozi wa Serekari na viongozi wa chama wamekuwa wakiimba wimbo wa Amani jee watanzania tuna upokea wimbo huo wa amani ni juu yetu hivi sasa kuingia katika chumba cha mtihani ili kila kiongozi anaye toa sera zake majibu yawe mwezi wa kumi mwaka huu, lakini katika kuingia darasani tusimusahau Mwenyezi Mungu.

Kijana machachali wa CCM  Nape Mnawiye akiteremuka katika ndege ya kukodi kueneza itikadi za Chama


Binadamu amezoea lawama mara zote anasahau kile anacho fanya yeye jee ni kizuri, umefika wakati wakujiandikisha katika dafutari la mpiga kura, uta kuta mwingine hana habari kabisa lakini akichaguliwa kiongozi mbovu yeye ana kuwa wa kwanza kulamu. Na mnukuru sipika wa Bunge la Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Anna Makinda amesema  :ujitahidi kufanya mazuri ili ukifa iwe ni kumbukumbu lako kwa vitendo vizuri ulivyo fanya

Ukiwa na nia ya kuwa pamoja na watu hutaona garama ya kukodi ndege unacho taka ni kuwa karibu na wananchi

RAIS WA JAMUHURI YA MUNGANO WA TANZANIA DR JAKAYA MRISHO KIKWETE AONGOZA MAZISHI YA CAP JOHN DAMIANI KOMBA LITUHI NYASA MKOANI RUVUMA

Watoto wa Marehemu Captn John Damian komba Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mangharibi wakiwa katika foleni ya kwenda kuweka Mavumbi katika Kaburi la baba yao mpendwa ikiwa ni Ishara ya kumbukumbu ya kuwa mwanadamu yu mavumbi katika Imani ya Kikristu.
Wafanya Kazi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioongoza kubeba Jeneza la la Marehemu Captn John Komba wakiwa katika Uwanja wa Michezo wa Majimaji ambako shughuli ya kuaga mwili wa Captn Komba ilifanyika mara baada ya kuwasili Mkoani Ruvuma.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akifanya Mawasiliano ya namna ya kufanikisha Mazishi ya Marehemu Captn John Damian Komba Kijijini kwake Lituhi Wilayani Nyasa Mkoani Ruvuma

Waombolezaji mbalimbali wakaazi wa Mkoa wa Ruvuma waliojitokeza kuupokea mwili wa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mangharibi Marehemu Captn John Damian Komba katika Uwanja wa Michezo wa Majimaji Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.
Viongozi mbalimbali wa Kitaifa wakiwa katika Viwanja vya Maombolezo Lituhi Wilayani Nyasa Mkoani Ruvuma ambako Mazishi ya Captn Komba yalifanyika. Kutoka kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea Mh, Mwanahamis Kwariko, anayefuatia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Anna Makinda, anafuatia Waziri Mkuu Mstaafu Edward lowasa na wanaofuata ni Familia ya Marehemu Captn Komba.
Hapo Makaburi ya Lituhi ambapo jeneza lililowekwa Mwili wa Marehemu Captn John Komba likishuswa katika Makazi ya Milele, Walioshika jeneza ni Wabunge na wafanyakazi wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh. Anna S. Makinda akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Ruhuwiko Manispaa ya Songea.

Naye Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Anne Makinda amesema Binadamu hivi sasa wanajiingiza katika Vitendo viovu kuliko kukimbilia Amani, ni juu ya Watanzania kuaca Tabia ya
Naibu Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Joel akielezezea namna kilivotokea Kifo cha Captn john Damian Komba baada ya kuwasili katika Uwanja wa majimaji ambako wananchi walijitokeza kuupokea na kuuaga mwili wa Marehemu Captn John komba.

Rais wa Malawi Bakili Mluzi alitoa salamu za rambirambi kwa serekari ya Jamuhuri ya Tanzani  kupitia kwa mbunge dr emanuel mchimbi salamu zilizo somwa na Afisa wa Bunge Yakubu Yakubu amesema amesitushwa na kifo cha cap john komba anamwomba mungu amweke mahali pema peponi
Serikai ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeahidi kusimamia Miradi yoye iiyoahidiwa na Marehemu Captn John Damian ambayo tayari ilishaingizwa katika Sera  ya Chama cha Mapinduzi.Mheshimiwa Jenista Mhagama ameyasema hayo  wakati  akitoa Salamu za Serikai za Rambirambi kwa familia ya Marehemu Captn John Damian Komba  na kwa Watanzania kwa ujumla

Mh. Jenista Mhagama amesema Serikali imepata Pengo kubwa kutokana na kifo cha cap John Komba kwa juhudi  na kazi ailizokuwa akizifanya  za kuleta maendeleo , amesema Serikali inathamini mchango mkubwa uliotolewa na Capt John Komba, Kwa hiyo Wananchi wa Jimbo a Mbinga Mangharibi wajue Maendelo yapo pale pale walichokikosa ni kutoweka kwa  Marehemu Captn John Komba.

Katapila iliyotumika kubeba mfuniko wa Kaburi wenye uzito wa Tani Tatu ikiwa Jirani na kaburi tayari kwa kuinua Funiko hilo baada ya Jeneza Kushushwa Kaburini.
Mhashamu Askofu John komba akibariki Jeneza la Marehemu Captn Komba katika Ibada ya kumwombea iliyofanyika katika Uwanja wa Michezo wa lituhi Wilayani Nyasa Mkoa wa Ruvuma.
Hapo wafanyakazi wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa tanzania na Kamati ya Mazishi ya Mkoa wa Ruvuma wakiinua Jeneza baada ya Ibada kumalizika tayari kwa kuelekea Makaburini kwa Mazishi.
Zaidi ya watu 20, wakiwa wameshika jeneza kwa makini lililobeba Mwili wa Marehemu Captn John Komba tayari kwa kulishusha kaburini katika Makao ya milele katika Makaburi ya lituhi Nyasa Mkoani Ruvuma.
Jeneza la Captn John Komba likiwa juu ya Kaburi kabla ya kulishusha kaburini.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Lituhi waliokuwa wamepanda juu ya miti ili kushuhudia kinachoendelea katika Mazishi ya Mbunge wao wa Jimbo la mbinga Mangharibi kutokana na umati wa watu waliokuwa wamfurika kuja kumzika Captn John Damian Komba.
Hapo Ibada ya kumuombea Marehemu Captn John Komba ikiwa inaendelea katika Uwanja wa Lituhi kijijini kwake Marehemu muda mfupi kabla ya Mazishi.


Askofu wa jimbo la Mbinga Mhashamu Askofu John Komba akisoma Misa ya mazishi ya Kumuombea Marehemu Captn John Komba Lituhi Wilayani Nyasa. Waliosimama jirani na Jeneza ni Wafanya kazi wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa tanzania ambao ndio walikuwa wanlibeba Jeneza la Captn Komba.


Katika hali isiyo ya kawaida Cap John Komba Alishachora ramani ya kaburi lake na alishatengeneza mlango wa zege wenye uzito wa Tani 3 ambao uliwekwa na Kijiko cha katapira


Hapo Jeneza likishushwa kwenye Ndege, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akipokea Jeneza la Mwili wa Marehemu Captn John Damian Komba ulipowasili Mkoani kwake katika Uwanja wa Ndege wa Ruhuwiko Manispaa ya Songea.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tanzania Mh. dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Viongozi mbalimbali wa Chama na serikali katika viwanja vya Makaburi ya lituhi ambako Mazishi ya Captn John Komba yalifanyika
Kutoka kushoto Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, akifuatia na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu na kulia ni Mke wa Rais Mama Salma kikwete wakiwa katika Mazishi ya Captn John Komba Kijijini Lituhi Wilayani Nyasa Mkoa wa Ruvuma.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma akipokea Taji la Shada la Maua ili akaweke juu ya kaburi la Captn John Komba.
Mazishi ya Marehemu Captn John Damian Komba yaliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na Misa Takatifu  ya kumwombea Captn john Komba iliongozwa na Askofu Johhn Komba wa Jimbo la Mbinga,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka Mavumbi katika Kaburi la Marehemu Captn John Komba.

Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Edward  Lowasa.
 Naibu waziri wa fedha Mwigulu Lameki Nchemba,
waziri wa Kilimo chakula na Ushirika Steven Wasira,Viongozi wa chama waliongozwa na katibu mkuu wa CCM taifa Abrahmani kinana