KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Tuesday, June 28, 2016

MAFANIKIO YA MKOA WA RUVUMA NA SAID THABIT MWAMBUNGU AKIWA MKUU WA MKOA


Mabadiliko ya Ukuu wa Mkoa na Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Luckness Adrian Amlima, Cosmas Nyano Nshenye, Isabera Octava Chilumba, Juma Homera na Polet Kamando Mgema umepokelewaje Mkoani Ruvuma.
Mkoa wa Ruvuma katika Miaka ambayo ametawala Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu umekuwaje,  Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu katika utawala wake Mkoani Ruvuma ameweza kuunganisha Uhusiano mwema na Nchi jirani ya Msumbiji  na Tanzania na Nchi ya Malawi na Tanzania upande wa Wilaya ya Nyasa na wilaya ya Songea na Tunduru katika Mipaka ya Mkenda Muhukuru na Tunduru Tunduru Mpakani mwa Msumbiji.

 Mkuu wa mkoa Said Thabit Mwambungu alisimamia kikamilifu swala la marndeleo hata ulipo fika mwenge uliweza kufungua miradi kadha ya maendeleo

Katika Sekta ya Elimu ameweza kuinua kiwango cha Elimu kwa upande wa Shule za Msingi na Sekondari  kupunguza upatikanaji wa mimba kwa wanafunzi kutoka asilimia 60% hadi  asilimia 15%
Kuongezeka kwa uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule  kuanzia awali hadi elimu ya msingi kutoka asilimia 40% hadi kufikia asilimia 90% na kufanya ongezeko la watoto wanaoandikishwa kuanza shule kuwa kubwa.

 Katika swala la usafi alisimamia kikamilifu hadi mkoa kila uendako kuna pendeza siyo kwa Songea pekee yake bali ni wilaya zote za mkoa wa Ruvuma. Tuta kukumbuka Mkuu kwa kazi ulizo fanya kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma tuna kutakia kazi mpya katika ofisi ya Waziri Mkuu

Katika Sekta ya Elimu ameweza kuinua kiwango cha Elimu kwa upande wa Shule za Msingi na Sekondari  kupunguza upatikanaji wa mimba kwa wanafunzi kutoka asilimia 60% hadi  asilimia 15%
Kuongezeka kwa uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule  kuanzia awali hadi elimu ya msingi kutoka asilimia 40% hadi kufikia asilimia 90% na kufanya ongezeko la watoto wanaoandikishwa kuanza shule kuwa kubwa.


Sasa kazi ilikuwa katika kusimamia suala la Usafi, Utengenezaji wa Madawati, Kuimarisha Vyama vya ushirika kupitia Saccos  kwa Wananchi ili kuinua Uchumi wa kati lakini kutakana na Uhamisho wake tunategemea Mkuu wa Mkoa Mpya Mh Mahenge kuendeleza maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma.


Kwa upande wa Afya Mwambungu ameweza kusimamia upatikanaji wa huduma nzuri za afya na kupunguza vifo  vya mama na motto kutoka watoto  .


Mkuu wa Mkoa kuna mambo mengi ambayo sijayaainisha lakini hayo machache ndiyo yaliyo jicho la wananchi katika Mkoa wa Ruvuma ikiwa utafanikiwa kuangalia hayo utaweza kusonga mbele. Pia jambo la muhimu ni kuwa na umoja na ufungamano na vyombo vya habari katika kuutangaza Mkoa wa Ruvuma.


Kwa Upande wa Uchumi Mkuu wa Mkoa Mwambungu Aliweza kuinua Sekta ya Kilimo kwa kuongeza uzalishaji wa mazao kutoka Tani 400,000 kwa Mwaka 2010 hadi kufikia Tani 1,480,000  ikiwa na maana ya kila Mwananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuwa na ziada ya Tani moja ya chakula.


Tukiingia wilaya ya Namtumbo kuna Madini ya Urenium, Mbuga za Seluu,  Kilimo cha Tumbaku pamoja na Kilimo cha Mahindi.


Tukiwa wilaya ya Tunduru tuna madini ya Vito ambayo yanapatikana  Muwesi na maeneo mengine  pamoja na Kilimo cha Korosho na Mpunga.


Aidha Wakuu wa Wilaya zote 5  za Mkoa wa Ruvuma  wamefanya kazi kubwa bila kumsahau Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya , Ukifika wilaya ya Songea zao kuu la biashara kwa wananchi katika kukuza uchumi ni Mahindi, Mazao mengine ni Kahawa, Maharage , Mpunga pamoja na mazao ya misitu ambayo ni mbao katika Milima ya Matogoro.


Mh Mkuu wa mkoa Mpya wa Ruvuma Binilith Saatano Mahenge kazi kubwa kwako ni kuinua uchumi wa mwana Ruvuma, Mkoa wa Ruvuma una Vipaumbele vya Uchumi vifuatavyo;


Wilaya ya Nyasa yako maeneo ya Utalii kama Milima ya Living Stone, Ziwa Nyasa Ufukwe wa Ziwa nyasa, Visiwa vya Pomonda na Samaki wa Mapambo wanaopatikana Ziwa Nyasa. Katika kilimo kunahitaji kuendeleza Zao la Korosho Mawese pamoja na minazi , Kilimo cha umwagiliaji na kuboresha Bandari ya mbamba Bay na uzalishaji wa Samaki na Dagaa.

hiki ni kisiwa cha pomonda ambacho kipo liuli katika wilaya ya nyasa ni kisiwa ambacho kilikuwa kikitumika kwa ajili ya watu kujificha vita ya kwanza ya dunia kilikuwa na uwezo wa kuhifadhi watu 250 wakiwa ndani ya pango, ugunduzi wa kisiwa hiki ni matokeo ya utawala wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu. Miti inayo onekana ina zaidi ya karine moja kiwa na maana ya miaka mia moja na miti hiyo iko juu ya mawe

Pia kuna Masuala ya Utalii katika Bonde la Agati pia mbuga za Seluu Mitomoni mpakani mwa msumbiji, pamoja na kuinua zao la Kahawa ambalo ni kiungo kikubwa cha uchumi katika wilaya ya Mbinga.  


Tukiingia Wilaya ya Mbinga tuna vyanzo vingi vya Mapato, kwa upande wa Madini kuna makaa ya Mawe yanayopatikana Rwanda, pia kuna Madini ya Vito na Zeebaki yanayopatikana eneo la Dar Pori.

 Aliye kuwa mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga akifungua mtambo wa mawasiliano eneo la Mhukuru karibu na mpaka wa msumbiji tuta wakumbuka kwa utendaji mzuri wa kazi
 katika utawala wa mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu alijitahidi kuhakikisha shule zote zilizopo mkoa wa Ruvuma kuanzia Shule za awali mpa Sekondari watoto wana kaa ka
tika Madawati, Mkuu wa wilaya ya Songea akiwa msitari wa mbele katika kutengeneza Madawati hapo ana pakua mbao zilizo tolewa na wafanya biashara  Mkuu wa wilaya Beson Mpesya ni huyo aliye vaa sweta ya njano

Mkuu wa Mkoa kuna mambo mengi ambayo sijayaainisha lakini hayo machache ndiyo yaliyo jicho la wananchi katika Mkoa wa Ruvuma ikiwa utafanikiwa kuangalia hayo utaweza kusonga mbele. Pia jambo la muhimu ni kuwa na umoja na ufungamano na vyombo vya habari katika kuutangaza Mkoa wa Ruvuma.

Monday, June 27, 2016

MABADILIKO YA WA KUU WA MKOA NA WILAYA KATIKA TANZANIA



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt.Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi



Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
1.                   Arusha –           Mrisho Mashaka Gambo
2.                   Arumeru –           Alexander Pastory Mnyeti
3.                   Ngorongoro –           Rashid Mfaume Taka
4.                   Longido –           Daniel Geofrey Chongolo
5.                   Monduli –           Idd Hassan Kimanta
6.                   Karatu –           Therezia Jonathan Mahongo
DAR ES SALAAM
1.                   Kinondoni –           Ally Hapi
2.                   Ilala –           Sophia Mjema
3.                   Temeke –           Felix Jackson Lyaviva
4.                   Kigamboni –           Hashim Shaibu Mgandilwa
5.                   Ubungo –           Hamphrey Polepole
DODOMA
1.                   Chamwino –           Vumilia Justine Nyamoga
2.                   Dodoma –           Christina Solomon Mndeme
3.                   Chemba –           Simon Ezekiel Odunga
4.                   Kondoa –           Sezeria Veneranda Makutta
5.                   Bahi –           Elizabeth Simon
6.                   Mpwapwa –           Jabir Mussa Shekimweli
7.                   Kongwa –           John Ernest Palingo
GEITA
1.                   Bukombe –           Josephat Maganga
2.                   Mbogwe –           Matha John Mkupasi
3.                   Nyang’wale –           Hamim Buzohera Gwiyama
4.                   Geita –           Herman C. Kipufi
5.                   Chato –           Shaaban Athuman Ntarambe
IRINGA
1.                   Mufindi –        Jamhuri David William
2.                   Kilolo –           Asia Juma Abdallah
3.                   Iringa –           Richard Kasesela
KAGERA
1.                   Biharamulo –           Saada Abraham Mallunde
2.                   Karagwe –           Geofrey Muheluka Ayoub
3.                   Muleba –           Richard Henry Ruyango
4.                   Kyerwa –           Shaban Ilangu Lissu
5.                   Bukoba –           Deodatus Lucas Kinawilo
6.                   Ngara –           Col. Michael M. Mtenjele
7.                   Missenyi –           Col Denis F. Mwila
KATAVI
1.                   Mlele –           Rachiel Stephano Kasanda
2.                   Mpanda –           Lilian Charles Matinga
3.                   Tanganyika –           Saleh Mbwana Mhando
KIGOMA
1.                   Kigoma –           Samsoni Renard Anga
2.                   Kasulu             –           Martin Elia Mkisi
3.                   Kakonko –           Hosea Malonda Ndagala
4.                   Uvinza             –           Mwanamvua Hoza Mlindoko
5.                   Buhigwe –           Elisha Marco Gagisti
6.                   Kibondo –           Luis Peter Bura
KILIMANJARO
1.                   Siha –           Onesmo Buswelu
2.                   Moshi –        Kippi Warioba
3.                   Mwanga –     Aaron Yeseya Mmbago
4.                   Rombo –       Fatma Hassan Toufiq
5.                   Hai –           Gelasius Byakanwa
6.                   Same –        Rosemary Senyamule Sitaki
LINDI
1.                   Nachingwea –           Rukia Akhibu Muwango
2.                   Ruangwa –           Joseph Joseph Mkirikiti
3.                   Liwale –           Sarah Vicent Chiwamba
4.                   Lindi –           Shaibu Issa Ndemanga
5.                   Kilwa –           Christopher Emil Ngubiagai
MANYARA
1.                   Babati –           Raymond H. Mushi
2.                   Mbulu –           Chelestion Simba M. Mofungu
3.                   Hanang’ –           Sara Msafiri Ally
4.                   Kiteto –           Tumaini Benson Magessa
5.                   Simanjiro –           Zephania Adriano Chaula
MARA
1.                   Rorya –           Simon K. Chacha
2.                   Serengeti –           Emile Yotham Ntakamulenga
3.                   Bunda –           Lydia Simeon Bupilipili
4.                   Butiama –           Anarose Nyamubi
5.                   Tarime –           Glodious Benard Luoga
6.                   Musoma –           Vicent Anney Naano
MBEYA
1.                   Chunya –           Rehema Manase Madusa
2.                   Kyela –           Claudia Undalusyege Kitta
3.                   Mbeya –           William Ntinika Paul
4.                   Rungwe –           Chalya Julius Nyangidu
5.                   Mbarali –           Reuben Ndiza Mfune
MOROGORO
1.                   Gairo –           Siriel Shaid Mchembe
2.                   Kilombero –           James Mugendi Ihunyo
3.                   Mvomero –           Mohamed Mussa Utali
4.                   Morogoro –           Regina Reginald Chonjo
5.                   Ulanga             –           Kassema Jacob Joseph
6.                   Kilosa –           Adam Idd Mgoyi
7.                   Malinyi –           Majula Mateko Kasika
MTWARA
1.                   Newala –           Aziza Ally Mangosongo
2.                   Nanyumbu –           Joakim Wangabo
3.                   Mtwara –           Khatibu Malimi Kazungu
4.                   Masasi –           Seleman Mzee Seleman
5.                   Tandahimba –           Sebastian M. Walyuba
MWANZA
1.                   Ilemela –           Leonald Moses Massale
2.                   Kwimba –           Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
3.                   Sengerema –           Emmanuel Enock Kipole
4.                   Nyamagana –           Mary Tesha Onesmo
5.                   Magu –           Hadija Rashid Nyembo
6.                   Ukerewe –           Estomihn Fransis Chang’ah
7.                   Misungwi –           Juma Sweda
NJOMBE
1.                   Njombe –           Ruth Blasio Msafiri
2.                   Ludewa             –           Andrea Axwesso Tsere
3.                   Wanging’ombe –           Ally Mohamed Kassige
4.                   Makete             –           Veronica Kessy
PWANI
1.                   Bagamoyo –           Alhaji Majid Hemed Mwanga
2.                   Mkuranga –           Filberto H. Sanga
3.                   Rufiji –           Juma Abdallah Njwayo
4.                   Mafia –           Shaibu Ahamed Nunduma
5.                   Kibaha –           Asumpter Nsunju Mshama
6.                   Kisarawe –           Happyness Seneda William
7.                   Kibiti –           Gulamu Hussein Shaban Kifu
RUKWA
1.                   Sumbawanga –           Khalfan Boniface Haule
2.                   Nkasi –           Said Mohamed Mtanda
3.                   Kalambo –           Julieth Nkembanyi Binyura
RUVUMA
1.                   Namtumbo –           Luckness Adrian Amlima
2.                   Mbinga –           Cosmas Nyano Nshenye
3.                   Nyasa –           Isabera Octava Chilumba
4.                   Tunduru –           Juma Homela
5.                   Songea –           Polet Kamando Mgema
SHINYANGA
1.                   Kishapu –           Nyambonga Daudi Taraba
2.                   Kahama –           Fadhili Nkulu
3.                   Shinyanga –           Josephine Rabby Matiro
SIMIYU
1.                   Busega –           Tano Seif Mwera
2.                   Maswa –           Sefu Abdallah Shekalaghe
3.                   Bariadi –           Festo Sheimu Kiswaga
4.                   Meatu –           Joseph Elieza Chilongani
5.                   Itilima –           Benson Salehe Kilangi
SINGIDA
1.                   Mkalama –           Jackson Jonas Masako
2.                   Manyoni –           Mwembe Idephonce Geofrey
3.                   Singida –           Elias Choro John Tarimo
4.                   Ikungi –           Fikiri Avias Said
5.                   Iramba –           Emmanuel Jumanne Luhahula
SONGWE
1.                   Songwe –           Samwel Jeremiah
2.                   Ileje –           Joseph Modest Mkude
3.                   Mbozi –           Ally Masoud Maswanya
4.                   Momba –           Juma Said Irando
TABORA
1.                   Nzega –           Geofrey William Ngudula
2.                   Kaliua –           Busalama Abel Yeji
3.                   Igunga –           Mwaipopo John Gabriel
4.                   Sikonge –           Peres Boniphace Magiri
5.                   Tabora –           Queen Mwashinga Mlozi
6.                   Urambo –           Angelina John Kwingwa
7.                   Uyui –           Gabriel Simon Mnyele
TANGA
1.                   Tanga –           Thobias Mwilapwa
2.                   Muheza –           Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
3.                   Mkinga –           Yona Lucas Maki
4.                   Pangani –           Zainab Abdallah Issa
5.                   Handeni –           Godwin Crydon Gondwe
6.                   Korogwe –           Robert Gabriel
7.                   Kilindi –           Sauda Salum Mtondoo
8.                   Lushoto –           Januari Sigareti Lugangika
Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Juni, 2016