KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Thursday, September 29, 2016

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AWATAKA WAZAZI KUTUMIA CHUO CHA UFUNDI STADI VETA SONGEA ILI KUWA WAFANYA VIJANA WAO KUWEZA KUJIAJIRI

 MKuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Dkt Binilith Satano Mahenge akiwa katika Chuo cha Ufundi VETA Mkoani Ruvuma akisoma na kupokea taarifa ya Utendaji wa kazi za Chuo cha Ufundi Songea.
 Mhandisi Dkt Binilith Satano Mahenge akiwa na uongozi wa juu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Songea kujadili changamoto zinazokikabili Chuo cha VETA ikiwemo ukosefu wa Mabweni na Ucheche wa wanafunzi wanaojiunga na Chuo hicho.
 Mhandisi Dkt Binilith Satano Mahenge akikagua Maeneo mbalimbali ya Chuo cha VETA akiwa ameongozana na Mkuu wa Chuo hicho Gideon Ole Lairambe.
 Moja ya shughuli zinazofanywa na Vijana waliojiunga na Chuo cha Ufundi Stadi VETA ni kuendeleza Miradi ya Kilimo cha Bustani kwa kutengeneza mashine za kumwagilia maji zikiwa zinauzwa kwa thamani ya shilingi 30,000 kwa kila moja.
 Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Songea Gideon Ole Lairambe akimtembeza Mkuu wa Mkoa kuendelea kukagua maeneo na shughuli mbalimbali zinazofanyika katika Chuo hicho.
 Mwandishi wa Habari wa Jambo Leo akiendelea kuziba kamera ya Blog ya songeahabari katika Ziara ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma katika Chuo cha ufundi Stadi VETA Songea.
 Wafanya kazi wa Chuo cha ufundi Stadi VETA ambao ni Wahandisi wakimsikiliza Mhandisi mwenzao Dkt binilith Satano Mahenge akiwataka kuongeza ujuzi katika vifaa vinavyotengenezwa chuoni hapo ili viwe na ubora na mtazao mzuri kuliko bidhaa zinazotengenezwa Nje ya Nchi.
 Wahandisi wa Chuo cha Ufundi VETA Songea wakiendelea kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma jinsi ya kuongeza ubora chuo cha Veta kwa kuwapa mwongozo wa masomo ya ufundi kuwa sio lazima Mtoto ajifunze ufundi wa Magari na umeme, Mafunzo yote yanayotolewa VETA yanaweza kuongeza Ajira kwa vijana na kuongeza Uchumi kwa Nchi yetu ya Tanzania.
 Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Songea Gideon Ole Lairambe akimuomba Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kusaidia kutafuta Ajira za Ufundi ili Vijana waweze kujifunza na kuweza kufanya kazi, jambo litakalosaidia kuongeza mapato katika Chuo cha Ufundi Stadi Songea.
 Mhasibu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Eusebi Peter akisikiliza kwa makini hotuba ya Mkuu wa Mkoa Dkt Binilith Mahenge kuhusu jinsi ya kukuza Mapato katika Chuo hicho cha Ufundi Stadi VETA Songea.
 Wafanyakazi wa Chuo cha Ufundi Stadi Songea wakiendelea kusikiliza Hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Dkt binilithh Satano Mahenge .
 Nao akina mama Wahandisi ambao wako katika kitengo cha Ushonaji, ususi wakisikiliza mbinu za uboreshaji wa Mavazi kwa kushona mitindo yenye kuwavutia wateja.
 Wahandisi wanawake wenye fani za Computer na Type Writer wakipokea maagizo kutoka kwa mkuu wa m koa kuhusiana na kuendeleza Elimu ya TEHAMA ili iwasaidie wanafunzi wanaowafundisha.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Dkt Binilith Satano Mahenge akikagua utengenezaji wa nguo aina ya Batiki iliyotengenezwa na wanachuo cha Ufundi Stadi VETA Songea. Mbele yake ni Mwenyekiti wa Chuo cha Ufundi.

Wednesday, September 21, 2016

KWA NINI AJALI ZINATOKEA MARA KWA MARA NA KUWEZA KUMALIZA WATU

Ni hivi juzi tu tuimeshuhudia watu kumi na mbili wakiwa wa mepoteza Maisha na wengine 30 kujeruhiwa baada ya Basi linye namba za usajili T429 DEU aina ya Zongtong liitwayo NEW FORCE  kupinduka na kusababisha ajali

Jee nikitu gani ambacho kina sababisha ajali kwa mda mrefu  ? Nimechunguza chazo cha ajali zinazo tokea nime baini kuwa Madereva ndio chanzo cha ajali wakichangia na kitu kinacho itwa Toch ambayo huangalia sipidi za magari

Kwa nini nimesema Madereva ni chanzo cha ajali Madereva hupeana tarifa kujua kuwa Trafiki yuko wapi Mwenye Tochi ikiisha julikana baada ya kupewa tarifa na Dereva Mwenzake ana jua eneo hili halina Asikari na kuanza  kukimbia kwa kasi ili kufidia dakika alizo chelewa kwa kuogopa  Asikari wa usalama barabarani

Jambo jingine ukiangalia usafiri kati ya Songea na Dar es salaam kuna mabasi zaidi ya 9 ambayo kila basi lina taka kupata wateje.Mwendo wa  mabasi hayoni  kilometa moja kwa dakika ili likitoka Songea kwenda Dar es salaam ili weze kuingia kati ya   saa mbili hadi saa tatu  usiku

kwa maana hiyo kila Dereva anataka kupata umarufu kwa kufika mapema. Ukiangalia Mmumiliki wa Super Fello Omary Omary yeye  ana mikakati  yake na wafanyakazi amesha waambia wafanyakazi wake ukikimbiza gari Trafiki aka kukamata fedha hiyo ya kulipa faini ita toka ita toka mfukoni mwako hivyo Madereva wana kuwa macho katika kuendesha  Mabasi na kuogopa kutumia posho zao jambo linalo salimisha Roho za Abiria .

Abilia mara zote wanashuhudia wakisikia  sauti zaMadereva  wakipeana tarifa kwa madereva walio nyuma ili kujua Asikari wa Usalama  Barabarani wapo maeneo gani ,Hapo ndipo linapo anza tatizo la kukimbiza mabasi ,Chaajabu ni kuwa hata kama Dereva ana kimbia sijaona hata siku moja abiria akisema Dereva punguza mwendo badala yake Abilia hulala usingizi na kusitukia ajali ikitokea au breki ikifun g"hafula Jambo ambalo watu hubaki kupiga kelele jambo ambalo halisaidii.

Sasa kwa kumalizia nasema Ajali nyingi zina tokea zina tokana na Madereva kufanya Mashindanoili   kwa kukimbiza magari ili kufika mapema kule unako kwenda.

Abiria waache kukaa kimya pale wanapo ona madereva wakikimbiza  magari .Lamuhimu ni kuwa  namba ambazo hutolewa kwaajili ya kutoa tarifa pale dereva anapo liuka taratibu za usalama Barabarani kwa kupiga simu kwa kamanda wa Polisi

Tuesday, September 20, 2016

WAANDISHI WA HABARI WALIO PATA KUWEZESHWA NA TMF KATIKA KUANDIKA HABARI KWA UFASAHA

 Mentees Furaha Levilal akitoa angalizo jinsi ya luchambua Habari na Kuwasilisha kwa wasomaji na wasikilizaji
 Doto Shashi akiendelea kutoa maelezo kuhusu namuna ya kujenga hoja katika Habari na kumuvutia msikilizaji
 Mwezeshaji Dotto akifafanua na kuwa elewesha wandishi juu ya kuandika Habari za TV
 Mwandishi wa BBBC akisikiliza Mada mbalimbali za kuwawezesha wandishi katika taluma yao
 Msimamizi wa waandishi wa habari {Mentees}akiboresha jinsi ya kutumia vizuri taluma ya Habari
 Waandishi wa habari kutoka Tanzania bara wakiwa katika kikao cha TMF Jinsi ya kuweza kuandika habari
Ashura Kisimba kutokea Radio Tumaini akichangia hoja jinsi ya kuwawezesha waandishi wa habari kuendeleza taluma zao

Saturday, September 17, 2016

KAMPUNI YA FREEDOM INAYO SAMBAZA VIFAA NYA NYUMBANI YA TOA MSAADA KWA SHULE YA MSINGI LITISHA VIFAA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 2.5

 Shule ya Msingi Litisha iliyoko Songea Vijijini ilianzishwa Mwaka Mmoja baada ya kupata Uhuru wa Nchi ya Tanzania mwaka 1962 Mpaka sasa imefanikiwa kufanya maafali ya darasa la saba kwa kutoa wanafunzi 2160 kwa maafali  ya 48
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Freedom Martias Zacharia amewaomba wadau wengine wa Elimu kuwekeza katika Elimu kwa kutoa misaada itakayo weza kumjengea maisha mazuri Mwanafunzi wa Elimu ya Msingi ili elimu anayotoka nayo imsaidie katika maisha 
 Katika maafali ya 48, kijiji cha Litisha Mkurugenzi wa Freedom Martias Zacharia akiwa na Mwalimu mkuu wa Shule ya Litisha Andrew Mapunda kulia kwa mgeni rasmi.
Mkurugenzi wa Freedom alisisitiza wanafunzi kwenda shule akitoa mfano amesema yeye Mwenyewe ametokea katika shule hiyo hadi akawa na maendeleo hivyo anajua changamoto za shule hiyo wale wote walionufaika na shule hiyo inawapasa kurudisha fadhila kwa kuwasaidia wanafunzi waliopo, hapo Martias Zacharia alisoma shule ya msingi Litisha  miaka ya 1984 - 1986 na baadaye alihama shule.
 Kibao ni nembo muhimu ya kutambulisha taasisi jambo ambalo wengi huona kama ni mali ya wanafunzi au walimu.Kuimarisha Vielelezo ni njia moja wapo ya kufahamisha historia ya maendeleo ya kitu au jambo kwa jamii.
 Shule ina Manjonjo yake, Kwanza ukiwa msafi inakupa hamu ya kupenda kusoma hebu ona wanafunzi hawa walivyopendeza huwezi kujua kama wako vijijini. Mkamilishe mtoto wako kwa kumpa mahitaji ya msingi katika kujifunza ili kumpa hamasa ya kusoma kwa bidii na kupenda kujifunza kuanzia viatu,sare za shule daftari peni na vitabu pia bila kusahau chakula cha shule.
 Wahitimu 56 wa Darasa la saba shule ya Msingi Litisha Songea vijijini wakifurahia kufikia darasa la saba na kuomba wazazi wawaandalie mahitaji ya Elimu ya Sekondari.
 Wahitimu wa darasa la saba wakisoma risala kwa mgeni rasmi wa maafali ya 48 ya Shule ya Msingi Litisha wameiomba Serikali kuwasaidia upatikanaji wa maji shuleni hapo ili waepukane na adha ya kutafuta maji umbali mrefu.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Biashara ya FREEDOM SHOPING CENTER Songea Martias Zacharia ameomba wafanya biashara wengine wakubwa kushirikiana na Serikali katika kuwekeza kwenye Elimu, Amesema yeye anatambua umuhimu wa Elimu ya Msingi aliyoipata kwa ufasaha na kumwezesha kufanya Biashara kwa ufasaha na kuchangia pato la taifa kupitia kodi.
 Kulia ni Mkurugenzi wa FREEDOM Martias Zacharia akiwa na Mwenyeji wake Andrew Mapunda Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Litisha katika Maafali ya Darasa la saba.
 Waalimu wa Shule ya Msingi Litisha wakiwa katika maafali hayo wamemshukuru mgeni rasmi kwa kuweza kutambua changamoto zinazozikabili shule za msingi katika ufundishaji kwa kutoa vitendea kazi ambavyo vitarahisisha utendaji kazi.
 Wananchi waliohudhuria katika Maafali ya 48 Shuleni hapo wamesema hii ni maafali ya kihistoria kwao kwa kitendo kilichofanywa na Mkurugenzi wa FREEDOM mfanyabiashara mkubwa kuwekeza katika shule za Vijijini.
 Mratibu Elimu Kata ya Litisha Erick Kifaru amewataka Wazazi kujua kuwa watoto wanaomaliza bado ni wanafunzi wanahitaji kuandaliwa mahitaji ya kuendelea na Elimu ya msingi, haitarajiwi kusikia mzazi amepokea mahari au kuidhinisha mtoto wa darasa la saba kuoa au kuelewa hilo ni kosa kisheria na yeyote atakayewaza hilo sheria itachukua mkondo wake.
 Mkurugenzi wa FREEDOM Martia Zacharia akifurahia kutimiza azima yake ya kutoa sehemu ya mapato yake katika kuchangia Elimu kwa watoto wa Tanzania.
 Mkurugenzi wa FREEDOM Martias Zacharia amewaomba waalimu na wazazi wa shule ya Msingi Litisha Peramiho Songea Vijijini kutobadilisha matumizi ya vitu alivyovitoa, amesema vifaa vimetolewa kwa ajili ya wanafunzi vitumike kwa wanafunzi na vihifadhiwe shuleni isitokee Jezi alitoa kwa ajili ya wanafunzi zikaenda kutumika kwa watu wazima timu za  wakubwa, vivo hivyo kwa makabati, laptop na mipira.
 Wananchi wamesema kwa hali aliyoionyesha Mdau wa Elimu Mkurugenzi wa FREEDOM SHOP watashirikiana katika kuhakikisha watoto wao wanaendelea na masomo ili nao waje wafuate mfano wa Mkurugenzi wa FREEDOM hata kama watashindwa kupata Ajira ya Serikalini.
 Wageni waalikwa wa maafali ya 48 ya kuhitimu darasa la saba shule ya Msingi Litisha, kutoka kulia ni Afisa Mtendaji wa kata ya Litisha, Mratibu Elimu Kata ya Litisha, Shekhe wa Kijiji na kushoto ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Litisha.
 Pamoja na nasaha za mgeni rasmi na utoaji wa zawadi shuleni hapo pia aliweza kutoa Vyeti vya kuhitimu Elimu ya Msingi kwa wanafunzi 56 waliohitimu darasa la Saba 2016.
 Wanafunzi waliohitimu elimu ya msingi shule ya Litisha walianza darasa la kwanza mwaka 2010 wakiwa wanafunzi 65 na leo wamehitimu wakiwa 56.
 Wanafunzi 9 kati ya 65 walioanza darasa la kwanza 2010 walipungua kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro, kuhama shule na ugonjwa.
 Kijana wa Darasa la saba akipokea cheti kwa mgeni rasmi Mkurugenzi wa FREEDOM ikiwa ni uthibitisho kwake kuwa amehitimu Elimu ya Darasa la Saba.
 Wahitimu wakiendelea na zoezi la kupokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi wa maafali ya 48 shule ya Msingi Litisha Bw. Martias Zacharia mkurugenzi wa FREEDOM SHOPING CENTER iliyopo Mjini Songea Mkoani Ruvuma.
 Kukabidhiwa mkono wa hongera kwa kuhitimu salama.
 Mkurugenzi wa FREEDOM SHOPING CENTER Martias Zacharia aliweza kupiga picha na wahitimu na wazazi mbalimbali ikiwa ni ishara ya kuboresha mahusiano na umoja katika uendelezaji wa masuala ya Elimu.
 Katika Maafali hayo Mkurugenzi wa FREEDOM Martias Zacharia ambaye ni mfanya biashara wa Fenicha za ndani na neti na mablanket aliweza kukabidhi zawadi za chaki , mipira, rim za karatas, peni, spika ya Amplifayer, Filimbi na Jezi za michezo kwa mpira wa mikono na mpira wa miguu.
 Mgeni Rasmi Mkurugenzi wa FREEDOM akikabidhi Spika kwa mwalimu mkuu na kuonyesha namna inavyofanya kazi amesema spika itawasaidia kutangaza matangazo mbalimbali kwa wanafunzi ili kuleta usikivu.
 Hapo akionyesha aina ya Jezi za Mpira wa miguu kwa wanafunzi wa kiume amesema michezo inahitaji kuwa nadhifu kwa kuvaa sare ili kuleta hamasa kwa wachezaji kucheza kwa malengo ya kuona mchezo ni sehemu ya ajira.
 Wageni waalikwa katika maafali ya mwaka 2016 shule ya Msingi litisha Tarafa ya Peramiho Songea Vijijini.
Maandamano ya pam,oja kuelekea eneo la sherehe ya maafali wahitimu waalimu na mgeni rasmi wa maafali hayo Mkurugenzi wa FREEDOM SHOPING CENTER.