KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, April 14, 2012

UNAKUMBUKA NINI KUHUSU PICHA HIZI ZA VIONGO MIAKA ILIYO PITA ?

Unapo taka kuzalisha viongozi nilazima waijue dini hapo ndani tunaye kiongozi mkubwa ambaye uongozi wake hufuata mapenzi ya Mungu na kupa mtihani msomaji umubaini mwenyewe

Chuo cha Liti Madaba kikiwa na wahimu wa kilimo na mifugo wakiwa na Mtalamu Anselimo Tarimo ambaye sasa amekuwa Rais kamili

Unaweza kuoona picha zina lingana lakini ukitazama kwa makini uta jua niwatu mbalimbali ambao wame piga na viongozi wao angalia kwa makini

siasa ni mchezo mzuri kama wanavyo sema wa henga jee una jionja nini unapo ona picha za Hapo juu ?

Kama nilivyo sema siku ya leo nawaletea viongozi walio fanya jitihada za kuleta maendeleo mkoa wa Ruvuma ,Sasa jee nani ata waiga hawa viongozi ili tuendelee zaidi ?


Hicho ni kikosi kazi kilicho buni mbinu mbalimbali za kuupandisha mkoa wa Ruvuma hadi kufikia hapa tulipo aliye vaa suti ya Buluu ni Mbunge wa Tanga Salehe Pamba wakati huo alikuwa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma

Historia ni ndefu mama huyu baada ya kujifungua mapacha watoto watatu alitaka kunywa sumu lakini watanzania waliweza kumchangia mpaka akawa mashuhuru watoto wake sasa wana soma kwa bahati mzuri alijifungua tena mapacha watoto wawili Mungu awa bariki wal;e wote walio mchangia




Ndugu msomaji napenda kukumbusha mambo mema ambayo yameta mafanikio katika mkoa wa Ruvuma unawaona hapo juu ni wanafunzi katika Chuo chaKilimo na Mifugo cha LITI MADABA hao ndio walio leta ufaulu katika kilimo na ufugaji mkoa wa Ruvuma

Friday, April 13, 2012

WANARUVUMA TUNAENDA WAPI ? HAYA MAUJI ASILI YAKE NINI

Wanaruvuma naomba niulize jee hivi utandawazi maana yake ni kufanya vitendo vya mauaji kila kukicha mwanamke kauwawa tuseme hawa wauaji wanapo ua hakuna sauti inayo tolewa na mtu anaye uwawa,Mia ya 1961 mpaka mwaka 2000 mtu akipiga yowe watu walikuwa wakikusanyika ili kutoa msaada. sasa hebu tuone kwa siku mbili mfululizo wanawake wawili wameuwawa, mmoja kutoka Magereza na mwingi unaye mwona hapo juu ameuwawa eneo la Majengo. Ndugu zangu mfichaficha maradhi kilio kina mfichua, ukiona mwenzako ana nyolewa basi wewe tia maji, Kama una tarifa basa toa tarifa kwa maandi au toa tarifa POLICE

Wednesday, April 11, 2012

YALIYO TOKEA YAME TOKEA CHA MSINGI TUMWOMBEE DADA LULU APATE AFYA NJEMA MWAMUZI NI MUNGU NDIYE MWENYE KUJUA UKWELI

Hatima ya msanii maarufu wa kike Elizabeth Michael maarufu kama “Lulu” (pichani) anayeshikiliwa Polisi kutokana na kifo cha Msanii Steven Kanumba iko mikoni mwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela alisema suala la msanii wa huyo kusema ana kesi ya kujibu au la liko mikononi mwa DPP ambaye atatakiwa kulipitia faili lake na kujiridhisha kama ana kesi ya kujibu au la.

“Kumpeleka Mahakamani ni mpaka DPP tutakapomwasilishia jalada ya tuliyoyakusanya na ndiye atakayeamua kama kuna kesi ya kujibu au hakuna” alisema Kamanda Kenyela.

Alisema hadi hivi sasa wanasubiri ripoti ya uchunguzi wa Daktari ambayo hata hivyo hatatolewa kwa vyombo vya habari kwa kuwa huwa ni siri.

“Bado tunasubiri ripoti ya Daktari na upelelezi unaendelea ila ripoti hiyo ni siri, si lazima apelekwe Mahakamani kesho kwa kuwa bado upelelezi.

KIFO CHA STEVEN KANUMBA

Mungu alito na Mungu amechukua Jina la bwana lihimidiwe pichani juu ni msanii Siteven Kanumba ambaye hivi sasa hatunaye wewe na mimi una zungumuza nini kuhusu kifo hiki. Panapo tokea kifo ni muda mzuri wa kutafakari ili kupunguza matatizo kati ya wewe na mimi. katika kitabu cha agano la kale Mhubiri sura ya 7 ina sema Hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu.mara nyingi tunapo kumbwa na hasira ujue kuwa umesha kuwa mpumbavu jambo la mhimu ni kujiepusha na hasira, Ndugu zangu jiepusheni na mambo yanayo tukabili

Binadamu hasitahili kufanya vurugu hebu ona ubongo wa binadamu ulivyo fuvu hilo hapo juu ni fuvu la msani Siteven Kanumba eneo lililo chorwa mkuki ni sehemu aliyo jigonga na ubongo kushindwa kufanya kazi ya kuruhusu mishipa ya hewa kufanya kazi yake , akina baba akina mama tujitahidi kuto kuwa wagomvi

Ukipatwa na matatizo mtegemee Mungu ndiye pekee mtatuzi wa majonzi hapo ndugu wa Siteven i Kanumba akiwa amezimia nakupewa huduma ya kwanza

Ingawa wengi hushutumu kazi za wandishi wa habari lakini katika kifo cha msanii Siteven Kanumba watuwengi walitarajia kupata habari zilizo sahihi hapo wandishi wahabari wakifanya kazi yao

Serekari ina majukumu juu ya Raia wake Ili kuonyesha ushikiano kati ya Raia na Serekari ni pale serekari inapo jitokeza katika matatizo ya raia. Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Mohamed Bilali akiongoza katika mazishi ya Msanii Siteveni Kanumba

watu waliendelea kupata msituko katika mazishi ya msanii Siteveni Kanumba ambaye alizikwa katika makaburi ya kinondoni Dar - es -Salaam

Ndugu wa Marehemu Kanumba wakiendelea kupoteza fahamu huku wengine wakitathimini maisha yao baada ya hapo watasaidiwa na nani

Umarufu wa mtu unategemea mchango wako ulikuwaje mbele ya wenzio ukiwa na huluka mzuri una sindikizwa kama alivyo sindikizwa Siteven Kanumba, Jifunze kufanya mambo ya watu na siyo yako tu


Shetani akiingia kati yenu anajulikana baada ya madhara kutokea dada Lulu akitafakali kwa makini kwa nini shetani alingia kati yao, cha msingi ni kutoangalia kosa ni swala la kuweza kusawazisha jambo kila nafisi Mungu aliipangia kifo chake ingawa kipo kitu kina itwa Kadiri ya Mungu

Sunday, April 8, 2012

SHEREHE ZA PASAKA SONGEA

Mhashamu Asikofu Mkuu wa jimbo la Songea Norobeti Mtega akiwa katika ibada ya Pasaka akiwahusia waumini kuacha starehe na badala yake fedha wanazo tumia anasa wanunue vitabu vya mwenyezi Mungu ikiwemo Bibilia Takatifu


waumini wa dhebu la kiluteli wakiwa katika ibada ya Pasaka katika Manspaa ya Songea

Wachungaji wa dhehebu la dini ya kiruteli wakiendesha misa ya Pasaka katika manispaa ya Songea

Thursday, April 5, 2012

CHAMA CHA USHIRIKA MANISPAA YA SONGEA CHA PATA MAFANIKIO

Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Halmashauri ya Manispaa ya Songea Meck Mguhi akitoa maelekezo kwa Wajumbe wa Mkutano wa mwaka uliofanyika katika Ukumbi wa Saccos ya Walimu Songea Vijijini kushoto kwake ni Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Mjumbe wa Mkutano wa Saccos ya Halmashauri ya Songea Martha Maongezi
aliyepata faida kupitia mikopo ya Saccos na kuweza kununua pikipiki, kujenga nyumba na kusomesha mtoto wake hadi chuo.

Wanachama wa Saccos ya Halmashauri ya Songea wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Kawaida wa chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo uliofanyika katika Ukumbi wa Saccos ya Walimu Songea Vijijini Manispaa ya Songea.

MWANAMKE SONGEA ABAKWA NA KUUWAWA

Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Maiko Kamhanda amewataka wanawake kuachana na wanaume wanawataka kufanya mapenzi kwa kuwapeleka porini hao hawana mapenzi kwao bali ni kutaka kuwatoa roho, kamanda ameya serma hayo baada ya mwanamke mmoja kuuwawa baada ya kubakwa

Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Police Wanake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo amelaani vitendo vinavyo fanywa na wanaume wasio kuwa na mapenzi ya dhati Mwenyekiti huyo ametoa ahadi mbele ya watu walio furika kushuhudia maiti ya bint huyo amewaomba watu kuitambua maiti hiyo

Maiti ya Binti aliye bakwa akiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti mkoani Ruvuma