Mungu alito na Mungu amechukua Jina la bwana lihimidiwe pichani juu ni msanii Siteven Kanumba ambaye hivi sasa hatunaye wewe na mimi una zungumuza nini kuhusu kifo hiki. Panapo tokea kifo ni muda mzuri wa kutafakari ili kupunguza matatizo kati ya wewe na mimi. katika kitabu cha agano la kale Mhubiri sura ya 7 ina sema Hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu.mara nyingi tunapo kumbwa na hasira ujue kuwa umesha kuwa mpumbavu jambo la mhimu ni kujiepusha na hasira, Ndugu zangu jiepusheni na mambo yanayo tukabili
Binadamu hasitahili kufanya vurugu hebu ona ubongo wa binadamu ulivyo fuvu hilo hapo juu ni fuvu la msani Siteven Kanumba eneo lililo chorwa mkuki ni sehemu aliyo jigonga na ubongo kushindwa kufanya kazi ya kuruhusu mishipa ya hewa kufanya kazi yake , akina baba akina mama tujitahidi kuto kuwa wagomvi
Ukipatwa na matatizo mtegemee Mungu ndiye pekee mtatuzi wa majonzi hapo ndugu wa Siteven i Kanumba akiwa amezimia nakupewa huduma ya kwanza
Ingawa wengi hushutumu kazi za wandishi wa habari lakini katika kifo cha msanii Siteven Kanumba watuwengi walitarajia kupata habari zilizo sahihi hapo wandishi wahabari wakifanya kazi yao
Serekari ina majukumu juu ya Raia wake Ili kuonyesha ushikiano kati ya Raia na Serekari ni pale serekari inapo jitokeza katika matatizo ya raia. Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Mohamed Bilali akiongoza katika mazishi ya Msanii Siteveni KanumbaShetani akiingia kati yenu anajulikana baada ya madhara kutokea dada Lulu akitafakali kwa makini kwa nini shetani alingia kati yao, cha msingi ni kutoangalia kosa ni swala la kuweza kusawazisha jambo kila nafisi Mungu aliipangia kifo chake ingawa kipo kitu kina itwa Kadiri ya Mungu




nice information
ReplyDelete