KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Monday, March 4, 2013

WAISHIO MPAKANI MWA ZIWA NYASA WAISHI KWA AMANI

Sehemu ya mpaka kati ya Tanzania na Malawi ni Rangi Nyekundu inayo onyesha pembeni mwa Ziwa Nyasa ,Alama kamili msitari huo unge pita katikati ya Ziwa Nyasa

Hakuna mgogoro wa mpaka Tanzania na Malawi-Serikali

Na Mwandishi Wetu,Dodoma

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rita Mlaki, aliliambia Bunge jana kuwa hakuna mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi unaosababishwa na Ziwa Nyasa.

Alisema wameshakaa vikao mara mbili na viongozi wa serikali ya Malawi kuzungumzia kuhusu mipaka na kuridhika kuwa hakuna tatizo hilo kati ya nchi hizo.

Waziri Mlaki alisema wanatarajia kukaa kikao cha tatu ili kupata tafsiri ya namna mipaka inavyogawanywa katika maeneo ya ziwa na bahari.

Alikuwa kijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mkwajuni (CCM), Mzee Ngwali Zuberi, aliyetaka kujua lini serikali za Tanzania na Malawi zitakaa kutatua tatizo la mipaka kati ya nchi hizo.

Swali hilo lilitokana na swali la msingi la Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu kwa Waziri wa Maji, aliyetaka kujua serikali imeshindwaje kunadi jina la Ziwa Nyasa ili kuondoa utata wa Malawi inayodai kuwa ziwa hilo lote ndani ya nchi yao.

Naibu Waziri wa Maji, Shamsa Mwangunga akijibu swali la Mbunge Nyalandu alisema Tanzania ina uhusiano mzuri na Malawi kwa muda mrefu na kwamba ahaina mgogoro kuhusu ziwa hilo.

Hata hivyo, alikiri kuwa sheria za wakati wa wakoloni ndiyo chimbuko la Ziwa Nyasa na kwamba mkataba wa Anglo German ulibainisha kwamba ziwa hilo ni milki ya Malawi kinyume na taratibu za sasa za mipaka inayopita majini, inayotoa fursa sawa kwa nchi zinazotenganishwa kwa ziwa au bahari, kwamba mpaka upitie katikati ya ziwa au bahari husika.

Alisema Tanzania na Malawi zinaendelea kutumia ziwa hilo kwa shughuli za kila siku bila ya mgogoro wa aina yoyote na pia zinaendelea kubuni miradi ya pamoja ya kuendeleza Bonde la Ziwa Nyasa.

Saturday, March 2, 2013

MINDO MBINU YA MANISPAA YA SONGEA HAYA RIDHISHI

Wananchi wanao kaa Eneola Mjimwema Manispaa ya Songea mara kwa mara wamelalamikia madaraja ambayo yana wekwa bila  vikinga Ajali. Hivi karibuni loli lililo beba tofali lilikosa njia wakati likipisha na gari lingene hatimaye kutumbukia mtoni .
Hebu ona Gari hilo baada ya kutolewa mtoni lilivyo haribika kwa kuwa Maiti inakuwa haina makosa ikisha kufa ndivyo wanyonge wanavyo kosa haki wakisha pinduka.
Napenda kumukuru Mkuu wa mkoa Wa Ruvuma ambaye alisema, Sheria haiwezi kukulinda unapo kuwa umepoteza maisha lakini mwenyewe una takiwa kujilinda unapo kuwa hai. Jee Manispaa Tusemi hajui maana ya kuweka vikinga Ajali ?

Wednesday, February 27, 2013

MKOA WA RUVUMA WAWAKUMBUKA MASHUJAA WALIO KUFA KWA KUNYONGWA WAKATI WA VITA VYA MAJIMAJI MWAKA 1906

Waziri wa Maliasili na Utalii Nchini Tanzania Balozi Hamis Kagasheki ameweza kuongoza Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika kuwakumbuka Mashujaa wa Vita vya Majimaji walionyonga tar 27/02/1906 na Wajerumani ambapo Mashujaa 61 walizikwa katika Kaburi moja.
  1. Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma hukumbuka Mateso waliyoyapata Babu zao, Hapo wapo katika Viwanja vya Mashujaa Mahenge Manispaa ya Songea kushuhudia Maombolezo yaliyoongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Hamis Kagasheki. 
Uwanja wa Mashujaa Mahenge umezungukwa na picha za Mashujaa wa Vita vya Majimaji hiyo ni picha ya shujaa Chifu Songea Mbano
Hapo Mh. Balozi Hamis Kagasheki akiongoza Maandamano yaliyoanzia Sehemu waliyonyongwa hadi katika Uwanja wa Mashujaa

  1. Katika Maombolezo yaliyofanywa Viwanja vya Mashujaa Mahenge Mgeni Rasmi Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Hamis Kagasheki aliweza kuweka Ngao na Mkuki katika Mnara wa Mashujaa wa Vita vya Majimaji, hapo anaonekana akiweka Ngao.
  1. Waziri wa Maliasili Balozi Hamis Kagasheki akienda kuweka Ngao na Mkuki katika Mnara wa Mahujaa Mahenge.
 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu akiweka kinjenje
 Mkuu wa mkoa akirudi jukwaani baada ya kuweka silaha ya jadi aina ya kinjenje
 Bregedia akiwa katika mnara wa Mashujaa Mahenge akiweka Upinde na Mshale
  1.  Chifu wa Wangoni Mbano akiwakilisha Wangoni kwa kuweka Kinjenje na Rungu (Kibonga)  katika Mnara wa Mashujaa
  1. Katika kuwakumbuka Mashujaa waliotangulia mbele za Haki Jeshi la Wananchi limeweka Utaratibu Maalumu ikiwa ni pamoja na kulipua mizinga na Fataki katika kuwakenzi Mashujaa.
 Hapo wanajeshi wakiendelea kutoasalamuza maombelezikwa njia ya kijeshi
 Hiyo yote ninjia ya kuwakumbuka Mashujaa walio  Tangulia
 Ukiwa umepitia mafunzo ya kijeshi  utajua uchungu wanao upata waombolezaji hawa
 Nimoja ya kuomboleza kuinamisha kichwa chini ni dalili ya kumwomba mwenyezi Mungu awaweke Mahali pema Mashujaa  walioo tangulia Mbele zahaki


 Jeshi  unatakiwa kungangamala ,hebu ona jinsi mashujaa wanavyo omboleza katika kuwa kumbuka Mashujaa waliotangulia
 Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wakiwa katika viwanja vya mashujaa Mahenge Manispaa ya Songea
Jeshi la Wananchi wa Tanzania likitoka nje ya Uwanja wa Mashujaa baada ya
             kumaliza taratibu zote za Maombolezo kwa kuwakumbuka Mashujaa 61
             walionyongwa na kuzikwa katika kaburi moja

 Mwalimu Kaisi Ally kutoka dhehebu la Ahamadiya Mkoa wa Ruvuma akiwaombea mashujaa walio Tangulia wakati wa maombolezo  katika uwanja wa mashujaa manispaa ya songea
Mkuu wa Wilaya ya Rudewa Juma Madaha akiwa mmoja wa waombolezaji wa
           Mashujaa wa Vita vya Majimaji.
Wanajeshi wakilipua Mizinga kuashiria kuwakumbuka Mashujaa wa Vita vya Majimaji.
Wanajeshi wakilipua Mizinga kuashiria kuwakumbuka Mashujaa wa Vita vya Majimaji.
Wanajeshi wakilipua Mizinga kuashiria kuwakumbuka Mashujaa wa Vita vya Majimaji.

Friday, February 22, 2013

KIGANJA CHA MKONO WA BINADAMU CHA KAMATWA LIZABONI SONGEA

KIGANJA CHA MKONO WA BINADAMU CHA KAMATWA LIZABONI

Katika Tanzania tuna kabiliwa na Vita vya aina mbalimbali kiuchumi, kiafya, pamoja na vita ya kulinda utulivu na amani tuliyo nayo.

Wapo wanao tegemea kufanikiwa katika biashara kwa kutumia viungo vya Watu wengine, kutaka viungo vya Albino na Kadhalika

Kwa mujibu wa Tarifa zilizo tolewa na RPC Mkoa wa Ruvuma  Desdedit Nsimike zina sema ,juu ya kukamatwa kijana Denes Fransis Kafinje  akiwa na kiganja cha Mkono wa Mtu nini maana ya Vitendo hivyo

Kwa hapa Ruvuma ni tofauti Kijana unayemwona hapo chini Denes  Francis Kafinje Mkazi wa Lizaboni anatuhumiwa kwa kupatikana na Kiganja cha Binadamu, akiwa ameweka ndani ya Box kwa umahiri mkubwa

Cha kujiuliza Kiganja hicho alimkata nani hakuna mtu aliyeripotiwa kukatwa Kiganja Mkoani hapa

Ndugu zangu mambo haya ni ya kutisha lakini tutafanikiwa ikiwa tutatoa taarifa kwa kuyaripoti matukio kama haya.
 Ona jinsi watu walivyo wakatili huo ni mkono wa Mtu ulio katwa angalia jinsi ulivyo katwa kwa makini tuta fikakweli
 Mtuhumiwa aliye kamatwa na kiganja  cha Binadamu Denes Fransis Kafinje akihojiwa na Jeshila Police Mkoani Ruvuma
Kiganja cha mkono  wa binadamu  hakijulikani nani alikatwa ni juu ya Watanzania kuwa fichua hawa wahalifu

Wednesday, February 20, 2013

BARAZA LA TAIFA LA UWEZESHAJIWANANCHI KIUCHUMI LA DHAMINI VYAMA VYA USHIRIKA NA KUWEZA KUKOPESHWA SHILINGI BILIONI 8 .5

Washiriki wa Semina ya Ujasiliamali katika Kijiji cha Mapipili Kata ya Kitumbalomo Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma wakisikiliza mada za ujasilia mali zilizo tolewa na Baraza laTaifa la uwezeshajiWananchikiuchumi

Afisa Mwandamizi wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi Raymond Justine Ritte akiwa katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mbinga . Wa kwanza kulia ni Oswald Yohana Karadisi Afisa Mwandamizi Ujengaji uwezo na uendelezaji Biashara kwa wajasiliamali na aliye katikati ni Dada Sarah Lupembe

Afisa Mwandamizi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi Raymond Justine  Ritte akiwa katika Ofisi ya Ushirika Wilaya ya Mbinga
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga akiwa na Afisa Ushirika Wilaya ya Mbinga akitambulisha ugeni kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi wakiwa katika Ofisi ya Mkurugenzi
 Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mh Kahindi akiwa na Afisa Mwandamizi wa ujengaji uwezona uendelezaji wa biashara kwa wajasilia mali Oswald Yohana Karadisi akisalimiana na mkuu wa wilaya ya Nyasa

Washiriki wa Semina ya Ujasiliamali wapatao 100 kutoka kijiji cha mapipili wakisikiliza Mada ya Jinsi ya kufanya Biashara na Kanuni zake

Washiriki wa Semina ya Ujasiliamali katika Ukumbi wa Mapipili kata ya Kitumbalomo wilayani mbinga wakisikiliza kwa Makini Mada ya Ujasiliamali

Washiriki wa Semina ya Ujasiliamali katika Kijiji cha Mapipili Kata ya Kitumbalomo Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma.

Washiriki wa Semina ya Ujasiliamali wapatao 100 wakisikiliza Mada ya Jinsi ya kufanya Biashara na Kanuni zake
Kijiji cha Mpipili Kata ya Kitumbalomo Wilaya ya Mbinga kilometa 25 kutoka Mbinga Mjini kinavyoonekana kikiwa kimezungukwa na Milima mikali

Kijiji cha Mpipili Kata ya Kitumbalomo Wilaya ya Mbinga kilometa 25 kutoka Mbinga Mjini kinavyoonekana kikiwa kimezungukwa na Milima mikali.

 Mwenyekiti wa Kijiji cha Mpipili Esau Esau akiwa nje ya Ukumbi wa Semina.

Friday, February 8, 2013

MILA NA DESTURI ZA MWAFRIKA KWA NINI HAZI FUATWI VILIVYO


 GOGO LA MAAJABU AMBALO VIONGOZI MBALIMBALI WALIKAA JUUYA GOGO HILO WALIFANIKIWA    KATIKA MAPAMBANO YA VITA VYA UKOMBOZI

Ndugu Msomaji wa Blog ya Songea Habari.blogspot.com. Napenda kukukaribisha ili uweze kuona Kitu kinachoitwa Imani kina maana gani.

Jambo la Msingi napenda kukurudisha katika Mila na Desturi ambazo zilikuwa zikiwafaa Wabantu. Ukumbuke kuwa Mila na Desturi za wenzetu hawa watu weupe au Wazungu ndio waliotuteka katika mila zao, huyu tunayemwita Mungu ambaye yupo katika Biblia na katika Kurani Tukufu .

Lakini hiyo haifanyi kuwa sisi Wabantu tulikuwa hatuna Mungu wetu. Hebu rudisha Mawazo yako nyuma, Jee hawa watu weupe tunaowaita Wazungu walikuwa wakijua lugha zetu la, 

Sasa hebu uone mimi Mungu wangu kwa Lugha yangu Mungu nilikuwa namwita Chapanga, wengine Nguluwi, Mulungu, Mnungu, Mluku .  hayo yote ni majina ya kibantu  yaliyo kuwa ya kitumika kumwita Mungu  hii ni kuthibitisha kuwa Waafrika walikuwa na Dini zao za Asili.

Kitu ambacho nataka kukuambia. katika kudai Uhuru Nchi mbalimbali za Africa zilikuwa na mila ya kutambika ili kupata Mafanikio, katika kuomba Mvua , kushinda Vita au Jambo lolote ambaloni Gumu.

Sasa hebu tuone Mfano mdogo katika Nchiya Msumbiji wakati wa Vita vya Frelimo na Wareno, Mkutano wa pili wa Vita hivyo ulifanyika Macheja mpakani na Tarafa ya Mhukuru Nchini Tanzania ,kitu cha ajabu wa kuu wote waliokuwa wakipigania Uhuru walikuwa hawa kai kwenye viti bali wali Tumia Gogo kubwa kukalia wakiwa na imani na gogo hilo kwa kupata ushindi .

Sasa tuingie Nchini Msumbiji tuone wenzetu walivyokuwa na Imani na gogo kubwa ambalo linasadikiwa Viongozi wote wa Afrika wameweza kukaa juu ya gogo hilo na kila aliyekaa hapo alifanikiwa kupata Ushindi.

Ziangalie kwa makini hizo picha hizo uone viongozi walivyokuwa wazalendo kwa kuipenda Nchi yao na mila zao.
 Mke wa Marehemu Moses Machel wakati wa mapambano wa vita vya msumbiji picha hiyo ili pigwa macheje Nchini Mozambiki
 Marehemu Samora Machel akipanga mashambulizi dhidi ya Wreno Nchini Mozambiq wakati ule
 Marehemu Candido Mondlane akiwa uwanja wa mipango ya vita Macheje Nchini Mozambiq
 Njia ya mapambano dhidi ya warenoili tegemea zaidi mto Ruvuma kwa uvushaji wa Silaha
 viongozi wandamizi wa Mozambiq aliye vaa kofia Samora Machel na wa mwisho ni Rais wa sasa wa msumbiji Armando Emillo Guebuza wakiwa wamekaka katitka Gogo la ukombozi
 Marehemu Samora Machel akitoa maagizo kwa ArmandoEmillo Geubuza wakiwa wamekalia gogo la ukombozi