KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Thursday, August 3, 2017

TFS SONGEA WAKAMATA MBAO NA KUWA FIKISHWa MAHAKAMANI



Wadau wa Mazingira Mkoani Ruvuma wametakiwa  kulinda Mazingira ili kuweza kuepukana na Janga la  kukosa  mvua na kushindwa kukabiliana na uharibifu wa Hewa Ukaa.

Hayo yamebainika baada ya Wakala wa Huduma za Mazao ya Misitu (TFS) kukamata Gari lenye namba za usajili T. 194 ABL Aina ya SCANIA likiwa n mbao 400 pamojana Mkaa  ukiwa na thamani ya shilingi 24,871,944

Mkuu wa Mkoa  wa  Ruvuma  Mhandisi  Dr. Binilith  Satano Mahenge  amewataka wafanya  kazi wa TFS kuacha kujadiliana na waharibifu wa Mazingira badala yake Mali zinazokamatwa zitaifishwe baada ya  kukidhi masuala yote ya kisheria.

Kaimu meneja wa Wakala wa Huduma za Mazao ya Misitu (TFS) wilaya ya Songea Juma Omary  Mbwambo amesema sasa hivi Mazao ya misitu hupelekwa Nchi  jirani ya Msumbiji baada ya kuona udhibiti wa usafirishaji mkaa nje ya Mkoa wa Ruvuma umedhibitiwa. 
 Mkoa wa Ruvuma umekuwa ukikabiliana na waharibifu wa Mazingira baad ya kuona eneo lililobaki kuchoma mkaa ni Ruvuma na Mbao zenye ubora zinapatikana mkoa wa Ruvuma.

No comments:

Post a Comment