KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Monday, March 28, 2016

ANUSURIKA KUPOTEZA SEHEMU NYETI ZA SIRI SONGEA



Kamanda wa Police mkoa wa Ruvuma Zuberi Mwombezi amekemea Vikali vitendo vya Unyanyasaji wa kijinsia baada ya Mfanyakazi mmoja wa Shirika la TANESCO Mkoani Ruvuma kukatwa sehemu za siri na  mwanamke wa  wa nyumba ndogo na kusababisha kuzirai mfanyakazi huyo.
Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Zuberi Mwombezi amesema katikka siku hizi za Siku kuu ya Pasaka Mfanyakazi mmoja wa Shirika la TANESCO mtunza Stoo, Philipom Msowola alikwenda nyumba ndogo hali ya kutoelewana ilianza na nyumba ndogo ikachukua kitu chenye ncha kali na kumkata Philipo Msoyola jambo lililosababisha apoteze fahamu ambapo baada ya tendo hilo mwanamke wa  nyumba ndogo hiyo ametoroka.

Sunday, March 27, 2016

SHIRIKA LISILO LA KISEREKARI LA PAD LA TOA VIFAA TIBA KWA WAZEE WA MANSPAA 7YA SONGEA

shirika lisilo la kiserekari la PAD likitoa vifaa tiba katika Zahanati za Manspaa ya S
ongea Dr Maida akitoa vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa PAD Isaka Msigwa

moja ya vifaa vilivyo tolewa ni pamoja na Mizani za aina mbalimbali
Mizani za kisasa ambazo zimetolewa na shirika la PAD
Vifaa tiba vilivyo tolewa na PAD Kutoka kwa wafadhili wa Inchi ya Ungereza ambayo ina saidia wazee Tanzania
                              watalamu wa zahanati za Manspaa ya Songea wakijaribisha Mizani za kupima uzito

                              watalamu wa zahanati za Manspaa ya Songea wakijaribisha Mizani za kupima uzito
         vifaa vilivyo tolewa ni jumula ya vifaa 66 ikiwa nipamoja na  vifaa tiba vikiwa na zaidi ya shilingi milioni 13

MTAFITI WA KILIMO KUTOKA KITUO CHA UTAFITI MIKOCHENI DAR-ES-SALAAM AKIELIMISHA KILIMO KATIKA KUPAMBANA NA UGONJWA WA MNI ILI KUENDELEZA ZAO LA MAHINDIRUVUMA

Mtafiti wa Kilimo Kutoka Mikocheni Dr. Juma Kayeke amesema ili kupambana na Ugonjwa wa wa kubungua Mahindi yakiwa shambani hayajavunwa ni vizuri mkulima akatumia njia ya kupanda mahindi na katikati mimea ya mikunde (Desmodium) ambayo husaidia kufukuza wadudu wanajitokeza katika mahindi kupitia harufu yake. (Katika Picha ni Mbegu za Desmodium)
Dr Kayeke ameyasema hayo wakati akiongea na Vikundi vya wakulima wa Mashamba darasa yaliyopo Namtumbo yenye lengo la kuendeleza Kilimo cha Mahindi kwa kutoharibu aridhi kwa kutumia Mabingobingo(Napier grass)  na meimea ya Desmodium ili kuongeza rutuba.
Shamba Darasa la Mkulima wakulima wa Namtumbo likionekana limestawi mimea ya mikunde ya Desmodiua kwa ajili ya kuzuia mbegu za viduha kuota na kufukuza wadudu waaharibifu wanaobungua mahindi shambani (Stock boores).
Wakulima wa Zao la Mahindi wakiwa katika shamba darasa ambalo limepandwa kwa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo na Mtafiti wa Kilimo kutoka Mikocheni Dr Juma Kayeke chini ya usimamizi wa Mratibu wa mashamba Darasa wilaya ya Namtumbo Sammy Mwakyusa wameomba kuendelea kupewa Elimu ya Kitaalamu ili waachane na Kilimo cha Mazao na kulima Kilimo chenye tija.
Wakulima wa Namtumbo wakikagua Shamba Darasa lenye uoto wa mahindi, mabingo bingo pembeni na Desmodium katika kukabiliana na wadudu waharibifu wa mahindi.
Mimea ya Mabingo bingo ikiwa imezunguka shamba ili kuvuta wadudu wanaoharibu Mahindi kukimbilia kwenye mabingobingo badala ya kushambulia mahindi. Kwa mujibu wa Dr Kayeke mtafiti wa kilimo na Uendelezaji wa zao la Mahindi amesema mabingo bingo pia yakichanganywa na Desmodium ni chakula kizuri chenye vitamini kwa wanyama kama Ng`ombe na Mbuzi.
Dr Juma Kayeke na wakulima wa Shamba darasa la mahindi lililopo eneo la magereza Namtumbo wakielezea jinsi watakavyonufaika na kilimo hicho kwa kupunguza gharama za uendeshaji wa kilimo na kupata faida ya chakula cha mifugo kupitia mimea ya Desmodium na Mabingobingo.
Akiainisha faida za kutumia kilimo cha Sukuma Vuta, Dr Juma kayeke amesema lengo ni kudhibiti viduha lakini pia kupitia mimea ya Desmodium inasaidia kupambana na ukame kwa kuwa mimea hii inasaidia kuhifadhi unyevu.
Wakulima wa wilaya ya Namtumbo wameshukuru kuletewa Elimu hii wameomba iwe endelevu na isiishie kwenye zao la Mahindik pekee ili mkulima aweze kunufaika na Kilimo.
Dr. Kayeke akitoa ufafanuzi jinsi Mbegu za Desmodiuma zinavyofanya kazi zikiwa shambani .
Dr Kayeke amesema ataendelea kushirikiana na wakulima wa Namtumbo katika kushirikishana utaalamu wa Kilimo bora anachohitaji mafundisho wanayoyapata yasiishie kwenye mashamba darasa bali elimu waisambaze kwa wengine na kila mmoja aone manufaa kupitia shamba lake.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya namtumbo ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii wa wilaya hiyo katikati akiwa na watgaalamu wa Kilimo kushoto ni Sammy Mwakyusa mratibu wa Mashamba darasa na kulia ni Mtafiti wa Kilimo Dr Juma Kayeke katika Shamba Darasa Namtumbo.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Mtani Martin amesema Technolojia hii ni nzuri hasa kwa wafugaji kwa kuwa ikitumika vizuri hakuna cha kupoteza mkulima ataweza kuvuna kwa tija na upande wa pili atanufaika na chakula cha mifugo, Ameomba wakulima wawatumie wataalamu ipasavyo ili kunufaika na fursa zinazopatikana kupitia kilimo kwa ustawi wa jamii.
Kaimu Afisa Mifugo wilaya ya Namtumbo Said Lwanda amethibitisha umuhimu wa Mabingo bingo na Desmodium kwa mifugo na kwamba mimea hiyo haina madhara yoyote kwa mifugo.
Wataalamu wa Kilimo na Mifugo wa wilaya ya Namtumbo wakiongozwa na Mtafiti wa Kilimo kutoka Mikocheni wakizunguka mashamba darasa kujionea manufaa ya kilimo cha kutumia technolojia ya Sukuma Vuta.
Shamba la Mahindi likiwa limezungukwa na Mimea ya Mabingobingo ili kuzuia viduha waharibifu wa mahindi.
Wakulima wa Mahindi wilaya ya Namtumbo wakipokea Elimu ya Kilimo bora cha kutumia technolojia ya sukuma vuta kupitia mimea ya Desmodium na Mabingo bingo.
Mratibu wa Vikundi vya Mashamba Darasa ya wakulima wila ya Namtumbo Sammy Mwakyusa amewaomba wakulima kuwashirikisha watoto elimu ya kilimo cha kitaalamu ili iwe na tija kwa familia nzima badala ya kushiriki wazazi peke yao kwa kuwa vijana ndio kizazi kinachopaswa kuendeleza kilimo chenye manufaa.
Shamba la Mahindi lililozingatiwa Elimu ya Sukuma vuta kwa kupanda Desmodiuma na Mabingobingo wilaya ya Namtumbo
Dr Juma Kayeke akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa wilaya ya Namtumbo Mtani Martin alipotembelea moja ya mashamba darasa yanayosimamiwa na Dr Juma Kayeke katika kuendeleza zao la mahindi.

WANAKIJIJI WAWEKA MSIMAMO KUHUSU ELIMU MAPOSENI



Wazazi wa vijiji vya Maposeni songea vijijini  wameiomba  Serikali kuingilia kati mtindo wa  vijijana  wanaotelekeza watoto  baada ya kuwazaa na  kuwaachia Wazee ambao umri wao hawawezi kuwalea wajukuu.
 Wazazi hao wameyasema hayo katika Semina iliyoandaliwa na Haki Elimu kutoka Makao Makuu Dar-Es-Salaam, Semina iliyofanyika Maposeni Songea Vijijini na kushirikisha watu 70 kutoka makundi yote ya kijamii.



Wazazi wamesema kumekuwa na mtindo wa Vijana kuzaa na kutelekeza watoto kwa wazee wao huko nikukimbia majukumu serekari kwa sasa ichukue hatua kali kwa vijana  wanao telekeza watoto baada ya kuwa zaa 

makao makuu ya Halimashauri ya wilaya ya Songea Vijijini ambayo ime jengwa Maposeni Songea Vijijini
Mlemavu akijisogeza bkatika ukumbi wa semina ya Haki elimu .Walemavu wameomba kujengewa vyoo ambavyo wata weza kuvitumia pia kuwe na uhamasishaji kwa wazazi wanao waficha walemavu wasipate Elimu


Semina ya marafiki wa Elimu ilijumuisha Wajumbe 70 wakiwemo Wanawake 20 na Wanaume 50 wakiwemo Walemavu, Viongozi wa Dini, Vijana, Wazee na Walimu wa Shule za Msingi.



Afisa Mipango wa Haki ElimuNaomi Mwakilembe  amewaomba wazazi kufuatilia kwa ukaribu  kwa watoto wao kuhakikisha elimu wanayo pewa  niile iliyo lengwa na serekari


Afisa Mipango wa Haki ElimuNaomi Mwakilembe  amewaomba wazazi kufuatilia kwa ukaribu  kwa watoto wao kuhakikisha elimu wanayo pewa  niile iliyo lengwa na serekari

Afisa Mipango wa Fedha kutoka Makao Makuu akiangalia wananchi wavyo weka Mikakati ya kuimarisha Eliumu
Mwenyekiti wa Haki Elimu Mkoa wa Ruvuma Juma Nyumayo akiratibu Semina iliyo jumuisha watu 70


Wadau wa Elimu ambao ni marafiki wa Elimu wameahidi kulinda Elimu kwa kuweka Mikakati ambayo itakuwa Dira kwao.

Afisa Mipango wa Haki Elimu kutoka Makao  makuu ya Halimashau Naomi Mwakilrmbe akitoka kuangalia offisi mpya ya Halimashauri ya wilaya Songea Vijijini

Mwenyekiti wa Haki Elimu Mkoa wa Ruvuma Juma Nyumayo amekemea vikali vitendo vya watoto kupelekwa Nchi jirani kwa ajili ya kufanya Biashara za  Mabaana na Ngono

Monday, March 14, 2016

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ATEUA WAKUU WA MIKOA



                                                                      
                                   TAATIFA HIZI NI KWA HISANI YA TOVUTI YA IKULU

OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
  2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
  4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
  5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
  6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
  7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
  8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
  9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
  10. 10.  Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
  11. 11.  Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
  12. 12.  Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
  13. 13.  Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).

Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016

Saturday, March 12, 2016

MFANYAKAZI WA HOSPITALI YA MKOA WA RUVUMA BENEDICT MLAPONI APOTEA YAPATA MIAKA 10 SASA


 Nimtoto wa Benedict Mlaponi ambaye amebaki kama yatima Emanuel Mlaponi ambaye yuko kidato cha pili hana Mbele wala Nyuma baba yake alitoweka mwaka 2005 .Mirasi ili funguliwa na serekari kuridhia watoto hao pamoja na mama yao kupewa mirathi hiyo sasa hatujui kama ilichukuliwa au ndiyo majipu yanayo tumia Fedha za wajane .Mheshimiwa Rais wangalie Watoto hawa ili waende na kauli ya Hapa kazi
Mtoto Emanueli Mlaponi na Mama yake Mzazi   wakiomba msaada kwa Rais wa Jamuhuri ya Mungano Mh,John Pombe Magufuli kuangalia masilahi ya mirathi ya baba yao ambaye alikuwa mtumishi wa umma katika Hospitari ya Mkoa wa Ruvuma, Mirathi ili pita lakini mpaka sasa familia hii ina endelea kuhangaika hajulikani fedha ime ingia mikononi mwa majipu au kutokana na mtui wakufuatilia hana uzito. Mh.Rais Ingilia kuisaidia Famila hii ili ijulikane serekari ipo
Ndugu Mtazamaji i unayemuona hapo juu anaitwa  Benedict Mlaponi  alikuwa Mfanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma, Alipotea toka 13/10 /2005 mpaka leo hajulikani aliko. 

Mara ya mwisho aliaga kuwa anasafiri kikazi Dar es salaam na alipata Ruhusa kutoka kwa Mkuu wake wa kazi Dr Wella kwa wakati huo, toka wakati huo mpaka leo 2016 hajapatikana na haijulikani kama yuko hai au amekufa.
Benedict Mlaponi ameacha watoto 5 na Mke Angetruda Milinga,  Masikini wa Mungu Benedict Mlaponi  kazini alikokua ameajiriwa bila kujua lililompata wakaandika barua ya kumfukuza kazi.  Mkewe Angetruda Milinga alifungua kesi ya mirathi baada ya kutoa ripoti police na kuona hapatikani Mahakama ikaamuru alipwe fedha ya mirathi lakini Serikali ya Mkoa wa Ruvuma haija weza kufanya hivyo. 
Ombi la Mke na familia kwa watanzania Mumewe alikuwa akifanya kazi Serikalini kwa nini asilipwe mafao ya mirathi wakati kesi ilishapitia na kuthibitika mumewe kafariki kwa mazingira ya kutatanisha.

 Mwisho anamuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumsaidia mjane huyu kwa kuwa sasa ana tegemea nguvu ya Rais ikishindikana aombe uwezo wa Mungu

Wednesday, March 2, 2016

MKUU WA MKOA AELEZA CHANGA MOTO KATIKA HIFADHI YA CHAKULA MKOANI RUVUMA KATIKA KIKAO CHA RCC

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akiongoza kikao cha RCC akieleza kipato cha wastani cha Mwana Ruvuma kuwa ni shilingi  2,082,167 kwa mwaka ikiwa ni ongezeko la asilimia 8% ikilinganishwa na mwaka 2013 ambapo ilikuwa shilingi 1,913,516
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma akielezea kuhusu mkutano wa ujirani mwema na nchi ya msumbiji uliofanyika 18/2/2016 na kudai katika mambo yaliyo zungumuzwa ni pamoja na manyanyaso yanayo fanyika mipakani mwa nchi hizo na jinsi ya kuzuia wahamiaji haramu kwa kulida mipaka inayo pakana na mkoa  Lichinga Nyasa na mikoa ya Mtwara na Ruvuma
Wajumbe wametakiwa kuelimisha wananchi umuhimu wa kuzingatia usafi ili kuendelea kujiepusha na Magonjwa ya mlipuko.
Uzalishaji wa Chakula Mkoa wa Ruvuma katika msimu wa 2014/2015 ulivuka lengo kufikia Tani 1,564,283huku wastani wa mahitaji ya chakula kwa wakazi wa Mkoa wa Ruvuma ni Tani 469,172 ziada ikiwa Tani 1,095,111
Uzalishaji wa Mahindi pekee Mkoa wa Ruvuma msimu wa 2014/2015 mavuno yalikuwa Tani 689,123 sawa na ongezeko la asilimia 17.3 za Hekta zilizolimwa.
Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo msimu huu wa 2015/2016  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema Mkoa umepokea Vocha 234,000 za mbolea ya kupandia na kukuzia na mbegu za mahindi chotara zilizolengwa kuzinufaisha Kaya 78,000 za wakulima. Katika ugawaji wa pembejeo changamoto ni baadhi ya watumishi kujihusisha kukwamisha utekelezaji wa malengo hayo kwa kushirikiana na mawakala wasio waadilifu.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amewataka wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa wa Ruvuma kusimamia ipasavyo suala la pembejeo za kilimo na kuwachukulia hatua wale watakaobainika kuhujumu zoezi hilo lisifanikiwe, sambamba na viongozi wa Vijiji na kata.
Aidha amesisitiza agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuwataka NFRA kuacha kununua mahindi kupitia mawakala badala yake wakanunue vijijini kwa wananchi wenyewe kwa bei itakayoelekezwa na Serikali.
Akizungumzia kuhusu Elimu bure amesema wazazi wanapaswa kulipia nauli za wanafunzi, kulipia magodoro, shuka na vifaa vya usafi binafsi kwa wanafunzi wa Bweni na zenye hosteli za Serikali pia ni jukumu lao kuendelea kujitolea nguvu kazi na mali ili kuleta ustawi wa maendeleo ya shule zilizoko ndani ya Jamii.
Wakuu wa Idara katika Kikao cha Kamati ya Ushauri (RCC) Mkoani Ruvuma
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyasa Jabir Shimweri katika kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Ruvuma kujadili maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma.
Wajumbe wa katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Ruvuma.
Wananchi wametakiwa kutoa hamasa kwa watoto ili wapende kusoma masomo ya sayansi toka wakiwa katika Elimu ya Msingi na kuwawekewa Mazingira mazuri ya kusoma ili wapende sayayansi hali ambayo itasaidi siku zijazo kuondoa changamoto za upungufu wa Walimu wa Sayansi. Hayo yameelezwa na naibu Waziri wa Elimu Mhandisi Stella Manyanya akiwa katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Ruvuma.
Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Ruvuma wakipokea maagizo ya utekelezaji wa Shughuli za maendeleo katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) na namna wanavyopaswa kusimamia utekelezaji huo katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Kilimo na kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa mapato kupitia Rasilimali za Utalii na Madini kwa maslahi ya wananchi wakishirikiana na Wakurugenzi wao. Wakuu hao wametakiwa kuchukua hatua dhidi ya viongozi wanaokiuka maadili ya kazi kwa kupelekea kukwama kwa shughuli yoyote ya maendeleo.
Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Ruvuma wakifuatilia miongozo na mikakati katika kuhakikisha wanatekeleza ipasavyo ulinzi wa mali na usalama wa Raia.
Wajumbe wa Kikao cha kamati ya Ushauri Mkoa wa Ruvuma wameomba Serikali kusimamia suala la Malipo ya wakandarasi wa Maghala ya kuhifadhi chakula hususani ghala la Halmashauri ya wilaya ya Madaba ambalo ujenzi wake umekamilika na tayari limeshaanza kutumiwa katika msimu wa Kilimo wa 2014/2015.
Sekretarieti katika Kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Ruvuma 2016 kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Wajumbe wa Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa wa Ruvuma wameomba wadau kuchangamkia fursa zilizopo za Maendeleo ikiwemo uhifadhi wa Misitu na Mabenki ya Biashara katika kujileta maendeleo na kukuza Pato la kila mwananchi mmoja mmoja.
Wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Ruvuma.
Aidha katika Kikao cha Kamati ya Ushauri wameombwa wadau na wabunge wa mkoa wa Ruvuma kusimamia Maboresho ya Hospitali za Wilaya ili ziweze kutoa huduma bora na kupunguza msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.
Wajumbe wameomba kuangalia upya vyama vya ushirika jinsi vinavyofanya kazi ili viendane na malengo yaliyokusudiwa ya kuboresha hali za wananchi kupitia kilimo na siyo kumdidimiza mwananchi.
Wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya mkoa kutoka sekta zote za maeendeleo Mkoani Ruvuma.
Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya katika Kikao cha Kamati ya Ushauri (RCC) Mkoa wa Ruvuma.
Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Ruvuma wakichambua mada katika kikao cha Kamati ya ushauri ya Mkoa wa Ruvuma wameomba ushirikiano toka kwa wadau wengine wa maendeleo pale inapohitajika kushirikiana katika utekelezaji ama utatuzi wa jambo fulani mfano Jeshi la polisi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani amesema kuna kila sababu ya kuhakikisha utalii wetu wa ndani unapewa nafasi kubwa kwa maslahi ya wananchi wa mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla pia kudumisha tamaduni zetu za asili kasma sehemu ya utalii.
Wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Ruvuma wamesema ni lazima kila mmoja kwa nafasi yake afanye kazi kwa weledi na uadilifu ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.