KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Thursday, August 30, 2012

WAUGUZI NA MADAKITARI WALALA WODI ZA WAGONJWA

Na noel Stephen mpwapwa Dodoma

Baadhi ya watumishi wa idara ya afya wilayani mpwapwa walio ajiliwa
mwezi mei mwaka huu ambao ni manesi na matabibu wanalala kwenye wodi
za wagonjwa kwa muda wa miezi mitatu sasa kutokana na halmashauri
hiyo kuto kuwapatia nyumba na hela za kujikimu.

Kitendo hicho cha aibu na cha uzalilishaji kwa wataalamu hao
ambacho kimetokea kwa muda wa miezi mitatu sasa bila halmashauri hiyo
kuto kutoa majibu yeyote juu ya suala hilo.

Wakiongea na gazeti hili wilayani hapo baadhi ya watumishi hao
wamesema kuwa tangu waajiliwe mwezi mei mwaka huu halmashauri hiyo
iliwaonyesha wodi za wagonjwa kuwa walale kwa muda wakati
wanatafutiwa uataratibu wa malazi lakini mpaka sasa wamekuwa
wakiendelea kulala wodini hapo kama wagonjwa bila mkurugenzi huyo
kuchukua hatua za kuwalipa madai yao wala kuwalipa mishahara yao .

Aidha wamedai kuwa lalamiko hili wamelipeleka mpaka kwa mkurugenzi
mtendaji wa halimashauri hiyo lakini wamekuwa wakipigwa danadana
bila mafanikio, huku wakiambia waje kesho siku zikidi kusonga mbele
na kuendelea kupata shida

Watumishi hao ambao wengi ni manesi na maafisa tabibu ambao waliomba
majina yao yasiandikwe kwenye Blog ya songea Habari kwa usalama wa kazi zao walidai
kuwa tangu wafike katika halmashauri hiyo mwezi mei wanaishi maisha ya
kuomba omba kutokana na kuishiwa pesa za matumizi na inawalazimu
kulala wodini hapo kama wagonjwa huku wengine wakiwa wanategemea chakula kinachopikwa haosptali hapo kwa ajili ya wagaonjwa walio
lazwa hospitali hapo,

Akiongea mmoja wa watumishi hao huku akitokwa na machozi alisema kuwa
tangu waajiliwe wakuu wa idara hiyo na ofisi ya mkurugenzi
wamekuwa wakisingizia mfumo wa sasa wa utoaji malipo kwa watumishi
ujulikanao kama EPICOR unawakwamisha kuweza kuwalipa watumishi hao
kitu ambacho baadhi ya watumishi hao walipingana nacho

P ia wakiongea zaidi walidakuwa baadhi ya watumishi wenzao wa wilaya
zingine walio ajiliwa nao walisha lipwa pesa zao za kujikimu na
tayari walisha anza kupokea mishahara ya ‘ iweje kwa mpwapwa tu
inamaana mpwapwa ndo inatumia epicor ya kwao peke yao”walihoji
watumishi hao .

Akiuliozwa juu malalamiko hayo mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya
wilaya ya mpwapwa FANUEL SENGE alikili kuwepo kwa matatizo hayo na
alisemakuwa mfumo huo wa LONSON ndio imesababisha kushindwa
kuwalipa watumishi hao .

Alipoulizwa kuhusu watumishi hao kulazwa wodi ni kama wagojwa
mkurugenzi h uyo alikanusha alisema kuwa hili halijui isipokuwa
ataongea na mkuu wa idara ambae ni mganga mkuu wa wilaya bwana
MOHAMED PATHAN.

Utafiti uliofanywa na Blog ya Songea Habari hapo wilayani hapo umegundua kuwa
halimashauri hiyo imekosa wataalamu wazuri wa IT kitu kinacho wapelekea baadhi ya watumishi kushidwa kulipa madeni yao na
mishahara kuchelewa kutoka kwa watumishi wote kwa miezi miwili mfululizo sasa kutokana na mfumo huu wa EPICOR.


JUMA NYUMAYO APATWA NA MSIBA MKUBWA SONGEA

Mwandishi wahabari Mwandamizi Juma Nyumayo akiwa kwenye mazishi ya Shemeji yake Mke wa Nasibu katika makaburi ya Mshangano Manispaa ya Songea

Nasibu Nyumayo akiwa anaingia kaburini ili kumzika mke wake ambaye alifarikikatika hospitali ya Mkoa Ruvuma

Ally Jaibu akitoa maelekezo baada ya Mazishi na kuweza kulishukuru jeshi la wananchi wa Tanzania kwa jinsi walivyo weza kushiriki kwa Hali na Mali

Watu wakiendela kuombeza kifo cha mrs Nyumayo huku wakiendelea kumimi nika kushiriki mazishi

Wazikaji wakiwa ndani ya Kaburi kuhakikisha Mwandani umekaa vizuri wakiongozwa na Nasibu Nyumayo mume wa Marehemu

Wanawake walio shiriki eneo la msiba wakikumbuka mwenzao walipo kuwa naye Hai

Waislamu waliswali sala ya Jeneza mbele ya nyumba Mama mzazi wa ukuoo wa akina Nyumayo

Sunday, August 26, 2012

MTOTO AFUNGA NDOA NA MAMA YAKE MZAZI - SONGEA

Umati wa watu uliofurika kwa Mganga wa Jadi Flora Ndembo Namabengo wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma watu wapatao 400 wameomba Serikali ichukue Mkondo wa Sheria pia Mtoto wa Pili wa Mama Kondrada Ngonyani ameomba Serikali ichukue hatua za kisheria dhidi ya condorada ngonyani na joseph Mapunda.
Joseph Mapunda mwenye umuri wa miaka 40 amesema ameweza kuishi kindoa na Mama yake Mzazi Condorada Ngonyani 70 baada ya yeye kukubaliana wenyewe yeye na mama yake mzazi kuishi kindoa kama mume na mke alipo ulizwa Mama alikiri kuwa kweli wameishi kindoa kwa miaka 10 na anampenda Mtoto wake Joseph Mapunda.Mama Condorada Ngonyani mwenye umuri wa miaka 70 ambaye ana ishi kinyumba na mtoto wake watatu wa kumzaa mwenyewe kama Mke na Mume hapo anaonekana akisononeka kwa nini jamii iingilie ndoa yake

Kwa mkoa wa Ruvuma hii ni mara ya kwanza mtoto wa kiume Joseph Mapunda pichani hapo juu kutembea na mama yake mzazi. Wana Ruvuma wanauliza tume jikwaa wapi watanzani hadi kupoteza mila desturi na maadili ya mtanzania pia kukiuka sheria za dini
Joseph Mapunda ana sema upendo ni upendo amempenda mama na anaishi kindoa wamependana nyie watu mnataka nini kwetu ?
Mama Condorada Ngonyani anasema mara baada ya kufariki mume wake Mzee Mapunda alimchagua mtoto wake amrithi baba yake Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Maendelo ya Jamii, Jinsia na wtoto kuangalia kati sheria inayomruhusu Mtoto na Mama Mzazi kuweza kuishi kindoa

Saturday, August 25, 2012

NDOA RAHISI AMBAYO KILA MMOJA ANAWEZA KUIMUDU

Ili kupunguza garama ya arusi bwana harusi ameamua kukodi toroli na bi Harusi kupanda kwenye Baiskeli ,huo ndio ujasilia mali tujaribu kubana matumizi

Thursday, August 23, 2012

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA WAOMBA MSAADA WA ULINZI KATIKA MABWENI YA WASICHANA

Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya wasichana Songea Welinald Riki Liwiki akieleza changamoto zinazo mkuta shuleni hapo ikiwa na bamoja na kuboka kwa wingo.Aidha amesema ingawa wanaume huingia shuleni hapo nyakati za usiku hakuna hata mwanafunzi mmoja aliye wahi kubakwa pia walimu wanasikia tu hawaja wahi kuwa ona wanaume hao

Adam Nindi Songea.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Songea wameiomba Serikali kuwaongezea ulinzi kutokana na kuingiliwa na Wanaume nyakati za usiku.

Mkuu wa Wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana ya Songea Janemary Mwinyikombo amesema tabia ya kuvamia mara mara na wanaume imeongeza hofu ya wanafunzi na kusababisha wanafunzi kushindwa kujisomea nyakati za usiku.

Kiranja Mkuu wa Shule ya sekondari ya wasichana songea Janemary Mwinyikombo akiwa na Katibu Bernadetha Mathew Pamoja na Wanafunzi waliofanyiwa vitendo vya kinyama ikiwa ni pamoja na kuchaniwa nguo kwa wembe na Mwanaume ajulikanaye kwa jina la Ankol .ambaye mara kwa mara huingia kwa njia ya kimazingira wamesema hali hiyo inawakosesha raha shuleni hapo

Wamesema pamoja na wanafunzi kufunga milango na kupigilia misumari kwenye madirisha lakini cha kushangaza wanaume hao huingia na kuchana nguo za wasichana maeneo ya kifuani, wamesema hali hiyo hutokea kuanzia saa 7.00 usiku na pale wanapo ingia wanafunzi hukumbwa na hali ya kushindwa kusema.

Mwalimu Mkuu wa shule ya sekonndari ya wasichana Songea Welinald Riki Liwiki amekiri kuwepo kwa Vitendo hivyo na amesema ameongeza ulinzi, yeye mwenyewe pia anashiriki ulinzi, ameomba Jamii kushirikiana na shule katika kuwafichua watu wanaofanya vitendo hivyo kwa wanafunzi.

Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana songea amesema katika hali ya ulinzi wa usiku kwa kuwa naye hushiriki siku moja alinusurika kuuwawa na mlinzi baada ya mlinzi kufikili yeye ndiye mwanaume anaye waingilia wanafunzi kimazingira

Shule ya sekondary ya wasichana songea kwa miaka miwili mfululizo kumekuwa na vitendo vya wanaume kuwaingilia wanafunzi kimazingira ingawa hali hiyo bado ni tata wanafunzi a secondary ya wasicha wameomba jamii na wazee wa mila kukaa na kuweza kulitatua tatizo hilo vinginevyo itasababisha wanafunzi kuathirika zaidi kisaikolojia jambo litakalo sababisha elimu kuteremuka

Tuesday, August 21, 2012

ALIYE TELEKEZA MTOTO SONGEA AKAMATWA NA JESHI LA POLICE

MamaZawadi Komba aliye mtupa Mtoto mwenye umuri wa miezi 5 katika guba ya Takataka Majengo songea
Mara baada ya kukamatwa na Police alipewa mtoto amnyonyeshe huku akijutia baada ya kudanganywa na Mwanaume
Adamu Nindi, Songea.

Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma limefanikiwa kumtia mbaroni Mama aliyemtupa Mtoto katika Guba ya kutupia takataka eneo la Mitumbani Majengo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma Ana Tembo ameyasema hayo wakati akiwa katika Ofisi ya Polisi wanawake Mkoani Ruvuma amesema Mama huyo ambaye alimtupa Mtoto wa kiume mwenye ummri wa miezi 5 wiki iliyopita amepatikana baada ya msako mkali ulioendeshwa na Jeshi la Polisi.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo amesema Mama huyo alipatikana katika nyumba ya kulala wageni eneo la Majengo akiwa amejificha chini ya uvungu wa kitanda akikimbia mkono wa Dola.

Jeshi la police lilipo mhoji Zawadi Komba 18 alidai siku hiyo alikuwa akifukuzwa na kichaa ndipo alipo mtupa mtot lakini baada ya kubana na mkono wa sheria ndipo alipo eleza ukweli kuwa alitumbukia katika dimbi la mapenzi

Mama aliyekayekamatwa na Jeshi la Polisi Zawadi Komba18 kwa tuhuma za kumtupa mototo wake na kutaka kuhatarisha maisha ya motto kwa kuliwa na Mbwa, amesema yeye alidanganywa na Mwanaume kuwa angeweza kumuoa endapo angemtupa mototo halafu wangekwenda kuishi Mkoani Mbeya.

Wadau mbalimbali wa Mtandao wa Polisi Wanawake, wakiwakilishwa na Fadhili Chacha wameshauri Wanawake wajishughulishena katika Biashara mbalimbali badala ya kutegemea Wanaume pia wajitahidi kuingia katika mpango wa uzazi wa mpngo ili kuepukana na kubeba mimba bila kutarajia.

Kwa Mkoa wa Ruvuma kuhusu ukatili dhidi ya Watoto hii ni mara ya tano katika mwezi mmoja, tukio la kwanza Baba na Mama walidiriki kumuua Mtoto kwa kumvunja shingo na kumtupa katika daraja la Bombambili, Tukio la Pili Mama mwenyewe na Baba walimuua Mtoto na kumtumbukiza katika sinki la maji taka, tukio la tatu Mtoto alitupwa eneo la Majengo na kuliwa na Mbwa na kubakizwa kichwa, watoto wengine wawili waliweza kuokolewa akiwemo na Mtoto mmoja ambaye alitupwa eneo la Msikitin

Sunday, August 19, 2012

WAISLAMU WAASWA KUDUMISHA AMANI NA KUFUATA MAAMURISHO YA MWENYEZI MUNGU KWA KUTENDA MAMBO MEMA

sheikh mkuu wa Bakwata Mufiti Issa Bin Shaban Simba akitoka inje ya ukumbi baada ya Kuhutubia wananchi katika sherehe za siku ya Iddi iliyo fanyika Mkoani Ruvuma
Dishi la TBC likiwa habarisha wa Tanzania shuguli zote zilizo Fanyika Mkoani Ruvuma katika sherehe za Sikukuu ya Iddi

Watalamu kutoka TBC Wakiwa kazinikuhakisha Picha zinazo pelekwa kwenye setilaiti zinawafikia watazamaji Vizuri hapo wapo Shule ya Wasichana Songea wakati wa Baraza la Iddi lililo fanyika songea Mkoani Ruvuma
Pia TBC kupia njia ya Redio nao walikuwa kazini Hapo Mafundi mitambo wakisiliza usikivu wa TBC 1
Waumini wa wa Dini ya Kiislaamu wakiwa katika ukumbi wa Secondary ya Wasicha Songea kusikiliza ujumbe wa baraza la Iddi Kitaifa
Waumini wanawake wakiskiliza mawadha ya siku ya Iddi katika ukumbiSekondari ya wawasicha Songea
Umati wawatu ulio kuja kumlaki Mufiti wa Bakwata Issa bin Shabani Simba wakati alipowasili mkoani Ruvuma
Maelufu ya Wanaruvuma wakiwa katika viwanja vya Mfaranyaki katika Masijidi Huda kushiriki sala ya iddi iliyo swaliwa Mkoani Ruvuma
Mufiti Issa Bin Shabani Simba akitoka inje ya msikiti wa Masjidi huda baada ya swala ya Iddi iliyo swaliwa Songea Mkoani Ruvuma

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akitoa salamu za serikali amesema utulivu na amani katika Nchi ndiyo njia pekee ya kuifanya Serikali iweze kuleta Maendeleo kwa Wananchi wake.

Sheikh Mkuu Nchini Tanzania Mufti Issa Bin Shabani Simba amewataka waumini wa Dini ya Kiislamu kuendeleza vitendo vyema ili vitendo hivyo viweze ni njia ya kuingia peponi.

Katika Misikiti mbalimbali Mkoani Ruvuma waumini wote kwa ujumla wameiombea Nchi yetu kuwa na Viongozi bora wenye kujali Watanzania na sio kujali Maslai yao.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akitoa salamu za serikali amesema utulivu na amani katika Nchi ndiyo njia pekee ya kuifanya Serikali iweze kuleta Maendeleo kwa Wananchi wake.

Sheikh wa dhehebu la Ahamadiya Mkoa wa Ruvuma Yusufu Kambaulaya amesema wanaruvuma tunatakiwa kumuombea Rais wetu Mh. Jakaya Mrisho Kikwete aendeleze amani kwa Nchi tunazopakana nazo, pia waumini wameomba waislamu washiriki Sensa ya watu na makazi.

Thursday, August 16, 2012

RAIS WA JAMUHURI YA MUNGANO WA TANZANIA DR JAKAYA MRISHO KIKWETE AZINDUA MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII AWAMU YA TATU

Dr Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Rasimi Mfuko wa Maendeleo ya Jamii [TASAF] kwa kubonyeza kitufe kuashiria ufunguzi Jumula ya shilingi bilioni 478 zita tumika katika awamu hii ya tatu

Rais Dr Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi wa Dodoma wakati wa uzinduzi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii awamu ya Tatu [TASAF]

Rais wa jamhuri ya Mungano Dr Jakaya Mrisho Kikwete akiwa jijini Dodoma hapo anaonekana akienda kukagua mabanda ya maonye





Hawo ni mabinti wa Wadzabe wakiwa katika maeneo ya ngorongoro wakingoja mwenge wa uhuru

Wednesday, August 15, 2012

MTOTO ATUPWA JALALANI ENEO LA MITUMBANI SONGEA

Adam Nindi, Songea

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Anna Tembo amewataka wanawake wa Mkoa wa Ruvuma kuwa na huruma kwa watoto wanaowazaa sifa ya kwanza ya mama ni kuwa na upendo na huruma kwa watoto.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Ruvuma Inspekta Anna Tembo ameyasema hayo baada ya Mtoto mmoja mwenye umri wa miezi 5 kutelekezwa kwenye Ghuba ya takataka eneo la Majengo Manispaa ya Songea.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo amesema kitendo cha mtoto mdogo kumtelekeza kwenye jalala ni sawa na Mtoto huyo kuwatupia Mbwa wamle hiyo ni kukosa sifa halisi ya Mama.

Anna Tembo amesema Mtoto huyo wa kiume ambaye aliokotwa kwenye Jalala katika manspaa ya songea Majengo anahifadhiwa na Mama mmoja ambaye amejitolea kumtunza. Mtoto huyo hana nguo, anahitaji chakula ambacho ni Maziwa mwenyekiti amewaomba wasamalia wema wajitokeze kumsaidia kupitia Mtandao wa Polisi wanawake mkoa wa Ruvuma.

. Mama ambaye amejitolea kumtunza Mtoto huyo wa kiume Futuma Ndimbangi amesema usiku wa saa moja jioni aliitwa na shemeji yake na kumtaka aende na taa nje walipofika eneo la tukio walimkuta mtoto akilia kutokana na baridi pia alionyesha kuishiwa nguvu alipo pelekwa hospitali alionyesha kuwa hajala kwa muda mrefu.

Mkoa wa Ruvuma ambao ulisifika kwa huruma kwa wageni na kusifiwa kwa kutunza watoto sasa umeingia kwenye adha ya ukandamizaji kwa kutesa watoto, katika mwezi mmoja zaidi ya watoto 3 wameokotwa na watoto wawili kuuwawa na mama zao ambao kesi zao zipo Mahakamani.

Monday, August 13, 2012

WANDISHI KATIKA ZOEZI LA KUTAMBUA MAENEO YA KUHESABU WATU KATIKA SENSA YA WATU NA MAKAZI

Zoezi la kutambua maeneo ni kazi kubwa waandishi wa Habari wakiwa katika jiji la Iringa kutambua maeneo hapo dada akiwa ameshikilia kichwani baada ya kupanda milima na kuteremuka
Hiyo ndiyo hali halisi ya jiji la Iringa wandishi wakiendelea kutafua alama za uhesabuji hebu angalia Mawe na mabonde yalivyo hiyo ni Iringa
Ndugu yangu kama huja patwa na mkasa katika maisha yako lazima umshukuru mwenyezi mungu ,ndugu unaye mwona hapo juu ni Mwandishi Mkongwe kutoka Mkoa wa Lindi Mussa Chilungo amekuwa mlemavu ghafula alikuwa hapo awali alikuwa anaona lakini sasa ni mpofu.wandishi wahabari walio hudhuria semina ya watu na makaazi wameweza kumchangia shilingi laki nne
Wandishi wakiendelea kutambua maeneo ya kuhesabiwa katika mkoa wa Ruvuma
waandishi 140 kutoka mikoa mbalimbali wakiendelea kutambua maeneo ya sensa na makaazi ya watu

Sunday, August 12, 2012

WAANDISHI WAASWA KUELIMISHA JAMII KUHUSU SENSA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr, Crisitene Ishengoma amesema sensa ya watu na Makazi ni msingi mkubwa wa kuweza kuwaletea maendeleo jamii kuanzia nyanja ya Elimu,Uchumi,Afya na kilimo bila kujua idadi ya watu serekari haiwezi kufanya chochote
Oliva Moto wa Star tv akiwa katika ukumbi wa RUCO akihudhuria semina ya watu na makaazi iliyo fanyika mkoani Iringa
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Crisitine Ishengoma amewataka waandishi wa habari kutumia taluma yao kuelimisha Jamii kuhusu sensa ya watu na makazi ili kulisaidia taifa kuweza kuleta maendeleo kwa kila mtu.
Semina ya sensa ya watu na Makazi kwa wandishi. imejumuisha mikoa ya nyanda za juu kusini ikiwemo mikoa ya Mbeya,Rukwa,Katavi ,Ruvuma,Lindi na Mtwara jumula ya wandishi 140 wameshiriki .
Washiriki wa semina kutoka mkoa wa Ruvuma wakisikiliza kwa makinikuhusu semina ya watu na makaazi mkoani ruvuma
Waandishi wa habari kutoka mikoa saba walio shiriki semina ya hiyo wamesema ili kufanikisha sensa ya watu na makaazi elimu ina takiwa itolewe zaidi kwa wanawake kwa kuwa ziko sehemu msemaji mkuu ni mwanaume asipo kuwepo mwanamke hawezi kusema lolote
Washiriki wa semina ya Sensa na Makazi ya Watu wakiwa katika ukumbi wa RUCO Mkoani Iringa
Waandishi wa Mkoa wa Iringa wakiwa wamepiga picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati wa semina ya sena na makazi ya watu
Wandishi wa Mkoa wa Lindi wakiwa wame piga picha ya Pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Irina Dr Crisitina Ishengoma
Wandishi wa Mkoa wa Mbeya wakiwa na Mkuu wa Mkoa katika Viwanja vya RUCO Mkoani Iringa anaye nyosha kidole ni Mwenyekiti wa Meya Press Club Cristofa Nyanyembe