KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, September 14, 2013

VIONGOZI MBALIMBALI WAKUMBUKE WALIKO TOKA ASEMA MHANDISI VINSENTI NJILA


Mhandisi Vinisent Njila amesema ametoa Msaada huo yeye na mwenzie Joseph Londo wa Jezi za Kike na za kiume pamoja na Mipira miwili wa kike na wa kiume vyote vikiwa na thamani ya Shilingi laki nne (400,000) ikiwa ni moja ya shukrani ya shule hiyo kwa kumpa msingi wa maisha

 Mama mzazi wa Mhandisi Vinsent Njila akielza alivyo pata Tabu katika kumsomesha Mtoto wake lakini amesema Mvumilivu hula Mbivu, Ukiwekeza katika elimu omba Mungu mtoto wako awe kichwa utafaidi amesema mama Mhandisi

Mhadisi wa Umwagiliaji wa Nyanda za Juu Kusini kwa Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma amewaomba wasomio mbalimbali kukumbuka walikotoka kwa kutoa Misaada katika Shule walizosoma.
Mhandisi wa Umwagiliaji Nyanda za Juu Kusini Vicenti Njila ameyasema hayo wakati akitoa Msaada wa Vifaa vya Michezo katika Shule ya Msingi Chiulu aliyosoma mwaka 1970 na kumfanya awe Mhandisi baada ya kumaliza Shule hiyo.


Mhandisi Vinisent Njila amesema ametoa Msaada huo yeye na mwenzie Joseph Londo wa Jezi za Kike na za kiume pamoja na Mipira miwili wa kike na wa kiume vyote vikiwa na thamani ya Shilingi laki nne (400,000) ikiwa ni moja ya shukrani ya shule hiyo kwa kumpa msingi.


Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ya Msingi Chiulu Mwalimu    amesema anashukuru kwa kupata msaada wa Jezi na Mipira hiyo itakuwa chachu ya kuwafanya Wanafunzi wasome kwa bidii ili na wao siku zijazo waweze kutoa Msaada kwa wenzao.

 Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Chiulu katika wilaya ya Nyasa akipokea jenzi kwa ajili ya shule hiyo kutoka kwa Vinsent Njila
 Mhandisi wa Nyanda za juu kusini Vinsent Njila akikabidhi Mpira wa Miguu kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Chiulu wilayani Nyasa
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chiulu akipokie zawadi ya jezi za kiume kutoka kwa Mhandisi Vinsent Njila

Mhandisi Vinisent Njila Amesema inatia aibu kuona wasomi waliosoma Shuleni hapo wakiwa na Maendeleo lakini hawakumbuki walikotoka, hizo ndizo sababu zilizotusukuma kutoa zawadi hizo katika Shule ya Msingi Chiulu

 Baba Mzazi wa Vinsent Njila akieleza changamoto za kusomesha mwanafunzi amesema kusomsha kuna taka moyo hasa kwa sisi tunao ishi pembezoni ambako hakuna miundo mbinu ya biashara, kinacho takiwa ni imani tu, Ndivyo nilivyo fanikiwa kumsomesha Vinsent Njila, Jambo kubwa ni kuepuka na makundi yasiyo jali elimu alimaliza
Ukifika katika Wilaya ya Nyasa Kitoweo kikubwa ni Samaki , hao unao waona ni samaki aina ya Mbufu ambao ni watamu kupita samaki ulio wahi kula

No comments:

Post a Comment