KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Monday, May 25, 2015

KIJANA ANA MTAFUTA BABA YAKE AMBAYE INA SEMEKANA YUKO ARUSHA Nikolaus Mramba



ATT RABEKA MLESI RFA

KIPINDI CHA KUTAFUTA NDUGU:

Raimond Nikolaus Mramba ni kiojana mwenye umri wa miaka 23 Anamtafuta Baba yake Mzazi Nikolaus Mramba. Alipotezana naye miaka ya 1992/1993 akiwa mdogo wakati wakiishi Dar-es-Salaam na Mama yake Edeleana Kalenga wao wakiwa wawili na Mdogo wake Ombeni Mramba.

Amesema Miaka ya 1993 Inadaiwa baba yao huyo Nikolaus Mramba ni mwenyeji wa Moshi Mkoani Arusha aliondoka Dar es – Salaam na kuhitaji kuondoka na wanae ambapo Mama yao hakupenda watoto wachukuliwe na Baba yao , aliamua kuwatorosha Kijijini kwa Mama yao Usokami wilayani Mufindi Mkoa wa Iringa ambako aliwaacha kwa Bibi yao na kurudi tena Dar-es Salaam ambako alikuwa akiishi hadi kifo kilipomkuta mwaka 2011.

Katika kipindi chote wamekuwa wakiishi kwa kuhangaika na Mdogo wake hawana Mtu maalumu wa kuwatunza hawakuweza kuzuru kaburi la mama yao na hawajui Baba yao yuko wapi.

Raimond Nikolaus amejaribu kuhangaika ili aweze kumsaidia mdogo wake asome ameshindwa kufanikiwa kwani alijitahidi kumsomesha hadi kidato cha nne mwaka jana akakwama kumlipia ada ndoto yake ikaishia hapo kwa sasa Yeye mwenyewe Raimond Nikolaus Mramba kwa sasa anaishi Makambi Mjini Songea ambako alikwenda kwa Rafiki yake kwa lengo la kutafuta maisha akijishughulisha na Biashara ndogondogo 

Popote alipo Nikolaus Mramba anatafutwa na wanae Raimond nikolaus Mramba na Omben Nikolaus Mramba awatafute kupitia Redio Free  Afrika Songea Simu namba: 0755 731234/0784731238.  0658 731234

KIJANA HUYU ANA HAMU YA KUENDELEA NA MASOMO YEYOTE AMBAYE ANA WEZA KUMSAIDI MUNGU ATAKUWA NAYE

No comments:

Post a Comment