Chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Mjini kimeishukuru Serikali kwa kutoa kiasi cha Zaidi ya shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya sekta ya Elimu.
Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini James Mgego amesema Zaidi ya shilingi bilioni moja zimetolewa kutekeleza miradi ya miundombinu ya Elimu na vilevile katika Kata ya Mshangano zimetolewa Zaidi ya milioni 800 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya elimu jambo lililoungwa mkono na Diwani wa Kata ya Mshangano Samweli Mbano.
Chama cha Mapinduzi wilaya
ya Songea Mjini kimeweka mikakati ya kutoa hamasa kwa wazazi kuchangia chakula
cha watoto Mashuleni.
No comments:
Post a Comment