KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Monday, June 17, 2013

UTALI WA NDANI ULIOPO KATA YA LIULI WA PASWA KUENZIWA NA WATANZANIA WENYEWE

Mwonekano wa Jiwe la kihistoria kwa ubavuni linalojulikana kwa jina Pomonda lililopo Ziwa Nyasa lililotumiwa kujificha na wananchi wakati wa Vita vya Dunia.
 Viongozi wandamizi wa Shirika lisilo la Kiserikali la RUNECISO wakielekea Katika Jiwe la Pomonda kuona hali ya Pamgo lilipo katika Jiwe hilo ambalo lilihifadhi watu waliojificha wakati wa Vita vya 1 na vya 2 vya Dunia
 Jiwe la POMONDA likionekana kwa nje katika Ziwa Nyasa eneo la Liuli.
 Kivutio kimoja wapo katika Mwambao wa Ziwa Nyasa katika eneo jirani na Jiwe la Pomonda ni Machweo ya Jua (SUNSITE)kama yanavyoonekana pichani kwa mbali
 Jiwe la POMONDA lililopo katika Ziwa Nyasa hapo ni nje ya Pango ambalo kwa ndani lina uwezo wa kuhifadhi watu 250 kwa wakati mmoja hapo ni namna maji kupwa yanavyoonekana pembeni mwa jiwe hilo.
 Katibu Muhtasi wa RUNECISO akiwa katika utalii nyuma ya Jiwe hilo la Pomonda eneo la Ziwa Nyasa akichukua kumbukumbu za Historia ya eneo hilo na Mabadiliko yaliyopo pembeni kushoto kwake ni mti ambao una umri zaidi ya karne moja lakini haukui zaidi ya hapo.
 Ufukwe wa Ziwa Nyasa namna unavyoonekana pichani na kuvutia kwa Madhari ambapo shughuli za kiuchumi kwa Wananchi wa Ziwa Nyasa huzifanya eneo la Mwambao wa Ziwa Nyasa au kuvuka Nchi jirani ya Malawi ambayo imetenganishwa na Ziwa Nyasa.
 Washiriki wa Mdahalo wa Mabadiliko ya HAli ya Hewa uliofanyika Liuli Wilayani Nyasa kwa Ufadhili wa Foundation for Civil Society wakionyesha Jiwe la POMONDA linalovutia watalii mbalimbali wanaokuja kutembelea Ziwa Nyasa.
 Hapo ni Meli ya MV Songea ambayo hutumika kusafirisha Abiria na Bidhaa kutoka Tanzania kuelekea Malawi kupitia Ziwa Nyasa ikiwa imetia Nanga Liuli Ziwa Nyasa
Viongozi waandamizi wa RUNECISO hapo wakiwa ndani ya Jiwe hilo la kihistoria na kivutio cha watalii, picha unayoiona ni ndani ya pango la Pomonda ambalo lina uwezo wa kuhifadhi watu zaidi ya 250 kwa wakati mmoja lililotumiwa kujificha wakati wa vita vya kwanza na vya pili vya dunia ambapo wazalendo wa Kitanzania walikuwa wanajificha. Aliyekaa Chini ni Makamu Mwenyekiti wa RUNECISO na Mwandishi wa Star Tv akiwa amechoka baada ya kupanda kwa shida jiwe hilo hadi kulifikia Pango.
Hizi ni  Nyumba zilizopo katika ufukwe wa Ziwa Nyasa za wakazi wa kawaida wanaofaidi Ufukwe wa Ziwa Nyasa.
Kutoka eneo la Ufukwe mpaka kulifikia Pango hili la Pomonda kuna umbali wa kilometa moja na robo. Pango hili la Pomonda limezungukwa na Miti ya Asili ambayo uneune wake hauzidi robo mita na umri wa miti hiyo yapata miaka 100,pango hili la Pomonda pia limezungukwa na Mawe yenye umbo la Mafiga Matatu kuzunguka eneo hilo mpaka kulimaliza unachukua muda wa saa . Hapo Mwandishi wa Habari Adam Nindi baada ya Kuzunguka katika kulifikia pango hilo inaonyesha jinsi gani alivyochoka akiwa amelala chini. Nilimnukuu akisema "ukistaajabu ya Mussa Utaona na ya Firauni" Nilipomuuliza una maana gani alisema katika maisha yake hakutegemea na wala hakufikiria kama kunaweza kuwa na Pango zuri la kitalii katika Tanzania hii kama hili lililopo eneo la Ziwa Nyasa.
Taarifa zilizotolewa na Wazee waishio katika eneo la Mwambao wa Ziwa nyasa wamesema kipimo cha ujazo wa Maji ya Ziwa Nyasa kujua yanapungua au yanaongezeka ni alama hizo zinazoonekana mistari mieupe na rangi nyeusi kuwa ziwa limepungua maji kwa kiasi kikubwa ambapo awali yalifikia katika mistari inayoonekana kwenye jiwe hilo.

No comments:

Post a Comment