KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, January 25, 2014

SIKU YA MKULIMA NA MAFANIKIO KATIKA KILMO RUVUMA



Mgeni Rasmi katika Sherehe ya Siku ya Mkulima Edes Lukoe sherehe zilizofanyika katika Kijiji cha Nakahuga songea vijijini .kijiji ambacho kimekuwa shamba la Majaribio kwa Mikoa ya Mtwara, Iringa, Mbeya na Ruvuma amewataka wakulima kuzigatia elimu wanayopewa na watalamu ili wapate mafanikio katika kilimo.


Wananchi walioshiriki Siku ya Mkulima katika kijiji cha  Nakahuga wakiongozwa na Mary Ntani wameishukuru Serikali kwa kupewa elimu ambayo imewafanya kupata mavuno mara mbili kuliko hapo awali


Mtaalamu wa Utafiti kutoka Uyole  Deogratus Kisandu amesema Wananchi wa Kijiji cha Nakahuga Songea Vijijini hivi sasa wamepata Mafanikio katika Kilimo cha Mpunga kwa njia ya Umwagiliaji ambapo Hekta moja hutoa Tani 6.5 za Mpunga.



Mtaalamu wa Utafiti kutoka Uyole Mbeya Deogratus Kisandu akiwa katika siku ya mkulima nakahuga songea amesema katika Utafiti uliofanywa umeweza kubaini Mbegu za Mpunga aina ya SARO 5 ina uwezo wa kutoa Tani 8 – 9 kwa Hekta ikipata Matunzo mazuri, hilo limebainika katika Mashamba ya Nakahuga Songea Vijijini.

 Mtalamu kutoka Uyole Deogratus Kisandu akitoa Maelezo jinsi mbegu ya SARO 5 ilivyo onsha mafanikio katika kilimo cha umwagiliaji kakika Bonde la Nakahuga Songea Vijijini
 Kama unavyo mwona Mtoto Erasimo Ntani akicheza Ngoma ya Kitoto katioka siku ya Mkulima Songea Vijijini

Mradi wa umwagiliaji maji Kijiji cha Nakahuga Songea Vijijini ambao umegharimu kiasi cha Sh. Milioni 295,504,200 umewawezesha Wakulima wa Nakahuga kwa mwaka 2013 -2014 baada ya kulima hekari270 wana tarajia kuvuna mpunga Tani 1755 kwa hekari 270

 Wakulima wa Nakahuga Songea Vijijini wakiburudika kwa ngoma ya Kitoto siku ya mkilima iliyo fanyika kijijini Nakahuga
Mgeni Rasimi aliye mwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halimashauri ya Songea Edes Lukoe akikagua shamba la mpunga katika shamba la mpunga nakahuga

Wednesday, January 15, 2014

MIKAKATI YA TENESCO KUHUSU UMEME MKOANI RUVUMA

 Engineer Boniface Njombe akitoa Elimu kwa Wandishi wahabari jinsi Umeme unavyo fanya Kazi akiwa na wafanyakazi wa Tenesco
 Engineer Boniface Njombe akionyesha mashine zilizoko Katika Mtimbo iliyoko Kiblangoma Manspaa ya Songea
 Engineer Boniface Njombe akicheza na Watoto eneo la Magagula Songea vijijini
 Alipo ulizwa jinsi gani anajisikia kucheza na watoto Engineer alijibu kuwa hujisikia vizuri kucheza na watoto kwa kuwa hata yeye alipata malezi mazuri kutoka kwa watu tofautofauti jambo lililo mpa ujasiri alio nao hadi leo


 Changamoto zipo pale unapo taka kitu kizuri hata Asali ni Tamu lakini utengenezaji wake ni mgumu ukiwa uliza nyuki kufika Tulila Chipole ni kazi hapo  Gari la Engineer Boniface Njombe lime kwama katika mlima Magagula songea vijijini ili chukua saa moja kuli kwamua
 Jopo la walatamu wa Umeme kutoka kulia ni Engineer Boniface Njombe anaye fuatia ni Mtawa Hisani Mhagama aliye kati ni Engineer Ake Aurebekk na anaye fuata ni Mhandisi chui na wa mwisho ni msaidizi wa meneja wa Tenesco Songea
 Engineer Ake Aurebekk akionyesha jinsi bwawa la umeme litakavyo jengwa eneo la Tulila

maporomoko ya maji katika mto Tulila yanayo jengwa kwaajili ya uzalishaji Umeme

Waandishi wahabari kutoka vyombo mbambali wakipata chakula baada ya kazi kubwa ya kutembelea mporomoko ya maji katika kijiji cha Tulila  ambayo yana jengwa kwa ajili ya kufua umeme

Thursday, January 9, 2014

NAIBU MKURUGENZI BONIFACE NJOMBE AELEZA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA UMEME MKOA WA RUVUMA

 Naibu Mkurugenzi wa Tenesco Boniface Njombe akiongea na wandishi wa Habari Jinsi Shirika la Tenesco lilivyo jizatiti kuondokana na Tatitizo la Umeme Mkoani Ruvuma. [1].Kufanya matengenezo ya Mara kwa mara kwa Mashine zinapo haribika. [2] Kupanua wigo kwa kuungana na wadau wanao zalisha Umeme katika Mkoa wa Ruvuma kama tulivyo jaza Mkataba na Masista wa Chipole kupata MG 7 za Umeme.[3] Kuunganishwa Umeme wa Taifa kutokea Makambaku kuja Ruvuma akatika uunganishaji huo Vijiji 200 vita Faidika na Umeme wa Taifa ambao haukati ovyo ovyo
 Meneja wa Tenesco Mkoa wa Ruvuma Timoth Ramadhani akiwa katika kikao na waandishi wa Habari amekiri kuwa Mgao wa Umeme Manspaa ya Songea ni changamoto kwake Mali ya Wananchi kukosa umeme kwa wakati mwafaka lakini hata shirika hukosa Mapato ,Ameomba uvumilivu wakati Shirika la Tenesco likitafuta njia ya kuondokana na Tatizo hilo,
Naibu Mkurugenzi wa Boniface Njombe amesema wale wote walio kuwa wakingpja kufungiwa Umeme kwa ukosefu wa Nyaya ,Nguzo Pamoja na Mita hivi sasa Wafanyakazi wa Tenesco wako kazini, Wateja watafungiwa umeme kutokana na jinsi walivyo wahi kulipia

KIKAO CHA USHAURI MKOA WA RUVUMA CHA JADILI UAJIBIKAJI WA TENESCO NA UTENDAJI WA TANCOAL RWANDA


Mbunge wa Namtumbo Mh. Vita Kawawa akishauriana na Mjumbe Mwenziwe  jinsi ya kuweza kuleta Maendeleo katika wilaya ya Namtumbo ambayo kipato chake kina tokana na Kilimo cha Tumbaku
 Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Nyasa Odo Mwisho akihojiwa na Blog ya Songea Haari kuhusu Maendeleo ya Wilaya Mpya ya Nyasa,Changamoto ni Vifaa vya Uvuvi vya Kuvulia Samaki katika Ziwa Nyasa na Mindo Mbinu mibovu ya Barabara kutoka Mbinga hadi Mbambabay
 Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Ruvuma akiwa katika kikao cha Mkoa kusikiliza Mawasilisho kutoka kwa Viongozi Mbalimbali Mkoani Ruvuma
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma akiwa katika kikao cha Bodi ya Barabara kujibu kero zilizopo akiwa kama Mwenyekiti
 Meneja wa Tan road Abrahamu Kishimbo akisikiliza kero zilizopo Mkoa wa Ruvuma Kuhusu Barabara
 Wajumbe wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Ruvuma wakijadili Maendeleo ya Mawasiliano ya Barabara na Changamoto katika wilaya ya Tunduru na Namtumbo kuhusu barabara ambazo hazija Kamilika
 Chares Mhagama akisitiza kuhusu uharibifu wa Barabara pamoja na Kuvunja madaraja ya Njia ya Kitai Lituhi kunako fanywa na Magari ya Kampuni ya Kuchimba Makaa ya Mawe ya Tan Coal
 Mjumbe katika kikao cha ushari cha bodi ya Barabara Chares Mhagama akieleza hasara ya kuweza kuya Ruhusu Magari makubwa kutumia barabara zenye uwezo wa Tani 10 lakini Magari ta Tan Coal hubea mzigo wa Tani zaidi ya 45
 Wajumbe wa RCC wakuu wa wilaya wakisikiliza Maelezo kutoka kwa watoa mada kuhusu Maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma pia Kuchanganua jinsi ya kuondokana na Tatizo la Soko la Mazao na Mgao wa Umeme katika Manspaa ya Songea yenye mahitaji ya MG 8
Naibu Mkurugenzi wa Tenesco Boniface Njombe akiwa katika kikao cha RCC akitoa maelekezo kuhusu changamoto zinazo likabili shirika la Tenesco katika kuwa hudumia wanchi wa Mkoa wa Ruvuma amesema Tatizo la Umeme katika Mkoa wa Ruvuma litaweza kutoweka Mwaka 2015 baada ya Mradi wa Umeme kuunganishwa kutoka Shilika la Masita wa Chipole ambao uta kuwa na uwezo wa MG 8 Pai baada ya kuunga nishwa na Umeme wa Taifa ukitokea Makambako

POLICE RUVUMA WAWEKA MIKAKATI YA KULINDA USALAMA WAWASAFIRI

 Kamanda wa police mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimike akimpongeza Meneja wa Sumatura kwa usimamizi mzuri wa safari za mabasi Mkoani Ruvuma
 Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimike akiendelea kukagua Mabasi yanayo toka na kuingia Mkoani Ruvuma
 Kila Dereva wa Basi nilazima aonyeshe leseni ya Udereva iliyo halisi na siyo kivuli cha leseni ili kujua madereva feki wanao tumia nakala za wenzao
 Meneja wa Sumatura akisimamia utokaji wa Mabasi na kuhakikisha ratiba zinafutwa
 Hii ni kuhakikisha taratibu na kanuni za usalama barabani zina simamiwa vilivyo ili kupunguza Ajali za Barabarani
Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma akipokea Tarifa kutoka Inpekita Fadhili Chacha baada ya kukagua Mabasi ya Endayo Dar -es - Salaam ana kuwa himiza abiria kufunga mikanda na kukemea mwendo wa kasi kwa madereva