KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, January 25, 2014

SIKU YA MKULIMA NA MAFANIKIO KATIKA KILMO RUVUMA



Mgeni Rasmi katika Sherehe ya Siku ya Mkulima Edes Lukoe sherehe zilizofanyika katika Kijiji cha Nakahuga songea vijijini .kijiji ambacho kimekuwa shamba la Majaribio kwa Mikoa ya Mtwara, Iringa, Mbeya na Ruvuma amewataka wakulima kuzigatia elimu wanayopewa na watalamu ili wapate mafanikio katika kilimo.


Wananchi walioshiriki Siku ya Mkulima katika kijiji cha  Nakahuga wakiongozwa na Mary Ntani wameishukuru Serikali kwa kupewa elimu ambayo imewafanya kupata mavuno mara mbili kuliko hapo awali


Mtaalamu wa Utafiti kutoka Uyole  Deogratus Kisandu amesema Wananchi wa Kijiji cha Nakahuga Songea Vijijini hivi sasa wamepata Mafanikio katika Kilimo cha Mpunga kwa njia ya Umwagiliaji ambapo Hekta moja hutoa Tani 6.5 za Mpunga.



Mtaalamu wa Utafiti kutoka Uyole Mbeya Deogratus Kisandu akiwa katika siku ya mkulima nakahuga songea amesema katika Utafiti uliofanywa umeweza kubaini Mbegu za Mpunga aina ya SARO 5 ina uwezo wa kutoa Tani 8 – 9 kwa Hekta ikipata Matunzo mazuri, hilo limebainika katika Mashamba ya Nakahuga Songea Vijijini.

 Mtalamu kutoka Uyole Deogratus Kisandu akitoa Maelezo jinsi mbegu ya SARO 5 ilivyo onsha mafanikio katika kilimo cha umwagiliaji kakika Bonde la Nakahuga Songea Vijijini
 Kama unavyo mwona Mtoto Erasimo Ntani akicheza Ngoma ya Kitoto katioka siku ya Mkulima Songea Vijijini

Mradi wa umwagiliaji maji Kijiji cha Nakahuga Songea Vijijini ambao umegharimu kiasi cha Sh. Milioni 295,504,200 umewawezesha Wakulima wa Nakahuga kwa mwaka 2013 -2014 baada ya kulima hekari270 wana tarajia kuvuna mpunga Tani 1755 kwa hekari 270

 Wakulima wa Nakahuga Songea Vijijini wakiburudika kwa ngoma ya Kitoto siku ya mkilima iliyo fanyika kijijini Nakahuga
Mgeni Rasimi aliye mwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halimashauri ya Songea Edes Lukoe akikagua shamba la mpunga katika shamba la mpunga nakahuga

No comments:

Post a Comment