KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Tuesday, May 16, 2017

WAKULIMA WA NYANDA ZA JUU KUSINI WANUFAIKA NA MRADI WA KILIMO CHA URUTUBISHAJI UDONGO CHINI YA ACTN, RUDI, AGRA NA CRDB

 Mradi wa Kilimo Hifadhi kwa vikundi vya wakulima Vijijini umewanufaisha zaidi ya watu 45,000 katika kipindi cha miaka mitatu 2014/ 2017 katika wilaya za Mikoa ya Ruvuma na njombe.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Shirika la ACTN Deogratias Ngotio wakati wa sherehe za Siku ya Mkulima Shambani zilizofanyika katika Kijiji Litapwasi Songea Vijijini Mkoani Ruvuma.
 Mradi wa Kilimo Hifadhi ni utoaji wa Elimu ya urutubishaji wa Udongo kwa wakulima na wagani kazi ili kujenga uwezo kwa wakulima kuachana na kilimo cha mazoea kisicho na tija na kulima kilimo hifadhi ambacho mkulima hupata tija katika mavuno kwa kupata gunia 20 - 25 kwa hekari.
 Mkulima Kiongozi Sesilia Twitbet Nindi kutoka Kata ya Litapwasi Songea Vijijini akielezea mafanikio ya Elimu waliyoitoa kwa wakulima wa Kata ya Litapwasi katika kufuata Kilimo Hifadhi chenye kurutubisha udongo. Amesema changamoto wanazozipata ni kukosa ushirikiano wa moja kwa moja kutoka kwa viongozi wa Kata na Vijiji kwa kuona kazi wanayoifanya ya kuelimisha wananchi katika kilimo ni kama wanafanya siasa ameomba jamii kuacha kukatisha tamaa wananchi wanapojengewa uwezo katika masuala ya Kilimo kwa kuchanganya na Siasa.
Mratibu wa Shirika la ACTN Deogratius Ngotio amesema katika kipindi cha misimu mitatu ya kilimo cha uteklelezaji wa Mradi wa kuelimisha vikundi vya Wakulima kupitia Mashamba Darasa ya wakulima wameweza kuwafikia watu zaidi ya elfu 45 kupitia mashamba

No comments:

Post a Comment