KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Friday, January 22, 2016

MMKUU WA MKOA WA RUVUMA AWATAKA MAAFISA WA ELIMU KUACHANA NA MICHANGO KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu amewataka Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari kuacha kumfukuza Mmwanafunzi kwa ajili ya kukosa kulipa Michango ambayo wamekubaliana wazazi wenyewe.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu ameyasema hayo baada ya wazazi kumlalamikia kuendelea kwa michango  ya nyuma ambayo ilikuwa ya walinzi pamoja na chakula


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Saidi Thabiti Mwambungu amewataka wazazi wajue kuwa Serikali imetoa msamaha wa ada na siyo wazazi kuwaacha watoto na njaa shuleni ni juu yao kuhakikisha watoto wanapata chakula.


Afisa Elimuj Manispaa ya Songea  Edith Malata Kangomba  amesema katika suala la kuandikisha watoto wenye ulemavu limeeleweka kwa wazazi kwa mwaka huu zaidi ya watoto 200 wameandikishwa ukilinganisha na zamni walivyokuwa wakifichwa majumbani.
Mwenyekiti wa kamati ya Shule ya Msingi Lilambo Osmundi Mwingira ameomba mwongozo kwa Serikali kwa kuwa Wananchi wanadai michango yao ya chakula baada ya Serikali kusema hakuna Michango.

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Jenifa akifafanunua jinsi alivyo jipanga kudhibiti swala la michango mashuleni


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema ni marufuku Walimu wakuu kushiriki katika kudai
Michango ambayo Serikali imekataza, suala la michango ya chakula kuboresha majengo isimamiwe na Wananchi wenyewe  kwa kutumia kamati za shule bila kumuathiri mwanafunzi.

No comments:

Post a Comment