KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, January 30, 2016

BIASHARA HARAMU YA BINADAMU INAYOFANYWA KWA USIRI NCHINI YALAANIWA NA WAUMINI WA UMOJA WA MAKANISA NDUGU - RUVUMA

Askofu wa KKKT Dayosisi ya Ruvuma Askofu Amon Mwenda amesema  Nchi ya Tanzania inaongoza kwa umaskini na kushikilia nafasi ya Tatu Duniani,  pia kwa watoto kuzaa watoto wenzao ni Nchi ya tatu  ukiachana na Biashara ya binadamu inayofanywa kwa usiri mkubwa baina ya pande mbili kwa imani ya kupelekwa katika nafasi nzuri ya maisha ni wajibu wa waumini kutafakari na kuomba juu ya mambo hayo.
 Mapadre na Maaskofu mbalimbali wamepongeza hatua ya Uongozi wa Makanisa ya Anglikan kwa kupinga Ndoa za jinsia moja kinyume na maadili ya kiAfrika wameahidi kuunga mkono jitihada za kulaani kuruhusu uhalali wa ndoa hizo.
 Katika Ibada ya Umoja wa makanisa ndugu mwaka Huu waumini wa Makanisa ya Moravian KKKT, RC na Anglikan mkoani Ruvuma wamemshukuru Mungu kwa kuwezesha Tanzania kumaliza zoezi la Uchaguzi mkuu kwa amani bila kuvuruga amani ya Tanzania.
 Umoja wa Makanisa Ndugu Mkoa wa Ruvuma umepinga Vikali Biashara haramu ya Binadamu inayofanywa na watu wachache wenye uchu wa uchumi wa haraka haraka.

Katibu wa akina Mama wa Umoja wa Makanisa ndugu Mkoa wa Ruvuma Imelda Mbawala amesema kumeibuka Biashara ya Binadamu ambapo Mkoa wa Ruvuma unashika nafasi ya tatu kwa kuuza binadamu kwa usiri mkubwa, Amesema Makanisa yana ushahidi baada ya familia moja kutoroka katika Nchi zinazofanya biashara hiyo .



Katibu wa Akina Mama wa Umoja wa Makanisa ndugu Songea Imelda Mbawala ameyasema hayo wakati wa kuhitimisha siku 9 za maombi ya pamoja ya kuombea amani na kulaani Vitendo vya Ukatili dhidi ya Binadamu, ikiwemo biashara haramu ya binadamu na kupinga ndoa za jinsia moja, Ibada  iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Ruvuma Ushirika wa Songea na kushirikisha Makanisa 4 ya Kikatoliki, 2 ya KKKT, Moravian na   makanisa 2 ya Anglikan.

 Waumini wa Kanisa la Moravian manispaa ya Songea wakimsifu Mungu katika Ibada hiyo ya pamoja ambapo wamekemea roho za ujasusi zikiwemo za Alishababu, na vitendo vya kuashiria uvunjifu wa amani.
Waumini wa Kanisa Katoli Jimbo kuu la Songea wakiwa katika Ibada ya pamoja ya Umoja wa Makanisa Ndugu iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Manispaa ya Songea.

Alipo ulizwa Kaimu Kamanda wa police Mkoa wa Ruvuma Revocatus Malimi  kwa njia ya simu kuhusu uwepo wa biashara haramu ya binadamu mkoani Ruvuma, alisema jeshi la Police lina fanya uchunguzi kuhusu suala hilo
 Lengo la makanisa kuungana pamoja na kufanya ibada za pamoja ni kudumisha umoja na kuondoa tofauti zilizopo kati ya kanisa na kanisa kwa kuwa mungu ni mmoja ambapo katika umoja huo hufanya maombi ya pamoja ya kuliombea Taifa, Viongozi wa Serikali na Mambo yanayoikumba Jamii.
 Waumini wakitafakari Neno katika ibada ya pamoja ya kuiombea Amani ya Tanzania.

Naye Padre Turdo Chuma akitoa mahubiri ameupongeza Uongozi wa Makanisa ya Anglikana kwa kupinga Ndoa za Jinsia moja kinyume na maadili ya kiafrika, amesema wanaunga mkono kwa kuwawekea vikwazo Makanisa ya Marekani yanayounga mkono ushoga
 Mapadre na Wachungaji wa makanisa  ya Kikatoliki, Moravian, KKKT na Anglikana wakiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja huo Padre Nicodemu mbano wa kanisa Katoliki la mtakatifu Mathias Mlumba kalemba Jimbo Kuu la Songea katika Ibada ya pamoja kuhitimisha wiki ya Maombi ya pamoja duniani.
 Askofu wa KKKT Dayosisi ya Ruvuma, Askofu Amon Mwenda kulia akiongoza waumini wa umoja wa Makanisa ndugu katika Ibada ya pamoja iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Songea, katikati ni Naibu Askofu wa KKKT Mchungaji Laurent Ngaoneka
 Bi Helena Kawinga Muumini wa Kanisa la Anglikan Songea Mjini akisoma Somo la kwanza katika Ibada ya Umoja wa Makanisa Ndugu.
 Waumini wa makanisa ndugu Songea wakiwa katika ibada ya pamoja kuhitimisha siku 9 za ibada ya pamoja.
 Waimbaji wa kwaya ya Romanic Katholiki Jimbo kuu la Songea katika Ibada ya umoja wa makanisa ndugu
 Waimbaji katika maombi ya pamoja wakimsifu mungu.
 Katika ibada hiyo ya pamoja waumini waliweza kuombea wagonjwa wanaohangaika na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya tano ajaliwe utawala  bora katika kipindi chake

Umoja wa Makanisa Ndugu Mkoa wa Ruvuma umefanya Ibada kwa siku 9 kwa kupitia kila Kanisa kuombea Amani na kumalizia Kanisa la KKKT kwa kulaani Biashara haramu ya Binadamu na kukemea Ndoa za Jinsia moja.

Monday, January 25, 2016

NBC YA WASAIDIA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA HATARISHI KITUO CHA NIA NJEMA MATOGORO SONGEA


 Taasisi ya Benki ya NBC Tawi la Songea imeamua kutoa sehemu ya mapato yake kwa kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi katika kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi Matogoro Manispaa ya Songea.Pichani ni Sista Aloisia Mbunda (OSB) mlezi wa watoto akiwa na wafanyakazi wa NBC Tawi la Songea.
 Benki ya NBC Tawi la Songea imeamua kutembelea jamii inayoishi katika mazingira hatarishi ili kuwatia moyo watoto wajione kama na wao ni sehemu ya Jamii ya Benki hiyo na wanastahili kuhudumiwa kupitia faida inayopatikana kutokana na watu kupata huduma katika Taasisi hiyo. Pichani Wafanyakazi wa NBC wakiwa katika kituo cha Nia njema cha watoto Yatima Matogoro.
 Watoto wanaoishi katika kituo cha kulea Watoto wanaoishi katika mazingira Hatarishi Matogoro wamesema kituo chao kinakabiliwa na changamoto ya chakula, Sare za shule na Michango ya Hosteli na mahitaji mengine ya shule kama daftari na peni. Wameomba Jamii kuwakumbuka katika misaada mbalimbali ili kuwafanya watimize malengo yao ya kuendelea na elimu.
 Benki ya NBC Tawi la Songea Imetoa Mahitaji yenye thamani ya Shilingi laki nne katiks kituo hicho cha Matogoro. Akikabidhi vifaa hivyo, Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Songea Simon Ntwale amewataka watoto kuzingatia Elimu ili siku za baadae waondokane na utegemezi  na kuwa mfano kwa jamii.
 Benki ya NBC imekuwa ikisaidia vituo mbalimbali vya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, hivyo jamii nyingine inapaswa kuiga mfano huo badala ya kutumia pesa nyingi kwa ajili ya starehe na anasa wakati kuna watoto wanalala njaa.
 Meneja wa Benki ya NBC Simon Ntwale amesema msaada walioutoa ni mdogo kwa mahitaji ya watoto katika kituo hicho ambapo pana watoto zaidi ya ishirini wanaosoma sekodari katika shule mbalimbali ni jukumu la kila mwanajamii kuunga mkono hatua hii.
 Watoto wakipokea msaada wameushukuru uongozi wa Benki ya NBC kwa kuwakumbuka wamesema wamejiona na wao kama wako na wazazi pindi wanapotembelewa, wameahidi kuongeza bidii katika masomo wanachoomba ni msaada wa watu wenye mapenzi mema ili waweze kutimiza malengo yao.
 watoto wanaoishi katika kituo cha Matogoro pamoja na kupata elimu na kutegemea misaada ya wahisani pia wanajiendeshea miradi ya ufugaji wa samaki, kilimo cha mahindi na kilimo cha miti ili kusaidia kupata baadhi ya mahitaji kupitia miradi hiyo.
 Helena Kapinga na wenzake wakipokea chakula kutoka kwa wafanyakazi wa Benki ya NBC walipotembelea katika Kituo cha Kulea watoto yatima Matogoro Manispaa ya Songea
 Sista Aloisia Mbunda (OSB) amesema kituo hicho zamani kilikuwa kinategemea wafadhili kutoka Ujerumani Uswis na Newsland ambao walikuwa wakitoa kiasi cha Dola 2000 mpaka 2500 ambazo zilikuwa zikisaidia kuwalipia ada na mahitaji watoto wa shule lakini kwa sasa baadhi ya wafadhili wamepungua baada ya kupoteza maisha hivyo waliobaki wanapata kama dola 800 hadi 1000 ambazo hazikidhi kwa mahitaji ya kituo.
 Kituo cha Nia Njema Matogoro kinachomilikiwa na Sista Aloisia Mbunda (OSB) chini ya Kanisa Katoliki kinachukua watoto wanaomaliza elimu ya Msingi na wanaosoma shule za msingi kuwagharamia mahitaji ya chakula na shule kwa sasa kina watoto ishirini na mbili ambao wako sekondari lakini mpaka sasa baadhi ya watoto  hawajaenda kuripoti shuleni kutokana na kusubiri ada ambapo kwa watoto wote kwa mwaka kituo kinahitaji si chini ya milioni 15 kulipia michango ya hosteli na mahitaji mengine ya shule.
 Watoto waliolelewa katika kituo cha Kulea watoto waishio katika Mazingira Hatarishi Matogoro wapo waliofanikiwa kusomeshwa na sasa wana ajira katika Sekta mbalimbali zikiwemo Jeshi la Wananchi, Manesi , waalimu na wengine Seminari ambapo kwa sasa ni wahudumu katika madaraja ya ushemasi na uchungaji.
 Wafanyakazi wa Benki ya NBC Tawi la Songea wakiwa katika kituo cha Matogoro wameguswa na hali ya kuwasaidika watoto kutokana na mafanikio yanayopatikana kupitia vituo vya kulelea watoto yatima, wamesema walezi wa vituo peke yao hususani masista hawawezi bila jamii kushirikiana na wamiliki wa vituo katika kuwasaidia watoto hao ambao hawana hatia na hawakupenda kuishi katika mazingira hayo.
 Kutoa ni moyo na si Utajiri, hujafa hujaumbika, Ukitoa kwa watu wenye mahitaji maalum kama watoto waishio katika mazingira magumu Mungu atabariki, imezoeleka miaka hii watu huchangia zaidi katika mambo ya starehe kuliko kwa wenye matatizo. Pichani Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Songea, Simon Ntwale akiwa ameshika mfuko wa unga wa kilo 50 ikiwa ni sehemu ya mahitaji waliyoandaa kwa ajili ya kuwakabidhi watoto wanaoishi kituo cha watoto yatima Matogoro Songea.
 NBC iliweza kutoa Magodoro ya kulalia watoto wakati kituo cha Nia Njema Matogoro kinaanzishwa na mpaka sasa wamekuwa wakikitembelea mara kwa mara, pia wametembelea na vituo vinegine vikiwemo kituo cha Yatima cha Chipole Songea Vijijini na Kituo cha Mkuzo Manispaa ya Songea.
 Sista Aloisia Mbunda (OSB) alipotembelewa na Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Songea kwa lengo la kuwafariji watoto wanaoishi katika Mazingira Hatarishi.
Sista Aloisia Mbunda (OSB) Msimamizi wa watoto wanaoishi katika Mazingira Hatarishi Matogoro Songea akiwa na wafanyakazi wa Benki ya NBC Tawi la Songea walipotembelea kituoni hapo.

Friday, January 22, 2016

WANANCHI WA KIJIJI CHA CHIULU WILAYANI NYASA WAWATAKA VODA COM KUWALIPA USHURU WA KUJENGA MNARA KATIKA ENEO LAO

Mwenyekiti wa kijiji cha Chiulu wilayani Nyasa ameuomba uongozi wa vodacom kuweza kuwalipa ushuru wa kujenga mnara katika kijiji hicho. Amesema zaidi ya miezi sita sasa hawaja pata ushuru wa ujenzi wa mnara huo wameomba uongozi wa Voda Com kuonana na uongozi wa kijiji cha chiulu kumaliza changamoto zao

MMKUU WA MKOA WA RUVUMA AWATAKA MAAFISA WA ELIMU KUACHANA NA MICHANGO KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu amewataka Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari kuacha kumfukuza Mmwanafunzi kwa ajili ya kukosa kulipa Michango ambayo wamekubaliana wazazi wenyewe.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu ameyasema hayo baada ya wazazi kumlalamikia kuendelea kwa michango  ya nyuma ambayo ilikuwa ya walinzi pamoja na chakula


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Saidi Thabiti Mwambungu amewataka wazazi wajue kuwa Serikali imetoa msamaha wa ada na siyo wazazi kuwaacha watoto na njaa shuleni ni juu yao kuhakikisha watoto wanapata chakula.


Afisa Elimuj Manispaa ya Songea  Edith Malata Kangomba  amesema katika suala la kuandikisha watoto wenye ulemavu limeeleweka kwa wazazi kwa mwaka huu zaidi ya watoto 200 wameandikishwa ukilinganisha na zamni walivyokuwa wakifichwa majumbani.
Mwenyekiti wa kamati ya Shule ya Msingi Lilambo Osmundi Mwingira ameomba mwongozo kwa Serikali kwa kuwa Wananchi wanadai michango yao ya chakula baada ya Serikali kusema hakuna Michango.

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Jenifa akifafanunua jinsi alivyo jipanga kudhibiti swala la michango mashuleni


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema ni marufuku Walimu wakuu kushiriki katika kudai
Michango ambayo Serikali imekataza, suala la michango ya chakula kuboresha majengo isimamiwe na Wananchi wenyewe  kwa kutumia kamati za shule bila kumuathiri mwanafunzi.