KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Tuesday, August 21, 2012

ALIYE TELEKEZA MTOTO SONGEA AKAMATWA NA JESHI LA POLICE

MamaZawadi Komba aliye mtupa Mtoto mwenye umuri wa miezi 5 katika guba ya Takataka Majengo songea
Mara baada ya kukamatwa na Police alipewa mtoto amnyonyeshe huku akijutia baada ya kudanganywa na Mwanaume
Adamu Nindi, Songea.

Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma limefanikiwa kumtia mbaroni Mama aliyemtupa Mtoto katika Guba ya kutupia takataka eneo la Mitumbani Majengo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma Ana Tembo ameyasema hayo wakati akiwa katika Ofisi ya Polisi wanawake Mkoani Ruvuma amesema Mama huyo ambaye alimtupa Mtoto wa kiume mwenye ummri wa miezi 5 wiki iliyopita amepatikana baada ya msako mkali ulioendeshwa na Jeshi la Polisi.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo amesema Mama huyo alipatikana katika nyumba ya kulala wageni eneo la Majengo akiwa amejificha chini ya uvungu wa kitanda akikimbia mkono wa Dola.

Jeshi la police lilipo mhoji Zawadi Komba 18 alidai siku hiyo alikuwa akifukuzwa na kichaa ndipo alipo mtupa mtot lakini baada ya kubana na mkono wa sheria ndipo alipo eleza ukweli kuwa alitumbukia katika dimbi la mapenzi

Mama aliyekayekamatwa na Jeshi la Polisi Zawadi Komba18 kwa tuhuma za kumtupa mototo wake na kutaka kuhatarisha maisha ya motto kwa kuliwa na Mbwa, amesema yeye alidanganywa na Mwanaume kuwa angeweza kumuoa endapo angemtupa mototo halafu wangekwenda kuishi Mkoani Mbeya.

Wadau mbalimbali wa Mtandao wa Polisi Wanawake, wakiwakilishwa na Fadhili Chacha wameshauri Wanawake wajishughulishena katika Biashara mbalimbali badala ya kutegemea Wanaume pia wajitahidi kuingia katika mpango wa uzazi wa mpngo ili kuepukana na kubeba mimba bila kutarajia.

Kwa Mkoa wa Ruvuma kuhusu ukatili dhidi ya Watoto hii ni mara ya tano katika mwezi mmoja, tukio la kwanza Baba na Mama walidiriki kumuua Mtoto kwa kumvunja shingo na kumtupa katika daraja la Bombambili, Tukio la Pili Mama mwenyewe na Baba walimuua Mtoto na kumtumbukiza katika sinki la maji taka, tukio la tatu Mtoto alitupwa eneo la Majengo na kuliwa na Mbwa na kubakizwa kichwa, watoto wengine wawili waliweza kuokolewa akiwemo na Mtoto mmoja ambaye alitupwa eneo la Msikitin

No comments:

Post a Comment