KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Saturday, November 28, 2015

WANA RUVUMA WA SHIRIKI KATIKA SIKU KUMI NA SITA ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA KUTOA MICHANGO MBALIMBALI

 Kamishina wa Police ambaye ni Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msekhela  akimukabidhi Mwenyekiti wa Dawati la Police Wanawake Mkude mchango wake kwa ajili ya kuweza kuwa saidia Watoto wanao ishi katika Mazingira Magumu
 Kauli mbiu ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia 2015
 Wageni waalikwa wakipokea salamu za wasanii.
 Maandamano ya Kupinga ukali wa kijinsia unaoendelea katika Jamii siku ya uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukali huo mkoani Ruvuma.
 Mwenyekiti wa Dawati ambaye ni mratibu wakuandaa mipango itakayo weza kufanikisha Maadhimisho ya Siku 16 za ukatili wa kinjinsia Renatus Matias mkude akimuliza fedha zilizo patikana

 Katika vikao mbalimbali watu huweza kuchangia hoja wakati amelala usingizi hapo kiongozi mmpja wa juu ambaye ashugulia na maendeleo ya jamii akitoa hoja huku akiwa akitafakari

 Watoto wanahitaji kuhurumiwa dhidi ya adhabu kali
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maadhimisho ya Siku kumi nasita za kupinga ukatili wa kijinsia Mkoa wa Ruvuma Mwanasheria wa Serikali Renatus Mkude akifafanua mwenendo wa makosa ya kijinsia.

Katika kusheherekea siku kumi na sita za kupinga Ukatili wa Kijinsia Mkoa wa Ruvuma watoto zaidi ya watano walitupwa na watoto watatu kufa baada ya kukosa huduma muhimu.
Mwenyekiti wa Dawati la Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo amesema ukatili dhidi ya Mtoto unatakiwa ushirikiano kwa jamii mzima kutokomeza ukatili huo.
 wadau wa dawati la kupinga ukatili wa kijinsia mkoani Ruvuma.
Mwenyekiti wa Dawati la Police Wanawake Mkoa wa Ruvuma Anna Tembo alitoa vyanzo kwa walemavu wawili ambao mmoja ni mlemavu wa mikono na mmoja ni mtoto ambaye anahitaji msaada wa kufanyiwa oparesheni ya kutoa maji kichwani, amesema tangu Dawati linatoa msaada kidogo lakini anawaomba Wadau mbalimbali kuweza kuchangia walemavu hao

Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela amewataka Wananchi wote kushirikiana na Serikali katika kufichua vitendo vya Ukatili kwa Jamii yote.

 Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Dawati la Kupinga Ukatili wa kijinsia Mwanasheria wa Serikali Renatus Matias Mkude, katikati ni Mama Mdaula Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa siku kumi nasita za kupinga ukatili na kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela.
 wageni waalikwa wakiongozwa na Mgeni Rasmi Mama Mdaula na wageni waalikwa katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa Manispaa ya Songea.
 Watoto wanatakiwa kupewa haki za msingi ikiwa ni pamoja na kulindwa dhidi ya ukatili wa ain yoyote ili waweze kukua ipasavyo
 wanafunzi waliohudhuria katika Uzinduzi wa Siku kumi na sita za kupinga ukatili wa kijinsia.
 wadau mbalimbali wa kupinga ukatili wa kijinsia, Kulia ni Mama Misango mtetezi wa Masuala ya msaada wa kisheria Manispaa ya Songea

Siku kumi na sita za kupinga Ukatili wa kijinsia Mkoani Ruvuma zitaambatana na kutoa misaada katika Vituo vya watoto wanaoishi katika Mazingira hatarishi.

 Katika Uzinduzi wa Siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia Mgeni Rasmi mama Mdaula aliweza kuwahamasisha wanafunzi wapende Elimu na kutambua umuhimu wa Elimu. pichani Mama Mdaula akisalimiana na wanafunzi katika Viwanja vya Makumbusho ya Mashujaa wa Vita vya Majimaji mjini Songea

Mwanasheria mkuu wa Serikali Mkoa wa Ruvuma Renatus Matias mkude alionyesha jinsi Serikali ilivyo makini katika kumlinda mtoto kuanzia akiwa tumboni.


Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa siku kumi na sita za kupinga ukatili wa kijinsia Farida Mdaula ameitaka Serikali kuchukua hatua kali kwa wale wote watakaopatikana na kosa la ukatili wa kijinsia wachukuliwe hatua kali. mgeni Rasmi Farida Mdaula katika sherehe hizo aliweza kulichangia Dawati la Police Wanawake kiasi cha  shilingi Milioni Mbili,

Mwenyekiti wa Dawati la Police Wanawake mkoa wa Ruvuma Anna Tembo aliainisha baadhi ya matukio yaliyofanyika wilayani Mbinga Mtu Mmoja ambaye aliwaua wapwa zake wata  kwakuwa chinja mmoja mmoja na hatimaye yeye mwenyewe kujinyonga.

 Pichani ni Matei Mukuru mlemavu wa mikono akiwa na mwenyekiti wa Dawati la Polisi wanawake Mkoa wa Ruvuma. Matei ni Mtaalamu wa Kunyoa lakini ana changamoto ya kukosa vifaa vya kuweza kumsaidia katika shughuli hiyo. Hivyo anaomba wasamaria wema wamsaidia kiasi cha Tsh laki tisa ili aweze kununua mashine ya kunyolea na jenerata.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela akiwa na viongozi wa Dawati la Poli wanawake katika Ofisi za Dawati la Polisi Mkoa wa Ruvuma.
 Wajumbe wa Dawati la Polisi wanawake Mkoa wa Ruvuma

Katika Siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia Dawati litaweza kutoa Elimu katika Shule za msingi na Sekondari pamoja na kutoa Msaada kwa vituo vya kulelea Watoto yatima wadogo mjini Songea na Songea Vijijini pamoja na kutoa Msaada kwa Mzee Mlemavu ambaye ameshajichongea Jeneza atakalolitumia mara baada ya mungu kumchukua.

Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia mkoa wa Ruvuma wakifuatilia matukio ya uzinduzi wa siku kuminasita za kupinga ukatili wa kijinsia uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa Mahend

Friday, November 27, 2015

WAFANYABIASHARA MKOA WA RUVUMA WATOA MCHANGO WA BATI KWA MKUU WA WILAYA YA SONGEA ILI KUWAPA WAHANGA WALIO EZULIWA NYUMBA ZAO


Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya amesema Serikali inawathamini wafanya Biashara wanaoungana na Serikali katika kutatua Matatizo  ya wananchi kuwa ni wafanya Biashara  werevu.


Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya amewataka wafanya biashara wajue kuwa Serikali inatambua kuwepo kwa wafanya biashara hasa pale wanapoungana na serikali kuwasaidia Wananchi wanapopatwa na Majanga.
Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya ameyasema hayo alipokuwa akipokea bati 112 na misumari ya bati kutoka kwa wafanya biashara wa manispaa ya Songea kwa lengo la kuwasidia wananchi walioezuliwa Nyumba zao na upepo mkali ulioambatana na mvua na kuziacha familia 15 bila kuwa na mahali pa kulala.

 Mkuu wa Wilaya ya Songea akielekeza jinsi yakuimarisha nyumba kabla ya kuezeka amesema haraka haraka au mtu kutaka nafuu ndicho chanzo cha nyumba kuezekwa tofauti. Amesisitiza kuwatumia wahandisi kabla ya kuezeka ,Wahandisi hulipwa Mshahara kwa ajili ya kuwasaidia wananchi elimu waliyonayo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea akipewa Maagizo na Mkuu wa Wilaya jinsi ya Kuwa saidia watu wanao ishi pembezoni ili waweze kuepukana na Majanga, amesema njia moja wapo ni kuwatembelea mara kwa mara na kuona kazi za maendeleo wanazozifanya zifanyiwe marekebisho kabla ya Madhara kutokea.

Mwenyekiti wa Wafanya Biashara Mkoa wa Ruvuma Issack Mbilinyi (Mwilamba) amesema wafanya biashara ni moja ya Jamii, hawawezi kuona watu wanateseka na wao wana pesa wakashindwa kusaidia Jamii bora ni ile inayosaidiwa katika Matatizo.

 Watu wa kijiji cha Nakahegwa wakichukua bati za msaada walizo letewa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya
 Mkurugenzi Mtendaji wa Hlimashauri ya Wilaya ya Songea Sixbet Valentin akiwa na Kaimu Mkurugenzi Weniselia Swai wakibadilishana mawazo ya kuweza kuimarisha uchumi pamoja na kuangalia upandishaji wa mazao ya biashara kama Mahindi,Kahawa na Maharage.
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nakahegwa Songea Vijijini Damiani Sanga akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Songea Beson Mpesya na kutoa shukurani kwa msaada wa Bati walio pewa wananchi wake
Wahanga waliopatwa na Matatizo ya kuezuliwa Nyumba zao katika Kijiji cha Nakahegwa waligala gala chini kushukuru kwa msaada waliopewa na kusema kweli huu ni Utawala wa sasa kazi
 Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Songea Benson Mpesya akiwa na familia ya Mzee Golihama wahanga wa kuezuliwa nyumba zao huko katika kijiji cha Nakahewgwa Songea Vijijini. kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Sixbet Valentine na katikati ni wahanga walioezuliwa nyumba zao Bibi Maria njovu na kijana wake John Matias Goliama.
 Kiongozi bora ni yule anayepaswa kufuatilia kwa karibu matatizo ya wananchi wake anaowaongoza na kushiriki katika kuyatatua. Pichani ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Sixbert Valentine akiwa na watoto wa wazazi waliopatwa na maafa ya kuezuliwa nyumba zao kwa mvua iliyoambatana na upepo katika Kijiji cha Nakahegwa Songea Vijijini ambapo mkurugenzi aliwapa kiasi cha fedha ili wanunue daftari za shule kufidia daftari zilizoharibika kwa kunyeshewa na mvua.

Mkoa wa Ruvuma ni Mkoa ambao unapata Mvua nyingi zinazoambatana na upepo mkali, Mkuu wa wilaya ya Songea Benson Mpesya amewataka wahandisi wa serekari Songea kutembelea wananchi na kuwaelekeza jinsi ya kulinda nyumba zao na upepo kwakufunga Tengo zinazozuia upepo badala ya kuwaacha wakizuia upepo kwa kufunga nyaya za matairi ya Magari.

 Baadhi ya nyumba zilizopatwa na maafa ya kuezuliwa na upepo ulioambatana na mvua katika kijiji cha Nakahegwa kata ya mbinga Mwalule Songea Vijijini.
Uongozi ni utumishi, kitendo cha mkuu wa Wilaya ya Songea Benson Mpesya na kamati yake ya Maafa wilaya kubuni mbinu ya kukusanya michango kwa ajili ya kwenda kuwafariji wahanga walioezuliwa nyumba zao kupitia wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo wafanya biashara waliopo katika eneo lake ni tendo la faraja kwa wananchi ambalo linastahili kuigwa kwa kutumia fursa zilizopo badala ya kutegemea kusubiri mfuko maafa kutoka ofisi ya waziri mkuu.

Sunday, November 22, 2015

MTAZAMO WAWANANCHI KWA RAIS WA JAMUHURI YA MUNGANO WA TANZANIA DR JOHN POMBE MAGUFULI UKOJE

Mungu ndiye mwanzilishi wa kuchagua Viongozi, tunaambiwa mtu wa kwanza aliyetawala Dunia alikuwa Adamu. Utawala wa Adamu ulikuwa wa huruma, Ukatili ulianza pale mtoto wa Adamu  Kaini alipomuua Habil.      Hivyo hivo tunaona Utawala wa Yusufu alikuwa mdogo na nduguze waliamua kumuuza mdogo wao lakini ndiye aliyewaokoa wakati wa njaa.                                                                                                                                                     Hebu tuone Daudi naye alikuwa mtoto mdogo kazi yake kazi yake kubwa ilikuwa kuchunga lakini Mungu alipotaka kuweka mtawala aliamua kumteua Daudi.                                                                                                             Sasa ninachotaka kusema ni jinsi gani Mungu ameweza Kumteua Dr. John Pombe Magufuli kuwa Rais, ni mfano wa Manabii waliopita,  kazi ya Mcha Mungu kuwaonea  huruma watu wanaoteseka. Hata Yesu alipofika Hekaluni alikuta Mafarisayo wakifanya Hekalu la mungu kuwa Soko. Lakini alimwaga vitu vyote na alisema msifanye Nyumba ya Mungu kuwa Soko la Wanyang`anyi.                                                                                              
Hivyo hivyo Rais Magufuli wakati wa kumwapisha Waziri Mkuu Majaliwa Kasim, watu walichanga fedha shilingi milioni 225 ili wafanye Sherehe lakini Rais akaamua kuzipeleka Fedha hizo katika Hospitali ya Taifa ya muhimbili na kuwezesha kununua Vitanda, Magodoro pamoja na shuka, suala kama hilo linahitaji ujasiri.

Hotuba yake aliyoitoa katika Bunge la 11 ameeleza jinsi fedha za Serikali zilivyokuwa zinashindwa kutumika ipasavyo kwa wanyonge, ambapo fedha nyingi zilitumika pasipokujali matatizo ya watanzania. Fedha zilizotumika kwa safari za nje zingeweza kufanya mambo makubwa.

Sasa jee? Mtu katoka CCM ni mchaguliwa wa CCM waliokuwa wanafuja fedha ni viongozi hao  hao wa CCM. Anapowafichua Mafisadi, wala Rushwa tegemeo lake ni nini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hivi sasa anasali sala ya Yesu Msalabani akisema Eloi, Eloi Lamasabakisani, Mungu wangu Mungu wangu kwa nini unaniacha.

Watanzania tujue kuwa Sala hiyo ni sawa wanavyosema Waislamu Ihidina Sita la Mstakimu Silataladhina  Ana mnta wala dhuarimu ghairimu maudhubi wala dhuarimu. Utuongoze katika njia ya watu walionyooka na sio wale walio wakasirikia.

Ndugu zangu, ninachomaanisha Mtu akiomba msaada hatuna budi kumsaidia, Rais wetu anataka silaha kali ya kumsaidia. Vita hii sisi Watanzania wote tuingie madukani kununua Bunduki kuwa Askari wa Rais Mteule wa Awamu ya Tano Dr. John Pombe Magufuli.

Silaha zinazotakiwa ni mkristo kununua Biblia na kuomba kwa Bidii, na Muislamu kununua Kurani Tukufu na kusimamisha sala tano ili Rais afanikiwe katika Vita hii.

Viongozi wanaojitoa kwa moyo wote wanatakiwa kusaidiwa, Miaka zaidi ya 51 iliyopita tulikuwa tukiomba kumpata Rais atakayewasaidia wanyonge, Siku ya kwanza Muhimbili alitoa Pochi yake kutaka kumlipia Bili ya Matibabu Mgonjwa. Jee, hapo huoni kuwa hali hizo zinamkera?

                                                                                                                                                                           
               


 Adam Nindi mkurugenzi wa Blog ya Songea Habri akiwa na Rais wa awamu ya tano Dr John Pombe Magufuli, hii ina maanisha viongozi wa juu walivyokuwa karibu na wananchi wote hata wadogo.
 Rais awamu ya tano Dr. John pombe Magufuli kipenzi cha watanzania akishukuru kwa kumuamini kuongoza watanzani na kuwathibitishia kuwa kwake ni kazi tu.

Rais wa Awamu ya nne Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amejitahidi kuiongoza Nchi mpaka kufikia hali hii tuliyokuwa nayo, Ni nadra kiongozi anayetawala kuweza kukabidhi utawala kwa Amani.   Kwa wastani hakuna mtu asiyekosea isipokuwa Mungu, Maksi ya Dr Jakaya Mrisho Kikwete ni kule kusimamia Amani na Utulivu na ndicho kilio cha Walimwengu wote.


Picha ya hapo juu ni picha inayoonyesha jinsi waandishi walivyokuwa wakiwajibika kutangaza habari za kuweza kuiweka Nchi yetu katika Amani ili Uchaguzi uwe wa Haki na uhuru. Adam Nindi M

 Watanzania ni watu waliokuwa na msimamo wa kuendeleza na kuilinda Amani na utulivu kama inavyojieleza nembo hiyo hapo juu.
Rais Mteule wa Awamu ya Tano alikuwa akitoa mfano wa wazi kuhusu Maendeleo ya Tanzania, alisema barabara za lami zimejengwa wale ambao hawana magari wasingelijua hilo, akitoa mfano mdogo kuwa katika simu unampigia mpenzi wako I Lovw You; hayo ni maendeleo ukilinganisaha na wakati wa TTCL Unakaa foleni mpaka uipate laini kumekucha, hapo Rais akipiga Simu.

Picha iliyo mbele yako ni Adam Nindi akisalimiana na Rais wa awamu ya tatu Benjamin Wiliam Mkapa, hiyo ni ishara ya kuwa Viongozi wa Tanzania wanawajali watu wadogo,  Adam Nindi na Rais Mkapa wapi na wapi lakini huo wote ni upendo.


Adam Nindi akimuuliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu Madini yaliyopo Mkoa wa Ruvuma, Watanzania watafaidika vipi kwa kuwa Mikoa yenye Madini mara zote watu wake wanakuwa wa kwanza kufaidika.


Adam Nindi akiwa na Rais Karume wa  Zanzibar akimuuliza akiuliza jinsi gain atakavyosimamia Muungano wa Zanzibar baada ya kuona watu wachache wakiubeza Muungano, lakini Rais Karume alikuwa imara aliongoza vizuri na mpaka anatoka Muungano ameuacha imara.