KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Tuesday, February 9, 2016

MKUU WA MKOA AKEMEA HUDUMA MBOVU ZA AFYA UPANDE WA VYOO KATIKA HOSPITALI YA MJI MWEMA MANSPAA YA SONGEA


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea kuhakikisha Vyoo vya Hospitali ya Mjimwema na Shule ya Msingi Majengo vinazibuliwa ili kutoa fursa kwa wagonjwa na wanafunzi kutumia vyoo hivyo.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu alichukua hatua hiyo ya kutembelea katika Hospitali ya Mjimwema baada ya kusikia kuwa wagonjwa wanajisaida kwaenye  ndoo au mifuko ya Rambo  na kutupa wanako jua wenyewe.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu ametoa agizo  hilo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  Jenifa Omolo baada ya kuona mazingira machafu yaliyopo katika hospitali ya mji mwema. katika ziara ya kusitukiza hospitarini hapo baada ya kusikia  wagonjwa wanaji saidia kwenye ndoo kutokana na vyoo hivyo kuziba


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma katika Ziara yake kusitukiza  aliyo ifanya   katika Shule ya msingi ya Majengo yenye wanafunzi 470 amebaini shule hiyo kutokuwa na choo na wanafunzi kulazimika kujisaidia vichochoroni na katika nyumba jirani hatari zaidi wengine kujisaidia kandokando ya  mto Ruvuma


Wagonjwa waliopo  katika Hospitali ya Mjimwema Manispaa ya Songea wamesema adha wanayoipata ni pamoja na harufu inayotoka katika vyoo hivyo, wamesema usafi umefanywa baada ya kubaini kuwa Mkuu wa Mkoa anatembelea Hospitarini hapo.

No comments:

Post a Comment