KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Wednesday, August 24, 2011

MKUU WA KITENGO CHA MIPANGO TGNP

Mjumbe wa Mtandao wa Jinsia Tanzani (TGNP ) Liliani Liundi akiandaa mada kwa ajili ya kuwawezesha wana Mtandao wa Ruvuma kuhusu haki za wanawake



Mjumbe wa Bodi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania Liliani Liundi akiratibu maswala ya Jinsia kwa Mkoa wa Ruvuma




Kamanda wa Police Mkoa wa Ruvuma Maiko Kamhanda akitoa tarifa kwa Wandishi wa Habari kuhusu utumikishwaji wawatoto wakike katika nyumba za starehe Nchini Msumbiji kinyume cha sheria






Na Adam Nindi , Songea.

Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma baada ya kutumia wataalamu wake wa Upelelezi wamebaini kuwa watoto walio chini ya Miaka 18 wapo Nchi jirani ya (Msumbiji) wakifanyishwa kazi zilizo kinyume na Sheria za Haki za Binadamu Duniani.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma Maiko Kamuhanda amesema kutokana na mkutano wa Ujirani Mwema uliofanywa kati ya Kamati ya Ulinzi ya Mikoa ya Mipakani Mkoa wa Nyasa Nchini Msumbiji na Mkoa wa Ruvuma Tanzania ulipeana mikakati ya kuzuia biashara haramu ya Madawa ya Kulevya pamoja na kusimamia haki za binadamu pamoja na kulinda haki ya watoto kutofanyishwa kazi katika machimbo na Kumbi za starehe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Maiko Kamhanda amesema kutokana na Mkataba ulio ainishwa kati ya msumbiji na Tanzania hakuna kizuizi kwa Askari wa Tanzania kufanya Uchunguzi wa kulinda na kutetea watoto walio chini ya miaka 18 .watoto kuingia Msumbiji na kufanyishwa kazinikosa

kamanda wa police mkoa wa ruvuma baada ya kuwasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Nyasa imebainika kuwa katika mchimbo ya Turo msumbiji wapo watoto wasiopungua 50 ambao wanafanya kazi katika Majumba ya starehe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma ameiomba Mitandao inayohusika na kusimamia haki za weanawake hasa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kusaidia Polisi kwa kutoa taarifa za vitendo vinavyo wazalilisha wanawake.

Mkoa wa Ruvuma wenye watu wapatao 1, 400,000 kutokana na kuwa na hali mbaya ya Kiuchumi kwa Ukosefu wa Viwanda, baadhi ya wazazi wanawatumia watoto wa kike kama Kitega Uchumi kwa kuwaoza wakiwa na umri mdogo au kuwaruhusu kufanya kazi katika Kumbi za starehe.
Mtandao wa Jinsia Wanawake kupitia TGNP umeanza Mchakato wa Kuzuia Hali hiyo.
MWISHO

No comments:

Post a Comment