KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Tuesday, May 22, 2012

SIKU YA VIPIMO DUNIANI



Adam Nindi Songea

Mawakala wa Vipimo Mkoani Ruvuma kwa Mwaka 2011 – 2012 wameweza kukagua Mizani 9473 na kubaini Mizani 162 zikiwa na ubora na kuzitoza faini ya Shilingi 33 . 603 ,00/=

Hayo yamebainika katika kuadhimisha siku ya Vipimo duniani Sherehe ambayo huadhimishwa kila Mwezi mei kila Mwaka mkoani Ruvuma iliambatana na utengenezaji wa mizani katika hosipitari bure.

Meneja wa wawakala wa Vipimo Mkoni Ruvuma Herold Mneney ameyasema hayo wakati alipokuwa katika Ukaguzi wa Mizani Mbovu katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ambapo Mizani 5 zilibainika kuwa mbovu na kuweza kutengenezwa.

Meneja wa vipimo amesema wafanya biashara wana njia mbali mbali ya kuwaiba wateja wao kwenye mizani kwa ndani hasa wauzaji wa nyama huweka mfupa ambao umewekwa kwa gundi ili kuongeza uzito, wakati mwingine huweka sumaku ili iende haraka yote ikiwa ni lengo la kumwiba mteja wananchi wawe macho na wizi unao tumiwa na wafanya biashara wakiona hilo watoe tarifa kwa wakala wavipimo songea,

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Philis Nyimbi amesema pamoja na kuadhimisha Siku ya Vipimo duniani kuna umuhimu kila Mwananchi kujua uzito wake ili anapopewa dawa ilingane na uzito wake dawa ikiwa pungufu ni madhara na ikiwa nyingi huweza kuleta madhara mwilini.

Nao Wananchi wakiongozwa na Daria Kapinga wamesema wanapata faida kubwa pale wanapojua uzito wao pia inasaidia kujua Maendeleo ya Mtoto anapokuwa Tumboni.

Mkoa wa Ruvuma unapokuwa na upungufu wa Wafanyakazi Mkoa mzima una Wafanya kazi 6 tu. Pia changamoto inayowakabili watu wa Vipimo ni Ukosefu wa Vifaa vya Vipimo vya kisasa upimaji wa Mionzi pia hata vipimo vya kupimia ongezeko la makelele havipo.

No comments:

Post a Comment