KILA WAKATI ANGALIA STAR TV NA KUSIKILIZA RADIO FREE AFRICA Matangazo

UKIWA NA TANGAZO TAFADHALI WA SILIANA NA SISI KWA NAMBA 0755731234 AU 0755061588
Tuna pokea Matangazo ya StarTV na Radio Free Africa. Wasiliana nasi kwa Email: adammzuza@yahoo.com au mzuzanindi@gmail.com | Simu: 0755 731 234 au 0655 731 234   kwa Mawasiliano zaidi unaweza kutumia NO 0755061588 Judith Lugoye ,shuguli zote za blog hii anaweza kukusaidia MATANGAZO , AU HABARI

Wednesday, June 20, 2012

MWANDISHI MKONGWE ATOA USIA SIKU YA KUFA KWAKE



· Abubakar Karsan
Furaha ya kufa bila makuu ni kuzikwa bila sifa na utukufu uliopindukia ubinadamu.Furaha ya kuzikwa kwenye kaburi lisilokuwa na ufahari kiasi ambacho miaka ikipita utakumbukwa kwenye nyoyo ya watu na sio kwenye miundo mbinu ya kifahari,


kaburi ambalo dahari na dahari litaonekana na jina lako,Mungu nijaalie nisizikwe hivo,nizikwe kwa kufukiwa udongo na wala kaburi langu lisiandikwe chochote.


Mungu nijalie niache sifa kwenye mioyo ya watu,sifa zitakazodumu milele,watu ntakaowaacha hawatanitafuta kwenye makaburi bali katika mapindo ya historia ya matendo makuu ya binadamu
·
Abubakar Karsan
Asante Mungu kwa uhai ulionipa kwa miaka hii 51,nimeitumikia hivi:miaka 8 Mwanza Press Club,

miaka 7 Media Council of Tanzania,miaka

12 Mwanza Non Governmental Organization,miaka

3 Non State Actors Support Programme,UTPC naitumikia kwa mwaka wa 7 sasa.Miaka hiyo yote inaingiliana.Kwa miaka 30 iliyobaki nimeweka malengo yafuatayo:


1.Kuijenga UTPC na klabu yake kuwa asasi bora kabisa Duniani

2.Kuchangia kukuza uwezo wa kitaaluma na kipato kwa waandishi wa habari Tanzania

3.Kuwawezesha watoto wangu na mke wangu kuishi maisha bora yenye uhakika

4.Kufa na kuzikwa bila madoido,isirafu au kutukuzwa.MUNGU wangu nijaalie nitimize hayo

No comments:

Post a Comment